Master PLan ya Mji mpya wa Singapore

Master PLan ya Mji mpya wa Singapore

Kulikuwa na plan ya kujenga mji mpya arusha maeneo ya kisongo plan ikafa arusha na mwanza ni majiji yanayokuwa kwa kasi lakini miundo mbinu na mipangilio bado mibovu,Mheshimiwa tunaomba mtupangie mjia na majiji mapya mfano badala ya kukazana kutengeneza jiji la dar es salaam upya,tengengenezeni jiji jipya la dar es salaam new dar esalaam mtoke njee ya jiji la sasa nakuanzisha jiji jipya tena mkoa wa pwani ikiwezekana maeneo yapo yakutosha.
 
Muheshimiwa wameahidi kutusaidia ama tutawasaidia ? waheshimiwa mnatuangusha kanchi kadogo kama Singapore itusaidie ji nchi kama Tanzania lenye utajiri kuanzia ardhi na mengine mengi ? Tuwache kujidhalilisha tunatakiwa tujipange sio kila kitu msaada hivi tutegemee maendeleo kwa misada mpaka vi nchi kama hivi ?
 
Mama Waziri, napenda uwazi wako kwenye hili

Vipi kuangalia uwezekano wa kumordenize kimara, mbezi, hadi kibamba bila kuathiri kwa kiasi kikubwa existing structures??
 
Profesa nina shida kidogo kwenu. Hivi kwanini ninyi kama wasomi wa nchi hii mliopo kwenye sehemu kama hizo za maamuzi msiwe wakweli wa mambo na kusimamia usawa? Hivi mapori yote tanzania yamekweisha kwenda kuanzisha mradi kama huo? Kwanini mnawasumbuwa watu katika maeneo ambayo wameyajenga hata kama bila mpangilio?
Ningewakubali kama mngechagua pori moja na kuanzisha mji wa mfano na kuweka kila kitu kinacho hitajika nazani ingesaidia hata mkisema basi mnawatoa wana kigamboni kuwapeleka huko itakuwa na maana kidogo. Mamlaka nyingi za kusimamia ujenzi wa makazi bora Tanzania mbona amziwezeshi kusimamia vyema kazi zao? Kama tukiamua kuwa makini Tanzania hasa ninyi viongozi wetu basi naimani kubwa sana maendeleo yatapatikana bila matatizo.
 
Mama " tibaiju" unatuangusha. Muleba tunajua tuna jembe letu, sasa siasa imeanza kukunyanyasa. Hebu itumikie taaluma yako. "Omukazi e-manzi"
 
Mimi huwa siku zote najiuliza uwezo wetu wa kufikili na kupanga mambo. Nadhani sisi Watanzania tuna mapatatizo makubwa. Nchi kama Uingereza (UK nzima ni kama robo ya Tanzania kwa ukubwa, kuna watu zaidi ya 66m sisi ni 46m. Waingereza wana open spaces katikati ya miji zaidi nyingi mno kulinganisha na Dar yetu ambayo ina bustani ya mnazi moja na Magomeni tu (ambayo ni kichaka). Barabara za kwetu ni finyu sana kulinganisha na barabara za wenzetu hasa kwenye motorways. Hapo ndo huwa najiuliza hivi kwetu hao wanaoitwa Town & Rural Planners walisomea nini?
 
Mama Prof Tibaijuka tafadhali tunaomba utoe majibu basi hata ya ujumla kuliko kunyamzaaaaaaaaaaaa kimyaaaaaaaaaa!
 
WanaJF

WaSingapore wamehaidi kutusaidia katika ujenzi wa Mji Mpya wa Kigamboni. Ninakaribisha maoni yenu hasa nyie mlio nje na mnaishi katika miji iliyopangwa? Je uholela unavumiliwa au kuendekezwa? Tupe habari.

View attachment 97055

Mama Tibaijuka


Prof. wazo la Serikali ni zuri sana katika kuuendeleza mji wa Kigamboni.

Lakini ni vyema kama badala ya kutafuta wafadhiri wa kujenga mji katika mfumo mzuri ni heri tuanze na kuboresha huduma za jamii hasa maeneo ya mikoani na vijijini.

Angalia mambo haya katika karne ya 21 na miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika ni aibu tupu!!!

Akina mama Hospitali.jpg

WAGONJWA_ZAHANATI_KISAKI[1]_.JPG

View attachment 97132

Wanafunzi wa darasa la tano katika shule ya msingi Selous wilayani Namtumbo wakiwa darasani.jpg

Wakati hoja za msingi zinapojadiliwa Bungeni, na kupitisha mradi wa mji mpya wa Kigamboni, viongozi wetu tuliowachagua ni hawa wanafanya mambo haya:-

View attachment 97135

View attachment 97136

View attachment 97137

View attachment 97138

Je Tutafika...........Tafakari.........

MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!!!
 
Mama shida ni jinsi usiri ulivyokatika mpango huu wa mji wa Kigamboni! Wananchi hawajui nani mlipaji! hawajui anayepanga bei ni nani! Hivi mama wewe unanyumba yako halafu akaja mtu tuseme serikali akaangalia nyumba yako akaondoka halafu Serikali yenyewe ikawa inasemasema tu Serikali inapesa za kulipa huku tukiambiwa bungeni kuwa serikali imeelemewa na madeni! mama huu ndo utaahira unapoanzia!!

mambo ya kuzidiana kwenye michongo ya udalali wa kwenye nyumba zetu na serikali hiihii tuliyoichagua!
mama mambo ya best of practice inaisha lini mpaka kwenye nyumba zetu!??
 
Kwanza ningependa kuchukua nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Anna Tibaijuka kwa kutushirikisha katika suala hili muhimu. Ni matumaini yangu viongozi wengine wa serikali wataiga mfano huu; kwani, uongozi bora lazima uende samba samba pamoja na kuwashirikisha na kuwasikiliza wale unaowaongoza.

Mheshimiwa Tibaijuka, nasikitika kwamba umefanya wrong diagnosis ya tatizo letu. Ujenzi holela hapa Tanzania hautokani na kukosa master plan bali kutofuatwa kwa sheria. Nitakupa mfano eneo la Mbezi Beach, nakumbuka miaka ya 1984, nilikuwa nikienda sana site na marehemu baba yangu. Nikiwa mtoto mdogo kabisa nilikuwa nikimwona baba na karatasi moja kubwa sana. Kuna siku nilimwuliza baba hiyo karatasi ni ya nini? Aliniambia hii ni master plan ya hili eneo? Nikamwuliza master plan ndio nini? Aliniambia master plan inaonyesha eneo hili litavyokuwa once likishajengwa, akanionyesha eneo ambalo shule, posta, polisi na maeneo ya wazi yatakapokuwa.

Kusema ukweli master plan ilikuwa nzuri na ilionyesha vitu kinagaubaga. Lakini badala ya muda akaja afisa mmoja wa ardhi ambaye namkumbuka kwa jina la Setumbi (nalikumbuka jina lake mpaka leo kwani baba alikuwa akilalamika sana kuhusu huyu mtu).Akaanza kuuza na kugawa viwanja kiholela; na mbaya zaidi, kuyagawa maeneo yote ya wazi. Walipomaliza kuuza maeneo ya ardhi, maafisa wa ardhi hawakuishia hapo wakaanza kuvigawa viwanja vyote vile vya low density na kuvigeuza higher density na badala ya hapo kuanza kushirikiana na matapeli wakubwa wa ardhi akina Mushi, nina uhakika umeshawahi kulisikia hili jina, katika kuviuza viwanja mara mbili.

Matatizo mengi ya ardhi tunayaona leo, yamesababishwa na wizara yako! Master plan toka Singapore ni jambo jema ila kama watu wa offisini mwako hawakuwa ethical, hata mkipata master plan toka mbinguni haitasaidia kitu. Mama Tibaijuka, tafadhali anza kwa kubadilisha mentality za watu wa offisini mwako; la sivyo, utakuwa unapoteza muda wako na wa hao Wasingapore ...
 
WanaJF

Nilikuwa mmojawapo wa viongozi tulioandamana na Mhe Rais katika ziara yake ya majuzi nchini Singapore. Ninawaletea sehemu ya Master Plan ya mji wao mpya unaojengwa kutokana na kuokoa ardhi baharini (reclamation). Unaona kila kipande cha ardhi mpya kimeshapangiwa matumizi yake na kuwekewa malengo ya majengo yanayotakiwa.

Kupanga ni kuchagua. Kunahitaji nidhamu na hakuna mchezo wala utani. Huwezi kuwa na mji uliopangwa kama unapenda na kuendekeza uholela na vurugu (chaos). Kinachotakiwa ni kushirikisha wadau wote kupanga malengo na viwango baada ya kupata maoni ya wataalam. Wanaoarithirika na kulazimisha kuhama kupisha maendelezo mapya wanalipw fidia stahiki na endelevu.

Anayedai vinginevyo si msema kweli. WaSingapore wamehaidi kutusaidia katika ujenzi wa Mji Mpya wa Kigamboni. Ninakaribisha maoni yenu hasa nyie mlio nje na mnaishi katika miji iliyopangwa? Je uholela unavumiliwa au kuendekezwa? Tupe habari.

View attachment 97055

Mama Tibaijuka
Mama, shikamoo?

Mosi, hongera kwa ramani uliyotoa, kwa maana inatoa hamasa na mvuto wa sisi kutamani kuwa na mji kama huo siku za usoni.

Pili, kuna mambo muhimu umeeleza hapo juu, refer to your post "..Kupanga ni kuchagua. Kunahitaji nidhamu na hakuna mchezo wala utani. Huwezi kuwa na mji uliopangwa kama unapenda na kuendekeza uholela na vurugu (chaos). Kinachotakiwa ni kushirikisha wadau wote kupanga malengo na viwango baada ya kupata maoni ya wataalam. Wanaoarithirika na kulazimisha kuhama kupisha maendelezo mapya wanalipw fidia stahiki na endelevu....".

Maneno niliyonakiri hapo juu ni muhimu sana ktk kizazi na jamii yoyote ile ili kufikia kule ambako akili na matamanio yetu yanalenga.

Tatu, ukitazama ujumbe uliopo kwenye quotation hapo juu, mfano; kupanga ni kuchagua, nidhamu, hakuna mchezo wala utani, unapenda na kuendekeza uholela na vurugu, kushirikisha wadau, kupanga malengo na viwango, kupata maoni ya wataalamu, fidia stahiki na endelevu...., these words are very strong and visionary but hayatimizwi kwa kiasi kikubwa sana.

Nne, tatizo la kushindwa kwa Tanzania na watanzania ni ktk kufahamu na kutenda kutokana na mawazo na mtazamo wa watu kama wewe, Mama Tibaijuka. Haiwezekani binadamu wa kawaida awaze masuala muhimu ya nidhamu, heshima, n.k, halafu utende kinyume na unayosema.

Tano, kuhusu fidia stahiki na endelevu, amin nakuambia kuwa watawala hamtendi haki ya dhati kwa watanzania ambao wanakumbwa na dhahama ya miradi ya maendeleo kama ambayo umetaja hapo juu, Kigamboni Satellite City. Katika hali yoyote ile, lazima uamini na kutambua kuwa wananchi hawatakuwa tayari kupisha miradi ya maendeleo ikiwa watafinywa/ kukandamizwa ktk ulipaji fidia stahiki na/ au endelevu, na mara nyingi watafanya hujuma za wazi au siri kwakuwa wanahisi na kuona uonevu unatamalaki.

Sita, ushirikishaji wataalamu, kuna tatizo kubwa sana ktk nchi yetu la kushirikisha wataalam wa ndani (local expertise). Hebu tuambie, ktk mradi wa Kigamboni, how many local companies are involved ktk stages zote za mradi, na tena, if possible, tell us the open procedures used to acquire those local, and even foreign, expertise ktk kuendeleza mradi wa Kigamboni?


Mwishowe, naomba nikujulishe kuwa kwa kiasi haturidhishwi na namna wewe na watawala wenzako mnavyotufanya wajinga na wehu ktk ardhi yetu. Nnchi yetu ni nzuri, yenye neema na kila aina ya utajiri lakini maisha ni magumu, fursa za biashara na kazi hakuna.

All the best.




 
Tena afadhali leo nimekupata mama kwa mm ni mkazi wa kigambon tena maeneo ya uvumba kigamboni. tarehe 25 april nilitathiminiwa eneo langu. lakn hv majuzi mbunge wangu alikuja na kudai watu wasikubali. me binafsi niliona kama tunazinguana tuu. mheshimiwa tatizo ninaloliona hapa ni utekelezaji wa yale unayoyaongea mara kwa mara ni zero. wananchi asilimia 80 ya watu wa mizimbin wamekubaliana na mradi lakin mnafanya taratibu sana kiasi kwamba tunapotezeana muda. kama mnachukua maeneo yetu tulipeni tuondoke hii ya kuongea sana haisaidii usitegemee watu wote wakubali lazima kutakuwa na wapingaji tuu. me binafs na baadhi ya wengi tumechoka kusubiri. ukumbuke mama hatukopesheki na taasisi za kibank au hata wakikukopesha ni kwa muda mfupi. na unajua madhara ya mikopo ya muda mfupi tunaumia sana tafadhali sana fanyeni hima au kama haiwezekani basi tuacheni tuendelee kuwekeza kwenye maeneo yetu
 
Hivi lile ghorofa pembezoni mwa lililoporomoka mheshimiwa Tibaijuka aliamuru libomolewe kwa niaba ya serikali limebomolewa au bado? ni nini kinasubiriwa? majanga majanga haya!!
 
kama singapore tulikuwa pamoja kiuchumi enzi tunapata uhuru lakini leo hii wamekuwa wafadhili wa kujenga mji mpya, mama pamoja na raisi mliyeambatana nae hamjisikii aibu kushindwa kujiendesha bila kuomba
 
Yaleyale ya kuwatimua Masikini mjini ! Mji Mmoja Ramani Kibao ! Najuta hata kufungua Uzi huu .
 
huyu mama mbona hataki kujibu chochote au ameona haya mawazo co ya watu wanaoishi kwenye nchi au miji iliyopangwa
 
Ni kweli Madam kupanga ni kuchagua, na bila kushirikisha wadau huwezi kufikia malengo yako kwa wakati.
Labda nikuulize kuwa, baada ya kuona Master Plan ya wenzetu Singapore uliweza kumshauri Mheshimiwa kuhusu master plan za miji yetu?
Je, umemshauri mkulu kuwa rasilimali za tanzania zinaweza ku plan miji yetu bila misaada kutoka kwa wawekezaji?
Tunapata mashaka sana kama mji wa kigamboni haujauzwa kwa bush, kama Loliondo ilivyo nchi nyingine ndani ya tanzania.
 
Hii nchi haina vipaumbele au yaani mapori yote haya leo mnazungumzia kufukia bahari ili mpate pakujenga is it a joke or what! Kwani lazima mji mpya uwe kigamboni why not tanga,mtwara,kibaha etc naona kama tunataka kubananisha kila kitu dar huo mji wa kisasa ungejengwa let's say tanga ikipunguza msongamano hapa dar nadhan tunahitaji some breathing space!
 
Back
Top Bottom