Master PLan ya Mji mpya wa Singapore

Master PLan ya Mji mpya wa Singapore

Why Kigamboni? Nikiangalia Resources zinazokwenda hapo sipati justification.

La swali la msingi, tunataka kufanya Land Reclamation Tanzania? Kwa nini?
Na kama hatuhitaji, kwa nini mlienda kujifunza?


Kuna case moja ya TZ na mikaratusi Australia nayo ilikuwa hivi hivi

walienda kukutana na wawekezaji (wafanyabiashara wa singapore) ili waje kuwekeza TZ, ndo wakaandaliwa na wenyeji wao kwenda kuangalia eneo mojawapo la uwekezaji nchini kwao, kwahiyo siyo kwamba walienda kujifunza land reclamation
 
Pole na safari ndefu Mama Anna; lakini nina mashaka kuhusu uwezekano wa Tanzania kama nchi kupiga hatua kama hiyo ya Singapura!! kwa sababu serikali ya Tanzania ni kinara katika kutunga sheria na kusimamia uvunjwaji wake.

Mathalani; Sheria ya barabara ya 2007; katika utekelezwaji wake kulikuwa na sababu gani Rais JK na PM Pinda kuanza kumpiga vijembe Waziri Magufuli tena hadharani eti aache ubabe; mara awe na subira; mara punguza kasi?!

PM Pinda alisafiri mpaka Chato jimboni kwa Magufuli kwa lengo hilo hilo la kumpunguza kasi waziri Magufuli asitekeleze sheria ya barabara; akamsema katika mikutano ya hadhara!

Je nini kimebadilika na haswa; Mama Anna huoni kuwa yatakusibu yaliyomsibu Magufuli; hapo ulipo tayari tunakuona kama you are no longer your former self! Anna Tibaijuka tuliyemtarajia, tunayemjua wa UN Habitat!!?
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Prof Tibaijuka tafadhali tuwekee humu JF sera inayosimamia mipango miji na pia masterplan za miji yetu km vile DSM,Arusha,Mbeya n,k. Maana wengi wetu hatuzijui na hakuna uhamasishaji na ufuatiliaji ili kuhakikisha mipango miji inafuatwa.

Pili kwa jiji la DSM mambo yameharibika kupindukia nashauri kama kuna nia ya dhati ya kuhamishia m.makuu Dodoma basi utekelezwe haraka ili kuipa unafuu DSM kwa haraka. kwani naamini ukiitoa serikali kuu DSM mji utashrink kwa muda
 
  • Thanks
Reactions: FJM
umefanya vizuri kuja na master plan y a singapore,lakini tofauti ya mipango ya kwetu na wenzetu,wao wanasimamia na kutekeleza mipango yao.sisi siasa tu.yapo mambo mengi ambayo hatukuyafanyia kazi mf mambo ya south south commission,maisha bora,yote haya kutekelezwa.hongera mama umejaribu lkn watakukwamisha kama prof.masau, inauma sana.

Lakini mh. Kwanini mumeshindwa kuboresha huu mji tulionao sasa hivi na munaanza kutafuta mpya wakati bado hamjachelewa? Tunahitaji tuone mabadiliko hapa tulipo sasa, Hizi sheria ndogondogo za miji zinafanya kazi?

Mtu kuweka maeneo ya mjini vibanda, parking ziko ndani ya barabara ukipita maeneo yote ya mjini sehemu za kupita watu na magari zimepakiwa gari na barabara inakua finyu. Majumba mjini yamekua kama magovu je hakuna sheria ya kuwaagiza wamiliki kuyarekebisha kila kipindi inapofika?
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Suala la msingi ni Waziri anakusudia kupata nini kutokana na hiki alichokiandika?

Yeye ndiye msimamizi wa ardhi yote ya Tanzania. Kama sheria hazifuatwi, hakuna nidhamu, kuna matani na mchezo ndio maana miji yetu iko chaotic, anataka sisi tufanyaje wakati yeye mwenye madaraka makubwa zaidi kwenye suala hilo ukiacha rais ameshindwa kuonyesha lolote?

Kwa nini anataka kutubebesha lawama Watanzania na anaacha kuchukua yeye lawama ya kushindwa kufanya kazi zake kwa ufanisi stahiki?

Mkuu naona umesahau kuwa vichwa vya nchi vinakutana hapa JF? mama amekuja kupata mawazo toka kwa Great Thinkers halafu tena unauliza swali kama hilo hapo kwa red!
 
Mmemuuliza mama maswali magumu hadi kakimbia mama hapa JF sio pazuri kabisa
 
Majibu ya matatizo mengi ya Tanzania yamo humu humu nchini. Ujenzi holela unaendelea mbele ya viongozi wetu waliozeoa kukaa ndani ya mashangingi wakifurahia viyoyozi. Hakuna michoro, sijui safari ya kujifunza nje au hata mbiu za uwekeji zitakazo tatua ujenzi holela kama walio kwenye ngazi za kusimamia sheria wataendelea kuwa bubu.

Kinadharia, sipingi hoja ya mama Tibajiuka, ila najiuliza tatizo ni mipango miji? Kwa upande mwingine mama Tibajiuka anaweza kuondoka kwenye hii wizara ya ardhi bila legacy ya kueleweka. So far sijaona mchango/mageuzi wa maana japo amekuwa anaongea mambo makubwa! amepatwa na nini?
 
Mh mama Tiba huitaji kuuliza walioko nje tu. Hata sisi tulioko hapa bongo hatutaki kuwa na mji ambao haujapangika vyema. Kinachotuangusha ni siasa kuingizwa katika utaalamu. Sidhani kama tunahitaji watu wa Singapore kuja kutusaidia kupanga miji yetu.

Kuruhusu ujenzi wa ovyo na kutosimamia mipango yetu haihitaji watu wa nje kutusaidia. Serkali ikiwa makini tunaweza kufanya maajabu kubadilisha majiji na miji yetu; na hata vijijini tunaweza kufanya hivyo. Kinachohitajika ni nidhamu tu kutoka kwa viongonzi na wataalamu tukishirikisha wananchi. bahati mbaya tumebaki walalamikaji tu wote, na waomba kura za wananchi kwa ahadi nzuri na kutosimamia mabo ili tusiwaudhi wapiga kura. Ebu anza wewe kwa kusimamia kikamilifu kubadilisha Dar es Salaam na hasa kwa kujenga 'satellite cities'.
 
Majibu ya matatizo mengi ya Tanzania yamo humu humu nchini. Ujenzi holela unaendelea mbele ya viongozi wetu waliozeoa kukaa ndani ya mashangingi wakifurahia viyoyozi. Hakuna michoro, sijui safari ya kujifunza nje au hata mbiu za uwekeji zitakazo tatua ujenzi holela kama walio kwenye ngazi za kusimamia sheria wataendelea kuwa bubu.

Kinadharia, sipingi hoja ya mama Tibajiuka, ila najiuliza tatizo ni mipango miji? Kwa upande mwingine mama Tibajiuka anaweza kuondoka kwenye hii wizara ya ardhi bila legacy ya kueleweka. So far sijaona mchango/mageuzi wa maana japo amekuwa anaongea mambo makubwa! amepatwa na nini?

Viongozi hao pia wanashiriki katika ujenzi horera. Wengine wana nyumba ambazo mashangigi yao hayawezi kufika!
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Mkuu naona umesahau kuwa vichwa vya nchi vinakutana hapa JF? mama amekuja kupata mawazo toka kwa Great Thinkers halafu tena unauliza swali kama hilo hapo kwa red!

Mawazo gani wakati majibu anayo na amekwisha yaweka?

Afanye kazi yake tuliyomtuma sio ku-play victim

Jengo moja tu lile katoa amri livunjwe hadi leo hii miezi kadhaa ishapita hakuna kilichotokea ikisha anakuja hapa kutueleza kuhusu kuacha matani na mchezo?

Yeye mbona hajauacha huo mchezo na utani akahakikisha alichokiamuru kinatekelezwa?
 
Mama Anna Tibaijuka,

Nakushauri kuwa Serikali ijitowe katika huu mradi na iwawachie "real estate developers" wa Kimataifa, wenye uzoefu wa hizi kazi.

Serikali yetu haina uzoefu wa hizi kazi na historia inatuonesha Serikali imeshindwa ku-manage mradi wowote wa maana wa kibiashara. Hata NHC inawashinda ni uozo mtupu, ilhali majumba yalikuwa ya kudhulumiwa watu.

Ikiwa Serikali imeshindwa kuendesha viwanda vya umma, leo itaweza kuendesha project ya "magnitude" ya jiji? Jiulize.

Tusipoteze wakati, tuwawachie wenye utaalaam, na uzoefu wafanye haya mambo, wazo ni zuri, watendaji hatuna, tuna wizi tu Tanzania.

Leo ni zaidi ya miaka 6 tunasikia hii lelemama ikiimbwa tu, hebu ondoeni ukiritimba muwape wenye uwezo, kama hamjui pa kuwapata mnaweza wasiliana na mimi kwa PM.

well said mkuu
 
Hii habari ya mji wa Kigamboni mbona maneno mengi vitendo sifuri? Yaani mpaka sasa ndio tupo kwenye hatua ya kuahidiwa kusaidiwa na watu wa Singapore! Je, ni aina gani ya msaada tunayotaka? What was our plan kabla wasingapore hawajaahidi kutusaidia? What are the timelines of implementation?

that is nice siasa pembeni utaifa na ukweli kwanza,
 
Uholela unaendekezwa.. fine kuendeleza Kigamboni, vipi kuhusu mji huu wa dar mna mipango gani? mfano huku sinza ujenzi holela umeendekezwa sana watu wamejenga kwenye open space na kuharibu plan ya kata, sasa hata njia hazipitiki inakera sana, imagine mtu anauwezo lakini anajenga gorofa kwenye ka-open space na viongozi wanaona na hawachukui hatua yeyote. pathetic..
 
Hili nalo ni la msingi, anataka kupata nini kwa sred hii. Na kitu kidogo kama jengo limemsumbua kusimamia utekelezaji, vipi kuhusu mpango/project kubwa kama hii yenye wadau wengi zaidi?


Lakini mie bado najiuliza, kwa nini walienda kujifunza hii reclamation?

Mtu hana uwezo hata wa kusimamia jengo moja anataka kutuaminisha araweza mradi wa majengo zaidi ya Mia moja?

Katika thread hii hakuna cha maana alichokisema
 
Ninakaribisha maoni yenu hasa nyie mlio nje na mnaishi katika miji iliyopangwa? Je uholela unavumiliwa au kuendekezwa? Tupe habari.

View attachment 97055

Mama Tibaijuka[/QUOTE]
Pole Mama Tibaijuka kwakuona waliopo nnje ndio wanaexposure yakutosha kukupa mchango juu ya mji wako mpya!sikushangai nikawaida yenu kutengeneza matabaka wakati mnatafuta maoni kwa wanannchi juu ya vitu mnavyoo vipenda viwemtakavyo. siku zote biashara yeyote huangalia nini wateja watataka, ili si kwa serikari yenu. kwani leo unaiata nyumba zetu ujenzi holela wakati mnafikiria kuwalipa watu pesa wakajenge holela kwa sababu hamjawapa viwanja vilivyo kuwa surveyed.sio hilo tuu pia nikawaida yenu kupima mashamba ya wananchi waliojenga ujenzi mnao uita holela na mkawalipa thamani ya chini ukilinganisha na bei yenu yakuwauzia baada yakuvipima.pia kwakuwa nyinyi ndio wenyezamana yakutoa viwanja vilivyo pimwa na istoshe ninyinyi ndio mliohalibu baadhi ya strategic places kwa kupima viwanja vya makazi kwa rushwa ;eneo la soko la feri kigamboni kunanyumba zimejengwa tatu nzuri zote zina hati ya serikari.Nikikuuliza walipataje hati kama hamkula rushwa? sasa huu ndio ujenzi holela. chakukushauri pima eneo lakutosha lisiwe mbali na mji mpya ilinasisi japo tunukie kuwa karibu na ua rose
kisha wapatieni viwanja hivyo ulivyopima watu vya kujenga ujenzi mjarabu lakini sio mnafukuza watu katika maeneo yao ya asiri kwa vijipesa vyenu kidogo kwa madai yakuondoa ujenzi holela bila kujua wataenda kujenga wapi ujenzi wenye mpangilio!. Huko nikuendeleza ujenzi holela na wala hakusaidii kuondoa umasikini ila kujaza matumbo yenu kwa kufuja fedha za miradi mbalimbali na huko nikuendeleza ujenzi holela.watu wa wizara yako wamefaidi sana kwakutudhurumu,kumilikiviwanja vingi kwa magumashi,kujiingiza kwenye miradi isiyowahusu,kutumia madaraka waliyopewa kulazimisha mambo na mengine mengi.Nashauri uwafundishe na mjifunze uzalendo sio kwakula mali na misahada ya yatima.
 
WanaJF

Nilikuwa mmojawapo wa viongozi tulioandamana na Mhe Rais katika ziara yake ya majuzi nchini Singapore. Ninawaletea sehemu ya Master Plan ya mji wao mpya unaojengwa kutokana na kuokoa ardhi baharini (reclamation). Unaona kila kipande cha ardhi mpya kimeshapangiwa matumizi yake na kuwekewa malengo ya majengo yanayotakiwa.

Kupanga ni kuchagua. Kunahitaji nidhamu na hakuna mchezo wala utani. Huwezi kuwa na mji uliopangwa kama unapenda na kuendekeza uholela na vurugu (chaos). Kinachotakiwa ni kushirikisha wadau wote kupanga malengo na viwango baada ya kupata maoni ya wataalam. Wanaoarithirika na kulazimisha kuhama kupisha maendelezo mapya wanalipw fidia stahiki na endelevu.

Anayedai vinginevyo si msema kweli. WaSingapore wamehaidi kutusaidia katika ujenzi wa Mji Mpya wa Kigamboni. Ninakaribisha maoni yenu hasa nyie mlio nje na mnaishi katika miji iliyopangwa? Je uholela unavumiliwa au kuendekezwa? Tupe habari.

View attachment 97055

Mama Tibaijuka
kilimo kwanza imefia wapi?
 
Mama Tibaijuka pole sana na Safari.Tunashukuru kuna ulichojifunza huko Singapore japokuwa tunaamini kwa uzoefu wako uliotoka Nao UN HABITAT lazima utakuwa unajua kuwa TOFAUTI yetu na akina. Singapore haipo kwenye uwepo ama kutokuwepo kwa Master Plan na blah blah nyingine Bali Ulegelege wenu,uvivu,ufisadi na 10% mnazoendekeza Katika kusimamia Mipango mliyojiwekea.
Samahani Hv unajua kwa nini wananchi tunaamua kujenga kiholela? Unafahamu ugumu wa kurasimisha ardhi hapo wizarani kwako? Nina miaka nazungushwa hapo wizarani kwako halafu baadae unanilaumu kwa kujenga kiholela!?/?/
Hivi lile jengo la TANESCO Pale kwenye hifadhi ya barabara sio ujenzi holela? Au ukitoka Uingereza utakuja na majibu? KIFUPI Mama yangu nyie! Ndo Chanzo.
 
69177_157820217583469_4081295_n.jpg
na hii ndio plani ya miji ya Tanzania, sasa mama kwa nini angalau usiunde vikosi jamii kwenye kila kata kama mfano inavyoanzishwa vikundi vya polisi jamii vitavyohakikisha kuwa kila kiwanja kina access the barabara na kuweka kipimo cha chini cha kiwanja. hamuwezi kukaa mnajivunia miji ya wenzenu huku yakwetu inazidi kuhabirika

Aha hapo wapi tz kweli tunaitaji mipango miji mipya yazamani ifumuliwe tupate mupango miji mupya.
 
Mama Tibaijuka,

Wala usishanhgae na kulalamika, wenzetu wanalitazama na kujenga Taifa lao liwe bora kwa Miaka 50-200! Sisi serikali yetu tunalitazama kwa miaka 5 tutaibaje kura!

Mfano#1: Hivi inakuwaje mpaka leo viwanja vya High Density bado vinapimwa chini ya qubic Meter 1000? Utakuta Kiwanja kinapimwa na Halmashauri ya mji 20X30! Baada ya miaka 20 mji unafika eneo hilo unamwambia ajenge ghorofa, matokeo yake vighorofa vinakuwa kama nguzo za umeme, tena hakawezi kwenda juu zaidi ya ghorofa 10 kwa sababu kana base ndogo! Huu ni uchafu mjini. Vighorofa vinaegemeana hata unaweza kusalimiana kwa kupeana mkono na mtu wa ghorofa la pili!

Mfano#2: Angalia ramani za miji, mtu kasoma mpaka ulaya anakuchorea ramani ya mji utafikiri katoka Kintinku jana. Anaminya minya viwanja mpaka barabara inakuwa nyembamba! siku mkitaka kupanua na kujenga barabara ya rami mnaanza kuwabomolea watu vijumba vyao. Kiasi kwamba barabara ina kuwa nyembamba gari kama imatanguliwa na pikipiki, hawezi ku-overtake kwa sababu akijaribu anaingia kwenye lane ya kurudi anaweza sababisha ajali.

Mfano#3: Nchi imeharibika serikali imeshindwa kudhibiti wenye pesa. Sehemu zote zilizokuwa na open-space na viwanja vya michezo vya mashule vimeuzwa. mji umebanana hakuna sehemu za kuchezea watoto na kupumzikia raia, matokea yake watu wanaenda kushinda bar kucheza pool na kulewa! Miji ya watu public open space zinaheshimiwa, sisi huku mtu anajenga mpaka anamaliza na wahusika wapo na mkubwa wao yupo!

Mama AT, tulikuwa na imani na wewe wakati unatoka UNHABITAT, tukasema 'jembe hilo, waliojenga kwenye open space watakiona' lakini sasa hata kale kajengo pacha kaliko uwa watu kamekushinda! Nadhani ulikuwa haujui maana ya "magamba". Utaendelea kutuletea vipicha vya huko na kule lakini magamba yanaendelea kuwa magumu. Badilisha mfumo wa uongozi, jipambanue kuwa wewe ni mwanamke wa shoka, fanya maamuzi magumu! usiitazame Dar peke yake njoo Mwanza tukuonyeshe mitaa iliyo zibwa, viwanja vya michezo na viwanja vya wazi, vilivyo porwa! Mfano, ilipojengwa Magnum lilikuwa ni eneo letu tunachezea tulivyokuwa wadogo, Kiwanja cha michezo cha Mwenge P/S kimemengwa mengwa mpaka kimekwisha nk, nk!
 
Back
Top Bottom