Maswali tata kifo cha Mchungaji Mtikila

Maswali tata kifo cha Mchungaji Mtikila

KILICHOTOKEA KWENYE HII AJALI

Hilo eneo lina makunyanzi ya kufa mtu barabarani kwa zaidi ya kilometa kadhaa. Ilikuwa ni alfajiri yenye giza na gari lilikuwa mwendo kasi kwa zaidi ya km 120 kwa saa. Ile gari ni saloon ya kawaida 'small size' na suspension system yake ni kwa barabara za Tokyo sio hiyo iliyodidimia kwa 'axe load inbalance' na low quality bedding.

Walikuwa wanapishana na Lorry, Lorry lilikuwa likiyumbishwa na hayo makunyanzi, dereva hakuona vizuri kwa kuwa Lorry lilikuwa limewasha full light. Na dereva wa ki saloon hakutumia tahadhari ya kupunguza mwendo akaja hivyo hivyo na spidi zake. Kashaambiwa tunawahi ibada na lazima tufike saa by saa mbili jeshi la wokovu.

Aliposhtukia Lorry hili hapa linahama 'lane' kwa kuyumbishwa na hayo makunyanzi ya barabarani akajaribu kukata kushoto ili kukwepa, tairi za kushoto zikapanda kunyanzi mstari( gema) gari ikaserereka na ikatoka mshazari hadi nje na kupinduka.
Dereva wa Lorry kaendelea na safari zake na hata hajui nini kimetokea nyuma yake japo vishindo vingeweza kumshtua.

Kufa ajalini kuna mengi, zile pilika pilika za kupinduka kuna mshtuko, majeraha, umri, mambo ya ufahamu hasa kama ulikuwa usingizini na 'mind' yako ilihama, kuna maamuzi ya Mola n.k, n.k

Onyo;

Hizo ni hisia zangu tu.



images
Z


Ufafanuzi mzuri sana.

Mwakajuzi nikiwa likizoni homeland Tanzania, nilikuwa na safari ya dharura toka Dar kwenda Morogoro na kurudi siku hiyo hiyo kuwahi jioni yake kupanda ndege kurudi ninakoishi.

Niliondoka Alfajiri sana Dar kama saa kumi na moja, ukweli usumbufu wa kipekee niliopata ni yale makunyazi na mibonyeo ya low quality ya barabara alizosimamia Mafuguli.

Kuna sehemu nilipishana na basi la abiria wa mikoani HOOD LIMITED baada ya kuvuka tu lile daraja la Reli baada ya Mto Ruvu kuelekea Morogoro alimanusura nipinduke na kagari nilikoendesha, nilichepuka kulipa site bus nikafikiri barabara za Obama, oh my goodness, niliyumba na bahati nilipunguza speed.

Ajali nyingi huchangiwa na quality mbaya ya barabara anazojisifia Magufuli.
 
Baada ya kifo maneno ni mengi(consipiracy).kwa mtazamo wangu ajali ilisababishwa na usingizi kwa dereva.fuatilia ratiba zao toka Mbeya hadi eneo la ajali.je dereva alipata muda wa kulala?saa 11 alfajiri ni muda hatari sana.ajali nyingi za muda huo husababishwa na usingizi
 
Labda utueleze wewe ulipanga afe kifo cha namna gani?
Nadhan sasa mmeanza kufanya kufuru.
 
Labda utueleze wewe ulipanga afe kifo cha namna gani?Nadhan NA wewe ni sehemu ya muendelezo Wakufuru inayofanywa na wana Ccm Kwa muumba.Endelea tu utapata majibu ya dhihaka yako.

Yani sasa hv wanaccm mmekuwa mkiendesha siasa za matukio. Mmeshapoteana hamna tena ajenda ya msingi. Akina Makamba wapo bize kufunga mambo ya kijinga wakidhan wanaouwezo Wa kuiokoa Ccm.

Mtamaliza kuni Kwa kuchemsha nawe. Mwaka huu ukawa bendara chuma mlingoti chuma NA lazma tutoboe ikulu. Mabadilikoooo....Lowassaaaaaaa, Lowassaaaaaaaa....mabadilikooooo!!
 
Labda utueleze wewe ulipanga afe kifo cha namna gani?Nadhan NA wewe ni sehemu ya muendelezo Wakufuru inayofanywa na wana Ccm Kwa muumba.Endelea tu utapata majibu ya dhihaka yako.

Yani sasa hv wanaccm mmekuwa mkiendesha siasa za matukio. Mmeshapoteana hamna tena ajenda ya msingi. Akina Makamba wapo bize kufunga mambo ya kijinga wakidhan wanaouwezo Wa kuiokoa Ccm.

Mtamaliza kuni Kwa kuchemsha nawe. Mwaka huu ukawa bendara chuma mlingoti chuma NA lazma tutoboe ikulu. Mabadilikoooo....Lowassaaaaaaa, Lowassaaaaaaaa....mabadilikooooo!!
 
Baada ya kifo maneno ni mengi(consipiracy).kwa mtazamo wangu ajali ilisababishwa na usingizi kwa dereva.fuatilia ratiba zao toka Mbeya hadi eneo la ajali.je dereva alipata muda wa kulala?saa 11 alfajiri ni muda hatari sana.ajali nyingi za muda huo husababishwa na usingizi

Hii nayo ni ya kuitizama kwa jicho la tatu kwa kusafiri usiku kucha pasipo kuwa dereva kazoea kusafiri mda huo nayo ni Hatari zaidi pia wachunguzwe Kama walipata nafasi ya kulala mchana kabla ya safari?
 
Mbona kama milango ya gari imefungwa Kwenye picha zote mbili? Na kwA nini picha ni hizi mbili? Kama hakuvaa mkanda sindio angejiumiza zaidi mbona ametoka mzima bila ya impact of colission ?na kama walitoka sheli muda mfupi inakuwaje dereva apate uchpvu na kudai ghafla loli limekuja karibu kupishana nalo na la mbele limesimama.?
Kwa nini wale wa kwenye loli bovu wasije kutoa msaada mapema sana mpaka kumepambazuka?
 
Kwani aligombana na hao tu? Najua wengi kuanzia baba wa Taifa hadi nyumba ya jirani upande wetu wa magharibi...ajali ni ajali
 
Gari haiachi njia na kupinduka kwa sababu ya tairi kupasuka tu. Inaacha nji kwa makosa ya kwenye gari na makosa ya kibinadamu. Hapo ilipoangukia panaonekana ni mbali kidogo na barabar, na hiyo ni dalili ya speed kalu, na kama ni saa 11 alfajiri, ina maana walisafiri usiku, usingizi. Ajali haichagui kuwa ukifanya uzembe, basi kwa sababu wewe nifulani, basi huipati.
 
ALWATAN KIZIGO and Moringe Sokoine1 hivi mnajua jinso barabara ilivyo pale kwenye eneo la ajali au mnapiga chafya tu!? Ili kujenga nguvu ya madai yenu labda kwa kuwa hamkuwepo eneo la ajali basi mngesubiri report ya polisi angalau tupate mwanga kwamba ilikwenda umbali gani nje ya barabara tangu iache barabara kuuu, na je iliburuzika kwa umbali gani, je uharibufu kwenye gari una akisi ajali husika, nani alikaa wapi, Airbag, pia report ya daktari inasemaje.
Kuna vitu na hoja nyingi za kipuuzi zinapelekea mtu kujiuliza je unapoanzisha mahusiano na mtu je huyo mshirika mpya anatakiwa aishi muda gani ndipo afe au apatwe na tatizo? Pia nimejiuliza uharaka wa watu hawa kuandika haya waliyo yaorodhesha, kama mazingira wayajengayo ni ya kweli basi wao watakua wanaujua ukweli na ni wahusika wa mchezo mzima Lizaboni anasema ni aibu mgombea wa uraisi kuwa implicated katika suala hili, hapa inaonyesha dhahiri muwasilishaji alichokilenga, hakulenga utu, zaidibya maslahi katika nyakati hixi.
Pia inabidi IDs mbili zinazotumika hapa JF ziangaliwe nazo ni Moringe Sokoine1 na ya huyu Lizaboni kwa namna Lizaboni alivyomkwoti Moringe Sokoine1 inaonyesha kabisa huenda ni mtu mmoja na hata style ya uwasilishaji ya Moringe inaonyesha si halisi bali ni style inayomficha mtu aliyezoeleka na kufahamika na hili linakuja kuchangiwa na mna muwasilishaji mkuu alivyochagua maeneo ya ku bold akijifanya kuunga mkono 'hoja'.
Lakini eti ninyi mnakimbilia kutoa madai ya kipuuzi kabisa kama watunga hadithi wa bongo movi, nimejaribu tena na tena kujenga picha kwa kutumia hoja zenu but nothing connects. Acheni upuuzi, msilete filam katika mambo siriaz
 
Last edited by a moderator:
Watu wanaopaswa kuulizwa maswali ni wale tu walisafiri naye pia mmiliki wa hilo Gari, si vyema kuwatuhumu Watu pasipo kuwahoji majeruhi pia wakazi wa jirani na pale Ajali ilipotokea, wakihojiwa kwa kina na umakini ndipo tutabaini kiini haswa cha Ajali na kuachana na story za kutunga tunga pasipo kuwa na uhakika wowote.
 
Kama umeangalia taarifa ya habari ya itv jana usiku ungejua chanzo cha ajari ni nini?
Huwez ku judge kifo cha mtu kwa kuangalia eti nguo hajachanika au hajatoka damu kifo katika ajali kinaweza sababishwa na vitu vingi sana ikiwemo mshtuko ama internal wounds ambazo kwa picha moja huwez gundua.
 
Mazingira ya kifo cha Mchungaji Mtikila bado kinatia shaka kuu mbele ya jamii na nachelea kusema huyu Mzee ameuawa na genge la mafisadi ili wafanikiwe kisiasa kwani Mtikila alikuwa ameshakusanya vielelezo vyote vya kuwashughulikia.


1. Jeshi la Polisi Watanzania tunaomba mtusaidie kumuhoji kwa kina huyu mtu anaeitwa Mchungaji Patrick Mgaya. Huyu alikuwa ni mmoja wa waliopata ajali pamoja na marehemu Mtikila. Ikumbukwe kuwa Magaya ni mmoja wa mashabiki muhimu sana wa Mgombea Urais kupitia Ukawa ndg Edward Lowassa.Taarifa za siri zinasema kuwa Mchungaji Mgaya na Mchungaji Mtikila walikutana takribani mwezi mmoja uliopita tu na kwamba kuna wasiwasi kuwa alipewa kazi maaluum ya kuhahakisha amamuua Mtikila.


Taarifa kutoka nyumbani kwa marehemu zinasema kuwa Mchungaji Mtikila akiwa na Mchungaji Patrick Mgaya walianza safari siku ya Ijumaa jioni kwenda mkoani Njombe ambapo waliambatana na madereva wawili ambao Mchungaji Mtikila hakuwafahamu. Aliewafahamu watu hawa wote ni Mchungaji Magaya ambae ndie aliekodisha gari waliokwenda nayo Njombe kupitia kwa Ndg Victor James Manyii ambaye mbali ya kutoa gari aliyokodisha pia alitoa madereva wawili ambao pamoja na Mchungaji Mgaya wao hawakufa isipokuwa Mchungaji Mtikila pekee.


Ajali hii imeacha maswali mengi kuliko majibu. Kwa mfano ukiangalia shingo ya marehemu Mtikila utaona kuna kitu kama kamba ambayo inaweza kuleta tafsiri kuwa ilitumika kumnyonga marehemu. Pili, kwanini mwili wa marehemu hauna hata kovu wala mchirizi wowote wa damu? Je, ni nani alimpiga picha Marehemu Mtikila? Je, Patrick Mgaya ni nani? Kabla kuwa mchungaji alikuwa anafanyakazi gani? Je gari lile lilipinduka lenyewe au liligongwa? Na kama lilipinduka ni kwanini liharibike eneo la mbele pekee?Je Ni chombo gani kilikuwa cha kwanza kumpiga picha na kusambaza kwenye mitandao?


Patrick Mgaya alipopiga simu nyumbani kwa marehemu alisema wamepata ajali na kwamba kulikuwa na majeruhi wengi sana akamaliza kwa kusema mtuombee kisha akakata simu, je, hao majeruhi wengi ni akina nani? Vyombo vyetu vya Ulinzi na Usalama muhojini Mchungaji Patrick Mgaya maana zipo dalili kuwa kuna mengi anayoyafahamu kuhusu tukio hili. Pia fuatilieni uhusiano uliopo kati ya Rais Paul Kagame, Patrick Mgaya na EADWARD LOWASSA. Pia nashauri Jeshi la Polisi kumuhoji mtu anaeitwa Dr. Jean Bosco Ngendahimana ambae anaishi nyumbani kwa marehemu pale Mikocheni.

Wale wote wenye misimo thabiti juu ya kuchukia Rushwa na Ufisadi wachukue tahadhari. Nasema hivyo sababu Humphrey Polepole alivamiwa nyumbani kwake Mbezi na Dkt. SLAA anapokea sms za vitisho. Vyombo vya dola viwe macho.

Mchungaji mtikila alishawahi kuwaandika watu wafuatao kwamba n watu hatari sana

1.innocent mchunku kapilipili
2.francis magege
3.james kabarebe
4.athanas kafurama (very dangerous)
5.mchungaji mgaya

Nashangaa na siamin kama leo ameongozana na mtu anaemjua kuwa n hatari mtu aitwaye mchungaji mgaya
Kwa hiari yake

Kuna kitu kinaendelea hapa

Mtikila kamsema sana kwa nguvu zote kagame na lowasa
Na hawa watu wanakonekshen sana
Na n watu hatari

Majasusi wa kagame wakikuhitaji hata kama uko whitehouse marekan wanakumaliza mara moja
Wanauwezo hata wakuingia nchi yoyote na kutekeleza waliloagizwa
Refer mwaikyusa

The same to lowasa
Refer. Ripot ya mwakyembe kwa IGP kuhusu mpango wa lowasa kutaka kumuua
 
Tena Kamanda Mohamedi Mtoi hakuea hata na kovu la miba lakini kumbe alivunjika pingiri moja ya UTI wa mng'ongo na ikazama ndani ikasabisha kifo! Nilikuwepo mwili ukifanyiwa uchunguzi! Japo watu wa nje wanadai ni uchawi! Mwacheni Mungu afanye kazi yake!
 
Allah ana siri zake kiukwl uyo mtikila cndio alikua akimbeza lowasa mgonjwa atafia watu, Yy mzima Leo yuko wap? Tuwe makin na midomo ye2 jmn
 
Kwani aligombana na hao tu? Najua wengi kuanzia baba wa Taifa hadi nyumba ya jirani upande wetu wa magharibi...ajali ni ajali

Ugonvi wake na Kagame Rais wa Rwanda ni wa siku nyingi hata kugombana na marais pia ilikuwa kawaida tu lakini sidhani hiyo Ajali itakuwa ina Uhusiano wowote na maadui zake wengi, hiyo Ajali kwa Uchunguzi wa kimazingira inaonekana ilitokana na dereva kusinzia kwani kusafiri usiku kucha toka njombe huku pengine dereva hana uzoefu wa kusafiri usiku pia pengine hakuwa amelala mchana kabla ya safari, inapaswa watu watafakari kwa umakini wasikurupuke kupakazia yeyote pasipo kupata maelekezo ya kutosha toka kwa dereva na wale abiria wengine aliokuwa nao kwenye hilo Gari wakati anasafiri.
 
Unaambiwa mchungaji hakufunga mkanda, unategemea angekuwa sawa na wale waliofunga mkanda???
 
Baada ya kifo maneno ni mengi(consipiracy).kwa mtazamo wangu ajali ilisababishwa na usingizi kwa dereva.fuatilia ratiba zao toka Mbeya hadi eneo la ajali.je dereva alipata muda wa kulala?saa 11 alfajiri ni muda hatari sana.ajali nyingi za muda huo husababishwa na usingizi

Mbona tumesikia Madereva walikuwa wawili
 
Back
Top Bottom