Kaimu Waziri wa Afya-Saada: Hatuwezi Kuwatibu wasio Wazanzibari

Kaimu Waziri wa Afya-Saada: Hatuwezi Kuwatibu wasio Wazanzibari

Inside10

Platinum Member
Joined
May 20, 2011
Posts
34,719
Reaction score
42,739
Kaimu Waziri wa Afya Zanzibar, Saada Mkuya Salum amesema Serikali ya Mapinduzi Zanzibar haiwezi kugharamia matibabu kwa Watu wasio Wazanzibar.

Saada ametoa kauli hiyo Juni 8, 2026 wakati akijibu hoja kwenye Baraza la Wawakilishi Zanzibar kupitia vikao vinavyoendelea vya kujadili bajeti mbalimbali.

SnapInsta.to_491441251_18045630191591832_4290940529571971534_n.jpg

“Mtu ambaye sio Mzanzibar anakwenda katika hospitali zetu anaonesha matibabu kadi, pili Watu kuzuiwa nadhani nilitoa maelezo sana, sio ZHF inaanza bali inaendelea kuwasajili wengine ambao sio wa sekta ya umma”

“Wakati Wanachama wa ZHF wakiendelea kusajiliwa kulikuwa na Matibabu Kadi zikitolewa unakwenda kwa Sheha unachukuliwa taarifa zako unakwenda hospitali hakuna anayekurudisha ilo moja, la pili kilichokuwa kikibainika kwa wenzetu wa hususan kwa ngazi ya Masheha si waaminifu, Mtu si Mzanzibar anakwenda kwenye hospitali zetu anaonesha matibabu kadi na wale waliokuwa wanakaa pale wanamwambia atoe kitambulisho cha Mtanzania”

Soma Pia: Zanzibar: Naibu Waziri wa Vijana, Hassan Khamis: Wanaofanya kazi kwenye Mahotel Zanzibar siyo wazawa inabidi tufanye Mapinduzi

“Bajeti yetu ya trilioni 8 tutaweza kuwatibu Watu milioni 60 ? Tumeona wengine sio Wazanzibar wanatibiwa kwa kutumia matibabu kadi,”amesema Kaimu Waziri wa Afya.

N.B: Huyu mama tukumbuke alikuwa waziri wa fedha katika serikali ya Muungano

 
Kaimu Waziri wa Afya Zanzibar, Saada Mkuya Salum amesema Serikali ya Mapinduzi Zanzibar haiwezi kugharamia matibabu kwa Watu wasio Wazanzibar.

Saada ametoa kauli hiyo leo Juni 9, 2026 wakati akijibu hoja kwenye Baraza la Wawakilishi Zanzibar kupitia vikao vinavyoendelea vya kujadili bajeti mbalimbali.

“Mtu ambaye sio Mzanzibar anakwenda katika hospitali zetu anaonesha matibabu kadi, pili Watu kuzuiwa nadhani nilitoa maelezo sana, sio ZHF inaanza bali inaendelea kuwasajili wengine ambao sio wa sekta ya umma”

“Wakati Wanachama wa ZHF wakiendelea kusajiliwa kulikuwa na Matibabu Kadi zikitolewa unakwenda kwa Sheha unachukuliwa taarifa zako unakwenda hospitali hakuna anayekurudisha ilo moja, la pili kilichokuwa kikibainika kwa wenzetu wa hususan kwa ngazi ya Masheha si waaminifu, Mtu si Mzanzibar anakwenda kwenye hospitali zetu anaonesha matibabu kadi na wale waliokuwa wanakaa pale wanamwambia atoe kitambulisho cha Mtanzania”

“Bajeti yetu ya trilioni 8 tutaweza kuwatibu Watu milioni 60 ? Tumeona wengine sio Wazanzibar wanatibiwa kwa kutumia matibabu kadi,”amesema Kaimu Waziri wa Afya.
Chanzo millard ayo

N.B: Huyu mama tukumbuke alikuwa waziri wa fedha katika serikali ya Muungano


Yes yuko sahihi
Kila mtu si ana kwake au kwao?

Naunga mkono hoja yake
 
Yupo kwenye Baraza la Wawakilishi akitetea uzanzibari na Zanzibar ambayo ipo kisheria. Kosa lake lipo wapi ?..

Kama waasisi waliona Tanganyika ife ili watanganyika wawe watanzania ila wazanzibari wabaki na uzanzibari wao na utanzania kama nyongeza.

Unawalaumuje, wapo sahihi kabisa
 
Kaimu Waziri wa Afya Zanzibar, Saada Mkuya Salum amesema Serikali ya Mapinduzi Zanzibar haiwezi kugharamia matibabu kwa Watu wasio Wazanzibar.

Saada ametoa kauli hiyo Juni 8, 2026 wakati akijibu hoja kwenye Baraza la Wawakilishi Zanzibar kupitia vikao vinavyoendelea vya kujadili bajeti mbalimbali.

“Mtu ambaye sio Mzanzibar anakwenda katika hospitali zetu anaonesha matibabu kadi, pili Watu kuzuiwa nadhani nilitoa maelezo sana, sio ZHF inaanza bali inaendelea kuwasajili wengine ambao sio wa sekta ya umma”

“Wakati Wanachama wa ZHF wakiendelea kusajiliwa kulikuwa na Matibabu Kadi zikitolewa unakwenda kwa Sheha unachukuliwa taarifa zako unakwenda hospitali hakuna anayekurudisha ilo moja, la pili kilichokuwa kikibainika kwa wenzetu wa hususan kwa ngazi ya Masheha si waaminifu, Mtu si Mzanzibar anakwenda kwenye hospitali zetu anaonesha matibabu kadi na wale waliokuwa wanakaa pale wanamwambia atoe kitambulisho cha Mtanzania”

“Bajeti yetu ya trilioni 8 tutaweza kuwatibu Watu milioni 60 ? Tumeona wengine sio Wazanzibar wanatibiwa kwa kutumia matibabu kadi,”amesema Kaimu Waziri wa Afya.

Hata hivyo, Serikali ya Zanzibar inaendeleza sera ya matibabu bure ambapo kila Mzanzibar halipishwi fedha yeyote kwenye matibabu mbali mbali ikiwemo dialysis, upasuaji, kulazwa, huduma za dharura, upasuaji au homa.
 
Nchi ikiwa na kiongozi asiyejitambua lazima ipoteze mwelekeo.

Haya mambo ya kijinga mara nyingi hutupata tukiwa na viongozi dhaifu, waliokosa dira, wasiojua wapi wanatupeleka kama taifa.

Ajabu ujinga wa kiwango hiki unazungumzwa, wala mjinga mwenzake hatamtumbua, wajinga wakidhani wanatukomoa, wasijue wanajivua nguo zao wenyewe.
 
Yupo kwenye Baraza la Wawakilishi akitetea uzanzibari na Zanzibar ambayo ipo kisheria. Kosa lake lipo wapi ?..

Kama waasisi waliona Tanganyika ife ili watanganyika wawe watanzania ila wazanzibari wabaki na uzanzibari wao na utanzania kama nyongeza.

Unawalaumuje, wapo sahihi kabisa
Ni uhalisia ila kuna mambo hayatakiwi kusemwa kwa sauti kubwa sana, ni kunong'onezana tu. Ni kama vile CCM wajitokoze waseme huwa wanagawa awamu za urais galatia-kobaz-galatia-kobaz...
 
Back
Top Bottom