Mapungufu ya Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr. Wilbrod Slaa

Mapungufu ya Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr. Wilbrod Slaa

Status
Not open for further replies.
Tatizo lenu mnafikiri watu tunadhani DR ni malaika,tatizo ni ninyi mnapo shindwa kuthibitisha hizo tuhuma zenu kwa hiyo mkipingwa mnasema tuna tetea sana.

kwa mfano kwenye hiyo barua hakuna anayejua kuwa ilivuja kabla au baada ya kufika kwenye ofisi ya katibu wewe uliiona hapa jf na ilikuwa imechapwa tuu.

alaf umesha fanya Conclusion na source zako na unategemea tuamini hizo source si wahusika na tukipinga hizo source zako na yaliyo andikwa utasema Dr slaa huwa asemwi kumbe nyie wenyewe ndio mnashindwa pa kumsemea mnajikuta mnaongea bila ushahidi usio tia shaka alaf mnata tusipinge.
 
Haya mtoto wa lumumba project kazi yako imeonekana, wahi lumumba kachukue buku saba yako faster!!!
 
UTENDAJI WA KATIBU MKUU DR WILBROD SLAA


Nimepata wasiwasi na utendaji wa katibu mkuu dr slaa kwa namna anavyoshughulikia mambo.

1. Kushindwa kumfahamisha kwa barua prof: baregu kuhusu maelezo ya kikao cha kamati kuu kuhusu kujitoa katika mchakato wa katiba mpya. Ukiwa mtendaji mkuu hupaswi kuagiza kwa mdomo unapaswa kutoa barua na kuijbiwa kwa barua utaratibu aliotumia kumfahamisha prof baregu unaonyesha mapungufu ya kutambua kazi za ukatibu mkuu. Source; gazeti la raia mwema

2.Katibu mkuu namna alivyoshughulika suala la kutaka kutekwa mama yake Zitto limeleta utata.

Namna katibu mkuu alivyolishughulikia na kushindwa kutoa press release kama chama kwani ye ye ndio mtendaji mkuu kwani watu wamezusha kwamba kuna mpango wa hujuma kama katibu mkuu naona kuna mapungufu.source: gazeti la mtanzania

3.Kuvuja kwa barua ya siri ya mh, Zitto Kabwe ambayo ilikuwa ni confidential haya ni mapungufu katika utendaji wa katibu mkuu dr. Slaa. Source: jamiii forum
.

Ukifatilia CHADEMA chini ya katibu mkuu kuna mapungufu yanajitokeza katika utendaji kazi nafikiri angepima mwenyewe kabla ya kuamua kujiuzulu.
Hayo Mkuu mbona ni madogo, vipi katibu mkuu wa CCM kumiliki meli zilizosafirisha meno ya tembo hadi Vietnam na kampuni za uwindaji za OTELO, ukiunganisha dots na utetezi wa nguvu wa Mhe Nchimbi Waziri wa mambo ya ndani hapo vipi?????

 
Mwache wewe bakia na Katibu Mkuu wa CCM you will be much happy kaka wacha kujisumbua na Chadema nawe ukiwa ni CCM

ushauri mzuri.
Amfuate ant.tembo.
Aachane na anayesababisha magamba yasilale.
 
UTENDAJI WA KATIBU MKUU DR WILBROD SLAA


Nimepata wasiwasi na utendaji wa katibu mkuu dr slaa kwa namna anavyoshughulikia mambo.

1. Kushindwa kumfahamisha kwa barua prof: baregu kuhusu maelezo ya kikao cha kamati kuu kuhusu kujitoa katika mchakato wa katiba mpya. Ukiwa mtendaji mkuu hupaswi kuagiza kwa mdomo unapaswa kutoa barua na kuijbiwa kwa barua utaratibu aliotumia kumfahamisha prof baregu unaonyesha mapungufu ya kutambua kazi za ukatibu mkuu. Source; gazeti la raia mwema

2.Katibu mkuu namna alivyoshughulika suala la kutaka kutekwa mama yake Zitto limeleta utata.

Namna katibu mkuu alivyolishughulikia na kushindwa kutoa press release kama chama kwani ye ye ndio mtendaji mkuu kwani watu wamezusha kwamba kuna mpango wa hujuma kama katibu mkuu naona kuna mapungufu.source: gazeti la mtanzania

3.Kuvuja kwa barua ya siri ya mh, Zitto Kabwe ambayo ilikuwa ni confidential haya ni mapungufu katika utendaji wa katibu mkuu dr. Slaa. Source: jamiii forum
.

Ukifatilia CHADEMA chini ya katibu mkuu kuna mapungufu yanajitokeza katika utendaji kazi nafikiri angepima mwenyewe kabla ya kuamua kujiuzulu.​

:msela::msela::msela::msela:

:msela::msela::msela:Ngoja wenyewe waje, wa "manage stress" zetu.:msela::msela::msela:
:msela::msela::msela::msela:​
 
Upungufu mwingine ni kwamba anajiita Dokta huku akijua ukweli kuwa hana hadhi hiyo. Ni dokta Kanjanja.

unamsema aliyepata udokta baada ya utafiti wake wa maisha bora kwa kila mtanzania na akapata majibu kuwa ishara yake ni kuwa na msongamano wa magari dar?
 
Haya, tumeyasikia ya Katibu Mkuu wa CHADEMA, sasa tujadili mapungufu ya Katibu Mkuu wa CCM Mh. sana Kinana.
Tukimaliza tutajadili na mapungufu ya wenyeviti Ili tupime upande upi dhaifu!
Mbona mnaupigia mbiu upungufu wa kumwarifu Prof. Baregu kwa barua wakati mnajua hilo si kosa la jinai, lakini mnafumbia macho kasoro za Katibu Mkuu wenu?
Kwanza kabisa Bwana huyo si raia wa nchi hii, ni Msomali na tunavyo vielelezo!
Pili anahusika na jinai za ujangili na yumo kwenye rada za mashirika yanayojishughulisha na ulinzi wa mazingira na wanyama wanaotishia kutoweka kipindi kifupi kijacho?
Unaelewa pia kwamba kutokana na ujangili unaosimamiwa na vigogo wa CCM tembo wanaweza kutoweka ndani ya miaka 20 tokea sasa kama ilivyotokea kwa faru?
Mengine malizieni wenyewe!
 
kila mtu ana mapungufu na hakuna mwanadamu aliyekamilika hata siku moja na haitaweza kutokea so Dr slaa pamoja na mapungufu hayo lakini yeye bado ni jembe kwenye uongozi waka
 
Dr. Slaa ni malaika aliyeshuka toka juu mbinguni hivyo hapaswi kukosea. Kama yeye ni kiongozi malaika basi kakosea.
 
Uimara wa Chadema unasababishwa na uwepo wa Dr Slaa. Maranyingi mti wenye matunda ndio unaotupiwa mawe
 
Thread zinazomuhusu Dr.SLAA ZINAUZA SANA HAPA JF.
NAOMBA WAHUSIKA MUMTUNUKU HUYU MHESHIMIWA TAFADHALI.
 
ambaye hajawahi kuzini na mke wa mtu ajitokeze hapa. Wote wadhambi tu. Afadhali doc. Kuliko wezi wafuatao:
Meremeta,
vitalu vya kuwinda tembo nk
epa groups
mabilioni ya cis
ununuzi nguzo za umeme
na mengine kibao
changia hoja acha maneno ya kitoto mke wa mtu sumu
 
Sijawahi kusikia umemwajiri Katibu Mkuu wa Chadema. Kumwajiri kungekupa uhalali wa kuhoji utendaji wake. Jiuzuru wewe kukurupuka na umbeya
 
yule ni dikteta halafu ana dharau, anataka akisema yeye hata kama amekosea watu wafuate kwa kutii tu
Hivyo ndivyo watanzania wanavyopenda kuongozwa. Kama Nyerere asingekuwa dikteta leo hii msingekuwa mnakaa chini na kumsifia kama rais shujaa. Watanzania usipokuwa mbabe hawafanyi kazi. Wamezoea kusukumwa. Angalia utawala wa Mkapa ulivyokuwa wa kibabe na namna ambavyo mambo yalikwenda. Ndiyo maana tunaamini kwamba Dr Slaa anaweza kuwa ndiye Rais bora kabisa kwa Tanzania ya sasa, maana hana muda wa kucheka na wezi na wahujumu uchumi. Nafikiri kile alichokufanyia kimekupa somo zuri sana kwamba si mtu wa kucheka na wajinga kama anavyofanya Kikwete. Tunashukuru kwa kushuhudia hili.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom