Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
- Thread starter
- #41
Nyereist yeyote hawezi kupinga Muungano, kwa hili suala Unyerere ulishamshinda Mwanakijiji zamani, wakati tunapigania haki na maslahi ya Watanzania Bara miaka yote hapa JF Mwanakijiji alitupinga vikali, aliweka mbele symbolism na utukufu wa "Baba wa Taifa."
Sasa anakula matapishi yake, ameona kweli tunaopinga Muungano tuna uchungu na nchi na tuna hoja za msingi, badala ya kushinda tunaimba nyimbo za kuabudu Nyerere this, Nyerere that. I mean, hata Wamarekani wanawatukuza founding fathers wao lakini kuna mambo ya karne zile wameyakataa leo hii, you know? Founding fathers wa Marekani walikua wana own slaves, kwa hilo wamekataa kuwatukuza.
Nyerere alichemka kwa kutuunganisha na ka nchi kadogo ambako kalikataa toka mwanzo kumezwa, kwa hiyo akakafanya eti kana hadhi sawa na Tanzania Bara. Matokeo yake ndio haya, Zanzibar kila uchwao wanadai more and more autonomy halafu CCM wanatudanganya eti tunaelekea "serikali moja." Serikali moja my foot, sasa hatutaki hata serikali saba, tunataka kuvunja Muungano, period!
Unazungumza kama una uhakika sana wa unachozungumza... wanaonisoma vizuri wanaelewa ninasema nini. Kama hujanipata naweza kukusaidia kuelewa kile ambacho ninakisema.