Masikini kaka huyu

Masikini kaka huyu

Haimaanishi kuwa atakua amemkataa au kumkimbia mtoto atapo sepa. Lkn atakua amejiepushia balaa hilo la mke wake kutaka kulala nae kilazima. Inaelekea analengo lake tu jamaa apate ili waishi wote kama waathirika mana anahisi jamaa atasepa tu no way out.

Hata Mimi nahisi hivi
 
Duuhh kazi kweli kweli, wakati mwingine mimi Huwa naamini hakuna ulevi mbaya kama DINI (mnisamehe kwa hili). Maana humwondolea mtu uwezo wa kufikiri kwa mantiki. Kwa hali ilivyo bora waachane (japo wengine huamini alichokiunganisha Mungu.....)

Umeongea kweli tupu
 
Si ndo maana mimi nimegoma kutafuta mchumba ndan ya makanisa ya kilokole,maana wanawake wengi walioko kule ni wale waliostaafu ukahaba,waliostaafu kuua kwa kutoa mimba...awashirikishe washenga na wazee

Aiseee
 
Mwambie arudi huko alipofunga ndoa ambako hata hawaku-bother kuwauliza vyeti vya clearance ya HIV status...

Hao ndio wampe ushauri wa nini cha kufanya...
 
wakati napokea hizi taarifa nilipata shida mnoo kwwa jinsi kijana alivyokuwa anamwamini mkewe

ndio maana kuna semi nyingi zinazopinga uaminifu wa wanawake, sidhani kama binti alikuwa hafaham afya yake au alikuwa ana mahusiano na kidumu chake angali bado yupo na mme mtarajiwa.
 
Huyo mwanamke ana hila

Atalazimishaje ngono bila kondom???

Ila mwanaume nae kiazi.... msimamo wake wa kiume uko wapi???
 
nimeamini hakuna kiumbe kipole duniani nikikumbuka binti alivyokuwa kapole na mstaarabu lakini leo kawa kama mbogo
Mkuu miss chagga hebu nifafanulie kwanza haya maswali yangu. Tatizo hili zito la wanandoa wamekuambia wakiwa wote wawili au unapata maelezo ya upande mmoja,yaani kwa huyo kaka rafiki?? Je! Majibu ya kaka yako umeyathibitisha au anakueleza mwenyewe!? Ukinijibu ntarudi kutoa ushauri.
 
Last edited by a moderator:
Tatizo ninaloliona hapa ni unyanyapaa...Mume kamnytanyapaa mkewe...Na hilo ndilo litamuathiri zaidi

Baba ampende mke wake...alale nae kitandani...atumie Condom kwa uangalifu mkubwa.....kama anampenda atamtimizia....kabla ya kumuingilia ahakikishe amekuwa tayari haswa....

Wapo watu wengi wanaishi na wenza wenye Maambukizi ...Lakini hawawatupi wenza wao....

Dada anatakiwa kufanyiwa Counselling ya kufa mtu....amechanganyikiwa sana...anatakiwa ajikubali


Watz bana. Kila kitu kinatafsiriwa kama unyanyapaa..nikisema walioathirika watoe shuhuda zao mtasema nanyanyapaa...
 
Aendelee kusubiri muujiza wa yeye kuambukizwa vvu!! Maana kuna mambo mengine inabidi kujiongeza na siyo kusubiri ushauri!!
 
Habari zenu wana Jf,

Ni moja ya rafiki zangu ni kijana mkimya, mpole, mcha Mungu, ana heshima na mpiganaji katika kutafuta maendeleo, katika pilika pilika zake Mungu akampa binti mzuri, mpole, msikivu na mwenye adabu hapa ndipo mwanzo wa misha yao mpaka ndoa. Kwa sasa wana mwaka mmoja ndani ya ndoa yao na Mungu kawamjalia mwanamke kwa sasa anaujauzito wa miezi miwili katika ile hali ya kuugua ugua akaenda hospital.

Kinachosikitisha na kuhuzunisha ni kijana mwezi huu kagundua mkewe ni muathirika (VVU). Huyu rafiki yangu huwa na mwita kaka ili kukata mzizi wa fitina si unajua mabinti tulivyo. Baada ya kugundua hivyo nikaanza kumuuliza je hawakupima wakati wa maandalizi ya ndoa.? Majibu aliyotoa kiukweli ni huzuni eti hawakuona haja ya kupima kisa wote aliona wametulia na hakukuwa na hisia yeyeote ya uchepukaji na pia walikutana Kanisani.

Nilivyo fyoko fyoko nikauliza vipi mlianza kuzini kabla ya ndoa na mlikuwa mnatumia Condom? akaijbu ndiyo ili kuzuia mimba kwa hiyo walivyofunga ndoa tu wakaanza kunjunjana bila Condom bila hata kujua afya ya kila mmoja.


Mungu si nanjilinji bwana wee kijana hajaathirika kapima zaidi ya mara 7 kila akipima anaona negative kawa kama chizi akipita mjini akiona hospital anashuka anapima aamini majibu anayopata.Lakini kutokana na vipimo inaonekana ajaathirika, kaenda hospital na mkewe doctor wamempa namna ya kuishi na mtu wa VVU lakini ameshindwa kinachotokea kijana analala sebuleni mwanamke chumbani.

Kinachotokea mke kawa na gubu anamlazimisha mwanaume mapenzi (ngono) mwanume hawezi, jamani mimi nimeshindwa mshauri zaidi nilimwambia alale sebuleni au Mzungu wa nne mwanamke amegeuka moto anataka ngono bila hata condom. Jamani naombeni anayeweza toa njia nyingine ya kumsaidia kijana ili waishi at least kwa amani mwenye suluhu

Karibuni, ushauri

Waachane kisheria usichezeee ngoma wajameni
 
Duuh! Huyu jamaa sidhani hata kama akiamua kufanya ule mchezo wa baba na mama dude yake itasimama. Hapo ni kama keshapigwa ganzi kisaikolojia.
 
Ukweli hali kama hii inauma sana. Waende kwa kiongizi wao wa kiroho kupata ushauri, pia wazazi wa pande zote mbili nao wahisishwe ili washiriki ktk kuamua.

Miss Chagga, mpe pole nyingi jamaa pia mke wake.
 
Inaonekana alikua hasugui sana. Aendelee aste aste tu.
ila mbona ni sababu tosha kuachana maana ni ushahidi wife alipira diversion.
 
walishauriwa na moja ya njia ni kutumia kinga binti hataki hilo swala la kinga anasema ni dhambi

He! ati kutumia kinga ni dhambi?? mbona walikuwa wanatumia kabla hawajaoana?? Ilikuwa si dhambi walipokuwa wanazuia nazo mimba ila sasa kuzuia VVU ishakuwa dhambi? Haki ya nani kuna mitihani mingine unaweza kufikiri uko ndotoni! Huyo mke hata kumshambulia naogopa maana sipati picha ndo ingekuwa mimi. Huku una VVU, huku una mshtuko, una huzuni, mtu unayemtegemea akufariji anakukimbia... kwa ufupi bidada yuko kwenye "denial" ndo maana hata anadai mngonoko kama kawa tena bila kinga. Na mantiki yake ni kuwa kama wameshangonoka mwaka mzima bila condom leo maambukizi yatatoka wapi? Kijana nae ana mshtuko. Mi ningemshauri asilale sebuleni. Alale kitanda kimoja na mkewe, tena amkumbatie kabisa maana tatizo la mke ni kubwa kuliko la mume. Huyu dada pamoja na VVU pia ni mjamzito. Hatakiwi kuachwa kulia lia hovyo na kukosa matumaini. Kama wanamjua Mungu basi wanajua hakuna jaribu lisilo na mlango wa kutokea. Kaka aache kuhukumu maana hakuna ajuaye mke amepataje VVU. Kokote alikopata, sasa wapo wote ndani, ni mkewe, ndo mama mtoto hivyo. Watulie sana, mi naamini watapata suluhisho pengine hata la kuendelea kuishi pamoja na kungonoka na kuendelea kuzaa. Wakipata suluhisho la kutengana basi nalo liwe la heri limuache kila mmoja akiwa na mzigo mwepesi. Mwambie akae kimya kwa sasa, watafakari wenyewe maana hawawezi kuendelea kuchachawa kama maharage yanayochemka. Ifike mahali watulie waongee na habari ya "Uliutoa wapi" isiwepo labda mwanamke mwenyewe aamue kufunguka kama anajua. Namaanisha maongezi yasiwe ya lawama bali ya kutafuta suluhisho. Huyo Mungu wao wakimrudia na kutubu ni mwaminifu, atawapa nguvu ya kuvumilia na atawapa hekima ya kulimaliza hili jambo. Amen.
 
Habari zenu wana Jf,

Ni moja ya rafiki zangu ni kijana mkimya, mpole, mcha Mungu, ana heshima na mpiganaji katika kutafuta maendeleo, katika pilika pilika zake Mungu akampa binti mzuri, mpole, msikivu na mwenye adabu hapa ndipo mwanzo wa misha yao mpaka ndoa. Kwa sasa wana mwaka mmoja ndani ya ndoa yao na Mungu kawamjalia mwanamke kwa sasa anaujauzito wa miezi miwili katika ile hali ya kuugua ugua akaenda hospital.

Kinachosikitisha na kuhuzunisha ni kijana mwezi huu kagundua mkewe ni muathirika (VVU). Huyu rafiki yangu huwa na mwita kaka ili kukata mzizi wa fitina si unajua mabinti tulivyo. Baada ya kugundua hivyo nikaanza kumuuliza je hawakupima wakati wa maandalizi ya ndoa.? Majibu aliyotoa kiukweli ni huzuni eti hawakuona haja ya kupima kisa wote aliona wametulia na hakukuwa na hisia yeyeote ya uchepukaji na pia walikutana Kanisani.

Nilivyo fyoko fyoko nikauliza vipi mlianza kuzini kabla ya ndoa na mlikuwa mnatumia Condom? akaijbu ndiyo ili kuzuia mimba kwa hiyo walivyofunga ndoa tu wakaanza kunjunjana bila Condom bila hata kujua afya ya kila mmoja.


Mungu si nanjilinji bwana wee kijana hajaathirika kapima zaidi ya mara 7 kila akipima anaona negative kawa kama chizi akipita mjini akiona hospital anashuka anapima aamini majibu anayopata.Lakini kutokana na vipimo inaonekana ajaathirika, kaenda hospital na mkewe doctor wamempa namna ya kuishi na mtu wa VVU lakini ameshindwa kinachotokea kijana analala sebuleni mwanamke chumbani.

Kinachotokea mke kawa na gubu anamlazimisha mwanaume mapenzi (ngono) mwanume hawezi, jamani mimi nimeshindwa mshauri zaidi nilimwambia alale sebuleni au Mzungu wa nne mwanamke amegeuka moto anataka ngono bila hata condom. Jamani naombeni anayeweza toa njia nyingine ya kumsaidia kijana ili waishi at least kwa amani mwenye suluhu

Karibuni, ushauri

Kuna mtu ananiuliza hapa kwamba huwezi kuongeza herufi moja kwenye hiyo kaka isomeke kakaa ili umsaidie kijana mwenzio? Samahani lakini!
 
Back
Top Bottom