Ndugu ZOMBA.
Ingawa mama hajaja na sijui atakuja lini kujibu, naomba nitofautiane na wewe kwa baadhi ya muono wako, wa kuhusu makazi. Nitaeleza kwa ujumla kwa sababu ya muda, na kusubiri majibu ya profesa Tibaijuka!
Kwanza naomba tuelewe serikali inauzoefu mkubwa sana, katika mambo mengi sana kuliko mtu/kampuni. Sababu serikali inaweza kuajiri mtaalam, kuandaa, kumsomesha na kumpatia exposure ( mfano ndo hata mama na uprof serikali imempeleka kujionea mambo Singapore) mtaalam yeyote mahili, kama itahitaji kufanya hivyo, Serikali imekuwepo kwa muda wa miaka 50 ( baada ya uhuru) hivyo hatuna mtu amefanya kazi 50 Years, ila kabati la wizara limekuwepo na nina amini uzoefu upo kabatini.
Kuhusu kamapuni binafsi, hapana sababu makazi ni mahitaji muhimu sana kwa binadamu. nakumbuka ni moja ya mambo ambao serikali duniani zinafanyia kazi kila siku. Ukisikia mtikisiko wa uchumi mojawapo ya sababu ni hayo mambo ya makazi. Hivyo ili kila mtu aweze kupata makazi stahili na bora serikali lazima ifanye kazi.
Real estate inahitaji mtaji mkubwa, siyo lelemama, ndo maana nilishauri baadala ya kuanzisha benki 3 kwa mwaka huu wa fedha wangeweza kuanzisha Real estate company, kama vipi NHC ijiunge stock market ipate mtaji mkubwa, then isiuze nyumba bali ipangishe na iboreshwe.
Siyo sehemu zote sekta binfsi imefanikiwa, mifano hai ipo siyo tanzania bali hata nchi jirani. Serikali itoe makazi kwa kupangisha, hapo itapanga mji (miji) na kulinda ukuaji wa uchumi wake.
Serikali itumie watalaam wake waliopo, ipange, isimamie mambo yataenda, sekta binafsi ije kujazilizia pale serikali inaona itahitajika na kufanya bei iwe ya kuangalia gharama halisi.
Hapo mwisho (rangi ya blue) mkuu tayari umeona hapo kuna deal, umejipigia pass mwenyewe, yaani wewe unaweza zaidi kuliko serikali? kazi ipo!!!!
0.5 cts
SP