Mkuu maringo
Wasiwasi wako unaujenga katika vitu vya kutunga/wa.
Mosi, hakuna barua yoyote kamilifu, hususan ya siri, kutoka kwa mtu yeyote kwenda kwa Katibu Mkuu, imewahi kuvuja mahali popote, si hapa tu Jamii Forum. Hakuna kitu kama hicho. Ni taasisi/ofisi makini inayofanya kazi zake chini ya usimamizi wa mtendaji makini vile vile.
Pili, suala la Prof. Baregu, labda wewe Maringo ndiyo haujui taratibu za utendaji kazi wa tume za namna hii na makamishna wake. Ungelikuwa unajua, ungekuja hapa na kumumwagia sifa za umakini Dkt. Slaa kwa namna alivyokuwa makini ku-communicate suala hilo, hasa kwa kujua implications na complications za kumwandikia barua mjumbe wa tume ya namna hiyo.
Tatu, suala la Mama Shida Salum, sijajua kama maelezo yako unakata rufaa ama vipi, kwa sababu Katibu Mkuu Dkt. Slaa alishalitolea ufafanuzi hapa hapa hasa katika maeneo ambayo chama ama viongozi walikuwa wameguswa katika ripoti ya gazeti lililoandika habari hiyo.
Katibu Mkuu wa CHADEMA anaendelea kuwa mtendaji mkuu makini akisimamia utendaji makini wa kila siku wa chama makini. Ni mtu ambaye huwezi kumfananisha na mtendaji wa chama kingine chochote wa nafasi yake au hata wenyeviti wa vyama vingine mbali ya CHADEMA.
Mtu yeyote makini hapa au nje ya jukwaa hili akiamua kuorodhesha criteria za umakini wa Katibu Mkuu wa CHADEMA anaweza kuandika mambo mengi sana, lakini itoshe kusema kwa hapa, ni mmoja wa watu waadilifu, watakaokumbukwa na historia ya vizazi vya nchi hii kama mtu aliyeshiriki kuzifanya siasa za nchi hii kuwa zilivyo hivi leo, kwamba CHADEMA inasimama kama tishio kubwa la uwepo wa CCM madarakani kuliko wakati mwingine wowote katika historia ya upinzani katika nchi hii.
Ni mmoja wa viongozi shupavu walioanzisha vita dhidi ya ufisadi na ubadhirifu, ikiwa ni moja ya hatua kubwa zilizowahi kupigwa katika safari ndefu ya harakati hizi za mapambano ya awamu ya pili, kusaka uhuru wa kweli, mabadiliko ya kiutawala na kimfumo, kwa ajili ya matumaini na haki za Watanzania, kupitia jukwaa la CHADEMA.
Huwezi kumfananisha na wale wengine wanaoandamwa kila kona ya nchi hii sasa kwa tuhuma kubwa za uhujumu wa rasilimali za nchi hii kiasi cha kukaribia kuzimaliza na kuzifanya kuwa historia tu. Wala huwezi kuwafananisha na wale wengine waliopewa madaraka, wakasahau bigger picture ya struggle waliyopaswa kuisimamia kwa ajili ya maslahi ya wananchi na nchi hii.
Viongozi na Watendaji wanaotembea na tuhuma za kutisha mbele ya vipaji vya nyuso zao na migongoni mwao, si tu kwamba uadilifu wao unatiliwa shaka kubwa na kila raia mpenda nchi hii, bali hawapaswi na hawana uhalali wa kukalia ofisi wanazoziongoza sasa, kwani kuendelea kuruhusu hali ya namna hiyo ni kuziunganisha ofisi zao na ufisadi huo wanaoufanya, waliowateua/ kuwachagua na wote wanaowaongoza.
Hatua kwa hatua, yeye pamoja na makamanda wengine, wakiwepo waliotawanyika nchi nzima, kila kona ya nchi hii, ikiwemo haoa jukwaani na kwingineko, ameendelea kusimamia ofisi ambayo imetokea kuwa mwiba mkubwa kwa walioko madarakani, kiasi kwamba hakuna siku watawala wanaweza kuamuka asubuhi na kwenda kulala usiku, kupata kifungua kinywa, kwenda lunch au dinner, kwenda safari au mapumzikoni, mchana au usiku, inanyesha au linawaka, wakicheka au wakilia, bila kupasua vichwa vyao kufikiria namna gani wataweza kuokoka katika wimbi kubwa la mabadiliko linalopiga kila kona ya 'bahari' hii ya Tanzania kuiondoa CCM madarakani kwa sababu imeshindwa...sera zake zimeshindwa, haiwezi tena.