Mazingira ya kifo cha Mchungaji Mtikila bado kinatia shaka kuu mbele ya jamii na nachelea kusema huyu Mzee ameuawa na genge la mafisadi ili wafanikiwe kisiasa kwani Mtikila alikuwa ameshakusanya vielelezo vyote vya kuwashughulikia.
1. Jeshi la Polisi Watanzania tunaomba mtusaidie kumuhoji kwa kina huyu mtu anaeitwa Mchungaji Patrick Mgaya. Huyu alikuwa ni mmoja wa waliopata ajali pamoja na marehemu Mtikila. Ikumbukwe kuwa Magaya ni mmoja wa mashabiki muhimu sana wa Mgombea Urais kupitia Ukawa ndg Edward Lowassa.Taarifa za siri zinasema kuwa Mchungaji Mgaya na Mchungaji Mtikila walikutana takribani mwezi mmoja uliopita tu na kwamba kuna wasiwasi kuwa alipewa kazi maaluum ya kuhahakisha amamuua Mtikila.
Taarifa kutoka nyumbani kwa marehemu zinasema kuwa Mchungaji Mtikila akiwa na Mchungaji Patrick Mgaya walianza safari siku ya Ijumaa jioni kwenda mkoani Njombe ambapo waliambatana na madereva wawili ambao Mchungaji Mtikila hakuwafahamu. Aliewafahamu watu hawa wote ni Mchungaji Magaya ambae ndie aliekodisha gari waliokwenda nayo Njombe kupitia kwa Ndg Victor James Manyii ambaye mbali ya kutoa gari aliyokodisha pia alitoa madereva wawili ambao pamoja na Mchungaji Mgaya wao hawakufa isipokuwa Mchungaji Mtikila pekee.
Ajali hii imeacha maswali mengi kuliko majibu. Kwa mfano ukiangalia shingo ya marehemu Mtikila utaona kuna kitu kama kamba ambayo inaweza kuleta tafsiri kuwa ilitumika kumnyonga marehemu. Pili, kwanini mwili wa marehemu hauna hata kovu wala mchirizi wowote wa damu? Je, ni nani alimpiga picha Marehemu Mtikila? Je, Patrick Mgaya ni nani? Kabla kuwa mchungaji alikuwa anafanyakazi gani? Je gari lile lilipinduka lenyewe au liligongwa? Na kama lilipinduka ni kwanini liharibike eneo la mbele pekee?Je Ni chombo gani kilikuwa cha kwanza kumpiga picha na kusambaza kwenye mitandao?
Patrick Mgaya alipopiga simu nyumbani kwa marehemu alisema wamepata ajali na kwamba kulikuwa na majeruhi wengi sana akamaliza kwa kusema mtuombee kisha akakata simu, je, hao majeruhi wengi ni akina nani? Vyombo vyetu vya Ulinzi na Usalama muhojini Mchungaji Patrick Mgaya maana zipo dalili kuwa kuna mengi anayoyafahamu kuhusu tukio hili. Pia fuatilieni uhusiano uliopo kati ya Rais Paul Kagame, Patrick Mgaya na EADWARD LOWASSA. Pia nashauri Jeshi la Polisi kumuhoji mtu anaeitwa Dr. Jean Bosco Ngendahimana ambae anaishi nyumbani kwa marehemu pale Mikocheni.
Wale wote wenye misimo thabiti juu ya kuchukia Rushwa na Ufisadi wachukue tahadhari. Nasema hivyo sababu Humphrey Polepole alivamiwa nyumbani kwake Mbezi na Dkt. SLAA anapokea sms za vitisho. Vyombo vya dola viwe macho.
Kama ni Mchungaji Mtikila, ninayemfahamu mimi, alikuwa na uadui wa kiitikadi na Ccm. Alijua ccm haiwezi kubadilika na hata hakuwa na sababu ya kuizungumzia kwa sababu ndiyo iliyojaa ufisadi, ufirauni na maswala mengi ya ki diplomasia chafu (according to Mtikila), yaliweka makao makuu ccm.
Ukihusisha Kifo cha Mchungaji Mtikila na mauaji, ninashauri uweke akili zako nje ya sanduku la ushabiki wa kisiasa, ulitazame kwa upana sahihi.
Mafisadi nguli wako ccm na hao ndio unapaswa hasa kuwaelekezea huo mfereji unaoutengeneza.
Wahujumu uchumi wako ccm na ndiko wanakolelewa na kufundwa, kwingine kote ni harufu tu.
Umafia uko ccm. Na kama unataka kuwa mkweli, agiza tume huru na vyombo vya kimataifa vije kufanya uchunguzi wa mauti nyingi za kisiasa zilizotokea hapa Tanzania na ya mwisho iwe ya Mchungaji mtikila kama serikali ya ccm itakubali.
Nimepokea taarifa hizi kwa masikitiko makubwa sana kwa sababu nilimfahamu Mtikila na mchango wake mkubwa wa ukombozi kwa Tanzania. Mashaka yaliyokuwa yakiimzunguka kwa mtazamo wa nje, hayakufichika. Lakini sijatoa comment yoyote labda sasa hapa kwa sababu ninatafakari nini kinafuata baada ya hii ajali.
Lakini kabla hujaanza kuropoka kwa masuala ambayo huna hakika nayo, ni vizuri kama Mtanzania, na kwa maslahi mapana ya taifa letu, ukahimiza utulivu. Tanzania inapitia mengi na hata kama ingelikuwa ni ajali ya kusubu, haiwezi kuwa direct kama unavyoweza kuhisi kwa mtazamo wanje. Ni vizuri ukatumia muda wako Kumwomba Mungu, Kuombea taifa letu, kuwaombea viongozi wetu wazalendo na kuomba hekima ya Mungu itawale.
Tunapita katika kipindi kigumu katika historia ya taifaletu.
Nisingependa, tuvurugwe ufahamu kwa lolote linalotokea tuache kumwanadama adui yetu sahihi, tuanze kutupiana mawe na lawama kwa maslahi ya adui.
Kuna ajali za kawaida na kuna ajali za kusubu. Ninaomba utulie, utafakari sana kisha uombe Mungu akupe macho ya Rohoni upate kuona zaidi ya unavyoona kwa sasa.
Ninaomba tunyamaze, tumalize msiba wa Shujaa wetu, mengine kama yapo yatafuata kwa utaratibu na weledi sahihi.