Mapinduzi ya Zanzibar: Mchango wa John Okello (Che Guevara wa Afrika Mashariki) umefutwaje?

Phillemon Mikael

Platinum Member
Nov 5, 2006
10,535
8,620
Mwaka 1964 siku thelathini baada ya uhuru wa bandia wa Zanzibar, wanamapinduzi kumi na nne wakiongozwa na mpigania uhuru John Okello aliwaongoza kwenye mapinduzi ya Zanzibar yaliyokuwa na umwagaji mkubwa wa damu.

Baada ya mapinduzi kufanikiwa John Okello [kiongozi wa mapinduzi] alichukua jukumu la kutangaza mapinduzi kwenye radio Zanzibar, ikumbukwe pia wakati mapambano yakiendelea ..aliyekuja kuwa rais wa Zanzibar mzee Karume na Babu walikuwa mafichoni na hawakushika wala bisibisi kwenye mapinduzi na hata ukiangalia ile picha ya wanamapinduzi ya kwanza John Okello amevalia kipolisi na amekaa kama kiongozi rasmi.

Baada ya hali kutulia Okello anamtangaza Karume rais na Abdulrahman Babu kuwa Waziri mkuu. Na ndie aliyeenda kumpokea Karume kutoka alikokuwa amejificha kwa siku kadhaa.

Baada ya siku chache mzee Karume akamfukuza Zanzibar kama mbwa John Okello [Field Marshal] na bila kujali mchango wake anatokomea kusikojulikana na historiaa ya mapinduzi ikafutwa na nafasi ya Okello ikaja kuwa mkwezi, mpiga tofali ambaye alibahatika kupiga picha [akiwa amekaa kitini katikati tu kwa sababu ya kuwa na kipaji cha kuongea - (kumbuka kuwa hata kiswahili chake kilikuwa 0kibovu)]

Naomba kuchokoza mada kuhusu nafasi ya John Okello kwenye mapinduzi, kwa nini historia ilifunikwa?

Je aliishia wapi,..wapenda historia ya kweli wameshatamani hata kujua lilipo kaburi lake..kumbukeni wenzetu Kenya baada ya kugundua hila wanahaha kutafuta kaburi la Field Marshal Dedan Kimathi...mbona wapenda hitoria Zanzibar na Tanganyika kwa jumla hamumtendei haki JOHN OKELLO [FIELDMASHAL]?



==============


Video ikimwonesha Okello,Karume na Babu masaa machache baada ya Mapinduzi

 
Last edited by a moderator:
Philemon umesema ukweli,

Historia ya Tanzania imekuwa na tabia ya kufuta michango ya wale ambao hawakupendwa na wakubwa: John Okello akiwa mmoja wao.

Ingawa sijasoma maandiko yaliyopo kuhusu historia ya Tanzania kwa muda mrefu ukweli wa kuwa majina kama ya Okello, Kambona, na Kanali Mahafudhi yamefutika kabisa katika historia ya Tanzania. Bibi Titi Mohammed alipata bahati baada ya kurudi CCM na hivyo kurudisha jina lake katika historia lakini nalo lilikuwa limeshapotea.

Tutafute utaratibu wa kutunza historia kamilifu ya nchi bila kujali uhusiano wa wahusika na "ukoo wa mfalme" ulikuwaje.
 
Wakati huo huo tusisahau kuwa wengine ambao tunalazimishwa kuwasahau ni
Abdulwahid na Ally Sykes, Hamza Mwapachu, Tewa Said Tewa, Ali Migeyo , Suedi Kagasheki, Dossa Azizi, Abdulkarim Karimjee,Chifu Abdieli Shangali wa Machame, Kleist Sykes, Ally Sykes na Abdulwahid Sykes.

Kwa uchache sasa huyo Okello alikwa ni just one in a million na at least eyey leo anazungumzwa.
 
Maprofessa mahiri wetu mko wapi kwa historia ya kweli,upo wapi haroub othman,proffesa mazrui, baregu na wengine tele wasomi..wanazuoni.

Historia ya mataifa yetu hapa afrika mashariki imepindishwa, andikeni upya.
kwa nini tunawafundisha watoto uwongo?
 
phillemon mikael said:
Mwka 1964 siku thelathini baada ya uhuru wa bandia wa zanzibar ...john okello [kiongozi wa mapinduzi] alichukua jukumu la kutangaza mapinduzi kwenye radio zanzibar,...baada ya siku chache mzee karume anamfukuza zanzibar kama mbwa ...


YAITWAYO "MAPINDUZI"

John Okello alitoka kwao Uganda, Injin aliyetoka kwao Kenya na Mfaranyaki aliyetoka Tanganyika, na kuivamia nchi huru usiku wa manane wa kuamkia tarehe12 Januari 1964. Wananchi, mafisadi kwa sababu ya maslahi ya nafsi zao hawakuhisi uchungu kuipoteza nchi yao, wala kuzipoteza roho za wazee wao, za ndugu zao na za marafiki zao. Kwa mujibu wa kitabu cha huyo aliyejipa ujamadari wa hayo 'mavamizi' ya Januari 12, 1964, John Okello, amesema kuwa watu waliyokufa katika 'mavamizi' hayo ni 13,000. Hii ni idadi ndogo kabisa aliyopenda kuitaja.

Ukatili, ushenzi na unyama uliofanywa katika visiwa hivi vilivyokuwa na ustaarabu wa kupigiwa mfano, hauwezi hata kuhadithika. Wengi waliokuwa wanaijua Zanzibar, waliona taabu kuyaamini waliyokuwa wameyasikia yametokea Zanzibar kutokana na hayo yenye kuitwa 'mapinduzi'. Ilifika hadi, siku hiyo ya 'mavamizi' washenzi na makatili hao kuwanajisi maiti wa kike.

Kitendo hicho hakijawai kufanyika katika nchi nyingi ulimwenguni zenye ubinaadamu na ustaarabu wake. Lenye kuzidi kushangaza na kusikitisha ni kumsikia mwananchi mwenye kujulikana kuwa yeye ndiye mwongozi wa hao wenye kujiita "progressives" akasema kuwa, watu waliyouliwa katika hayo yenye kuitwa 'mapinduzi' ni 491! Duh!

Mwenyewe Okello alieongoza hayo mauwaji amesema kuwa wamekufa wananchi 13,000. Hata wangekuwa watano tu, bali ni binaadamu, ni wananchi, jee, ndio wawe wamestahiki kuuliwa kwa kuvamiwa nchi yao na wageni ambao wewe na wenzio kama wewe mmechanganyika na hao wageni katika kuifisidi nchi na wananchi wake? La kustaajabisha zaidi - ni pale ilipojulikana kuwa haya yote yalipangwa kabla - kwa siku 30 tu yaaani Desemba 10 mpaka Januari 11 ilitosha kujuwa uovu wa Serikali hata ikastahiki kupinduliwa? Hata ingelikuwa ni ovu hivyo, bali njia za kuiondowa za kikatiba zilikuwepo ambazo zingaliweza kutumika, khasa na hao Wapinzani. Haikuhitaji hata kidogo kutumia nguvu. Lakini hakika khasa ni kuwa mambo yalikwisha pangwa zamani, hayo yalikuwa ni matekelezo tu!!
 
drwho,

Good question. Atupe source yake siyo kuandika tu yale anayoyafikiria moyoni mwake. Kama asemavyo rafiki yangu FD lazima uangalie kila upande wa shillingi, lakini toa source.
 
Maana kuna watu kibao walikuwa mashujaa wa Tanzania waliachwa ka kusudi wakati wanaandika historia sasa hizi kelele za Okello naona haziishi

Iweje watu kama akina Suedi Kagasheki na Dosa Aziz wasipewe kipaumbele wakati Okello mnataka kumfanya Mungu Mtu?

Charity begins at home na tunao our sons and daughters ambao walipigania na kumwaga damu zao pale lakini husikii kitu.
 
Okello was a foreigner lakini kazi yake ilipokwisha akaambiwa kuwa muda wake ushaisha aanze

Sasa kuna jopo linaanza ku re write history

Huko nyuma walifanya hayo na leo hii wanarudia hayo hayo.
 
Besty,

Tulia kwanza, are you allright?!?, tunazungumzia utaifa, Znz ni taifa sio kabila, dalili za kupenda ukabila ni dalili za ubinafsi na ufinyu wa kufikiri.

FD

Kuna sehemu ambayo nimezungumzia ukabila? au umeshindwa kuelewa nilicho andika? Fikiri kabla ya kujibu tafadhali, kina Chief Mkwawa, Mangi Sina, Mangi Mandara, Wakina Chief Songea Mbano na Chief Chabruma wa kule Ruvuma, au Saidi Milambo wa tabora, wakina Isike, Kinjekitile, au Chief Masanja, Chief Mataka wa kule kwa wayao hawa ni alama ya taifa letu la Tanzania na ndio hawa tunapaswa kuwaenzi, watu hawa walionyesha uzalendo wa hali ya juu kulitetea Taifa letu la Tanganyika.
 
Mzee Philemon ahsante kwa kutoa topic hiii.Kwa ukweli mchango wa Okello katika mapinduzi ya waafrika umesahaulika sana.Inatakiwa ijengwe sanamu kubwa ya Okello kwa kuwa naamini kuwa huyu ni shujaa na jasiri mkubwa kuliko wote afrika ya mashariki,sidhani kama kuna mwanamapinduzi yoyote anayemkaribia huyu.

Bahati mbaya mafanikio yake yametekwa na karume na wengine....lakini naamini Tanzania na Zanzibar tutamkumbuka mtu huyu miaka ijayo..wakati wanahistoria wetu watakapoacha mtindo wao wa kuchanganya historia na siasa.

Ndio watu wengi walikufa,lakini revolution sio tea party,watu wanakufa lakini mafanikio ya kuondoa tabaka la makupe ambao waliwatweka wazanzibari mika zaidi ya 500 ya utumwa sio mchezo.

Cha kushangaza, 'wanahistoria' wetu wa so called udsm no one among them has ever written anything on Okello,wenywewe huangalia 'mashujaa' wa nje tu.

Ni aibu kubwa kwa watanzania!!!

Ahsante Phil kwa insight yako!!
 
kina Chief Mkwawa, Mangi Sina, Mangi Mandara, Wakina Chief Songea Mbano na Chief Chabruma wa kule Ruvuma, au Saidi Milambo wa tabora, wakina Isike, Kinjekitile, au Chief Masanja, Chief Mataka wa kule kwa wayao hawa ni alama ya taifa letu la Tanzania

Kweli machifu wetu hawa walionyesha uzalendo halisi , bila influence yeyote ya nje, licha ya kuwa jamii zao ziliishi kwenye 'ujima' (afrika ya leo, wapinzani/wanaharakati wengi, hubebwa na wageni). Chifu tuliyefundishwa kumtukana, Mangungo wa Msovero, aliyeuza ardhi kwa wageni, leo hii warithi wake tunawasifia kwa kuinua uchumi
 
[URL="home.globalfrontiers.com/zanzibar/nine%20hour%20revolution.htm"]home.globalfrontiers.com/zanzibar/zanzibar_revolution.htm[/URL]

Please members, go through these catches above. I am afraid to say that Mapinduzi yanayosheherekewa lewa its just a nightmare, I dont see anywere unless in zanzaibar gorvernment side of story the role of abeid karume and fellows in revulution, walijificha hadi kina Okello walipomaliza kazi ndio wakaibuka. Revolutionarry gorvernment should come out watuambie kwa nini hawataki kumsikia okello na pia inaonekana wwaliopigana kikweli hawajaenziwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…