Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar: Kumbe Waarabu Hawakufukuzwa! Walikimbia Wenyewe - Mzee Sukari

Pasco,
Kipi kinachokufanya wewe uamini kuwa Zanzibar kuna watu
hawastahili kuwapo ndani ya visiwa vile?

Ikiwa kufungua uzi wa kuufungua uzi ni wewe tujadili hili la
nani ni raia wa Zanzibar na nani si raia.
Mkuu Maalim Mohamed Said, hakuna popote niliposema kuwa Zanzibar kuna watu hawastahili kuwapo ndani ya visiwa vile!.

Nilichosema huko nyuma na nina sema tena na tena, Zanzibar ina wenyewe halisi Wazanzibari, waliokuwa chini ya Utawala wa Mwinyi Mkuu!, na Zanzibar ina wageni waalikwa, utawala wa Sultani, uliokaribishwa na Mwinyi Mkuu ili kumdhibiti Mreno asiviteke visiwa hivyo!.

Huyo mgeni mwalikwa, Sultani baada ya kukaribishwa kwa kazi maalum tuu, ile kazi ilipokamilika, yeye alihamia jumla!, sii yeye tuu bali na kuhamisha makao makuu ya ufalme wake toka Bara Arab nchi ya Oman na kuihamishia bara la Afrika katika visiwa vya Zanzibar, yeye sasa sio mgeni mwalikwa tena, sasa yeye ndio akawa mtawala wa Zanzibar na sii tena Mwinyi Mkuu!.

Kwa kadri miaka ilivyopita, ukoo wa Sultani mgeni na wote aliokuja nao, wakazaliana na kuzaliana na kuzaliana hadi kuwa wengi ajabu!. Wageni wote hawa waliozaliwa Zanzibar sii Waarabu tena bali wote ni Wanzanzibari wenye asili ya Waarabu, na muingiliano na wenyeji, ukatengeneza kizazi chengine cha machotara ambao nao ni Wazanzibari pia!. Ulifikia wakati wageni wote waliokuja kutoka Omani, waliishatangulia mbele ya haki, na wazaliwa wao wote waliofuatia, wamezaliwa Zanzibar, hivyo kwa kizazi kilichopo, na utawala uliopo waliamimi visiwa hivyo ndio kwao, ndio mali yao na kuvitawala ni haki na halali yao, tena hawa waliopo hawakuijua habari ya Mwinyi Mkuu wala kujua kulikuwa na makubaliano gani kati ya Mwinyi Mkuu kumkaribisha Sultani na kumpisha kiti!.Waliopo maadamu wamezaliwa Zanzibar na wamezaliwa katika ukoo wa Sultani, kwao Zanzibar ni kwao, Zanzibar ni yao na kila kilichomo ni mali yao!, hivyo na kuitawala milele ni halali yao!.

Katika miaka hiyo, pia kizazi cha wenyeji ukoo wa Mwinyi Mkuu na watu wao, wenye Zanzibar yao, kiliendelea kuzaliana na kuongezeka!, kikafikia kipindi zile sababu zilizomfanya Mwinyi Mkuu kuwakaribisha wageni kuja kuitawala Zanzibar, hazikuwepo tena!. Hakuna ajuaye makubaliano kati ya Mwinyi Mkuu na Sultan Sayyed Said yalikuwaje!. Hivyo wenye Zanzibar yao wakaanza kuhoji na kuitaka Zanzibar yao kutoka kwa wageni wenyeweji waliojimilikisha visiwa hivyo!.

Jee wajua kiliwakuta nini wajukuu hawa wa Mwinyi Mkuu waliodai haki yao?!, naomba hili nisiliseme humu, likazua mjadala mwingine kwa watu kubaki midomo wazi kwa kutoamimi kuwa binadamu mmoja anaweza kumfanyia unyama wa kiwango hicho binaadamu mwingine, kunaweza kupelekea watu tukaishia kuapizana humu!.

Harakati hizi za wenye chao kuidai haki yao, dhidi ya dhulma ya mgeni mwenyeji aliyepora hali na halali yao, ilifikia mwisho kwa Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar!, mwenye chake alichukua kilicho chake mwenye halali nacho, kwa kufanya waliochofanya, huku mgeni mwenyeji aliyeamini na yeye hicho alichonacho nacho ni chake na halali yake, hivyo hicho alichofanyiwa na wenyeji ni dhulma!.

Wakati mmoja anashangilia kurejesha kilicho chake mikononi mwake kwa kuyaita ni Mapinduzi Matukufu, yaliyorejesha hishma ya ukoo wa Mwinyi Mkuu kwenye visiwa hivyo, na kushangilia kwa neno "Mapinduzi Daima" ambayo yalihusisha umwagaji mkubwa wa damu!, mwingine anaililia damu iliyomwaika kwa kuielezea ni dhulma kubwa waliofanyiwa na wamwagaji damu hao!.

Mada yangu ya uzi huu ni shuhuda wa kilichotokea siku hiyo, ambapo wahusika wakuu wote ni Wazanzibari, mpindua na mpinduliwa, sasa kuna watu wanadhani mpinduliwa alitimuliwa toka katika visiwa hivyo!, ukweli ni kuwa hakuna aliyefukuzwa katika visiwa hivyo!, waliovikimbia visiwa hivyo, walikimbia wenyewe!, hawakufuzwa!.

Zanzibar ni ya wote, wenye halali yao, na wageni wakaribishwa ambao sasa sasa nao wamegeuka wenyeji!.

Jumatatu njema!.

Pasco
 
Mkuu Maalim Mohamed Said, hakuna popote niliposema kuwa Zanzibar kuna watu hawastahili kuwapo ndani ya visiwa vile!.

Nilichosema huko nyuma na nina sema tena na tena, Zanzibar ina wenyewe halisi Wazanzibari, waliokuwa chini ya Utawala wa Mwinyi Mkuu!, na Zanzibar ina wageni waalikwa, utawala wa Sultani, uliokaribishwa na Mwinyi Mkuu ili kumdhibiti Mreno asiviteke visiwa hivyo!.

Huyo mgeni mwalikwa, Sultani baada ya kukaribishwa kwa kazi maalum tuu, ile kazi ilipokamilika, yeye alihamia jumla!, sii yeye tuu bali na kuhamisha makao makuu ya ufalme wake toka Bara Arab nchi ya Oman na kuihamishia bara la Afrika katika visiwa vya Zanzibar, yeye sasa sio mgeni mwalikwa tena, sasa yeye ndio akawa mtawala wa Zanzibar na sii tena Mwinyi Mkuu!.

Kwa kadri miaka ilivyopita, ukoo wa Sultani mgeni na wote aliokuja nao, wakazaliana na kuzaliana na kuzaliana hadi kuwa wengi ajabu!. Wageni wote hawa waliozaliwa Zanzibar sii Waarabu tena bali wote ni Wanzanzibari wenye asili ya Waarabu, na muingiliano na wenyeji, ukatengeneza kizazi chengine cha machotara ambao nao ni Wazanzibari pia!. Ulifikia wakati wageni wote waliokuja kutoka Omani, waliishatangulia mbele ya haki, na wazaliwa wao wote waliofuatia, wamezaliwa Zanzibar, hivyo kwa kizazi kilichopo, na utawala uliopo waliamimi visiwa hivyo ndio kwao, ndio mali yao na kuvitawala ni haki na halali yao, tena hawa waliopo hawakuijua habari ya Mwinyi Mkuu wala kujua kulikuwa na makubaliano gani kati ya Mwinyi Mkuu kumkaribisha Sultani na kumpisha kiti!.Waliopo maadamu wamezaliwa Zanzibar na wamezaliwa katika ukoo wa Sultani, kwao Zanzibar ni kwao, Zanzibar ni yao na kila kilichomo ni mali yao!, hivyo na kuitawala milele ni halali yao!.

Katika miaka hiyo, pia kizazi cha wenyeji ukoo wa Mwinyi Mkuu na watu wao, wenye Zanzibar yao, kiliendelea kuzaliana na kuongezeka!, kikafikia kipindi zile sababu zilizomfanya Mwinyi Mkuu kuwakaribisha wageni kuja kuitawala Zanzibar, hazikuwepo tena!. Hakuna ajuaye makubaliano kati ya Mwinyi Mkuu na Sultan Sayyed Said yalikuwaje!. Hivyo wenye Zanzibar yao wakaanza kuhoji na kuitaka Zanzibar yao kutoka kwa wageni wenyeweji waliojimilikisha visiwa hivyo!.

Jee wajua kiliwakuta nini wajukuu hawa wa Mwinyi Mkuu waliodai haki yao?!, naomba hili nisiliseme humu, likazua mjadala mwingine kwa watu kubaki midomo wazi kwa kutoamimi kuwa binadamu mmoja anaweza kumfanyia unyama wa kiwango hicho binaadamu mwingine, kunaweza kupelekea watu tukaishia kuapizana humu!.

Harakati hizi za wenye chao kuidai haki yao, dhidi ya dhulma ya mgeni mwenyeji aliyepora hali na halali yao, ilifikia mwisho kwa Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar!, mwenye chake alichukua kilicho chake mwenye halali nacho, kwa kufanya waliochofanya, huku mgeni mwenyeji aliyeamini na yeye hicho alichonacho nacho ni chake na halali yake, hivyo hicho alichofanyiwa na wenyeji ni dhulma!.

Wakati mmoja anashangilia kurejesha kilicho chake mikononi mwake kwa kuyaita ni Mapinduzi Matukufu, yaliyorejesha hishma ya ukoo wa Mwinyi Mkuu kwenye visiwa hivyo, na kushangilia kwa neno "Mapinduzi Daima" ambayo yalihusisha umwagaji mkubwa wa damu!, mwingine anaililia damu iliyomwaika kwa kuielezea ni dhulma kubwa waliofanyiwa na wamwagaji damu hao!.

Mada yangu ya uzi huu ni shuhuda wa kilichotokea siku hiyo, ambapo wahusika wakuu wote ni Wazanzibari, mpindua na mpinduliwa, sasa kuna watu wanadhani mpinduliwa alitimuliwa toka katika visiwa hivyo!, ukweli ni kuwa hakuna aliyefukuzwa katika visiwa hivyo!, waliovikimbia visiwa hivyo, walikimbia wenyewe!, hawakufuzwa!.

Zanzibar ni ya wote, wenye halali yao, na wageni wakaribishwa ambao sasa sasa nao wamegeuka wenyeji!.

Jumatatu njema!.

Pasco
Pasco,
Ikiwa hali ya Zanzibar ndiyo hii kama unavyoiona wewe ya kuwa kuna
''Mapinduzi Mtakatifu,'' na Mapinduzi Daima,'' inakuwaje CCM Zanzibar
wameshindwa chaguzi tano mfululizo?
 
Pasco..mm nipo na ww nadhani ww unataka kujua kama mm ninavyo takakujua nisilolijua.
kibumpwini unaita ya urongo mm nimekuuliza simulizi za mzee Aman Thani na Ali Barwani nk nazo nizaurongo?
Huja yangu hapa sio kumtafuta mshindi hoja yangu ni kuelimika na kueleweshana.
Mkuu Sahim, hii simulizi ya Mzee Sukari ameisimulia katika BBC Swahili, ipo na unaweza kuifuatilia na kuisikia kwa masikio yako!.
Baada ya mapinduzi Zanzibar - BBC Swahili - BBC.com
Zanzibar na miaka 51 ya Mapinduzi - BBC Swahili

Naomba link nisikilize simulizi ya Amani Thani na Ali Barwani ili nami nisikie kwa masikio yangu ili kuepuka kulishwa urongo?!.

Pasco
 
Pasco,
Ikiwa hali ya Zanzibar ndiyo hii kama unavyoiona wewe ya kuwa kuna
''Mapinduzi Mtakatifu,'' na Mapinduzi Daima,'' inakuwaje CCM Zanzibar
wameshindwa chaguzi tano mfululizo?
Mkuu Maalim Mohamed Said, sababu ni simple!, jee wajua huyu mgeni aliyekaribishwa na Mwinyi Mkuu, aliofanya nini ukoo wa Mwinyi Mkuu ili usije tena kuchukua kilicho chake?!, aliu wipe out!.

Kaitafute historia ya Yusufu alipouzwa utumwani Misri na nini kilitokea, ndivyo vivyo hivyo hao wageni walivyozaliana kwa wingi hivyo hata uchaguzi ukifanyika kesho, lazima watashinda kwa wingi wao!, na ndio maana kila chaguzi lazima zitumike mbinu kuhakikisha mshindi ni lazima awe mtu wa ukoo wa Mwinyi Mkuu na sio hao wageni walowezi wakaazi wa Zanzibar.

Hili nimelizungumza sana hapa
Imethibitishwa pasi na shaka kuwa CUF Ndio Iliyoshinda Kihalali, Zanzibar !.
Jee Kuna Uwezekano Siku Zote Huwa Hazitoshi, Bali Zinatosheshwa ...

Pasco
 
Mkuu Maalim Mohamed Said, sababu ni simple!, jee wajua huyu mgeni aliyekaribishwa na Mwinyi Mkuu, aliofanya nini ukoo wa Mwinyi Mkuu ili usije tena kuchukua kilicho chake?!, aliu wipe out!.

Kaitafute historia ya Yusufu alipouzwa utumwani Misri na nini kilitokea, ndivyo vivyo hivyo hao wageni walivyozaliana kwa wingi hivyo hata uchaguzi ukifanyika kesho, lazima watashinda kwa wingi wao!, na ndio maana kila chaguzi lazima zitumike mbinu kuhakikisha mshindi ni lazima awe mtu wa ukoo wa Mwinyi Mkuu na sio hao wageni walowezi wakaazi wa Zanzibar.

Hili nimelizungumza sana hapa
Imethibitishwa pasi na shaka kuwa CUF Ndio Iliyoshinda Kihalali, Zanzibar !.
Jee Kuna Uwezekano Siku Zote Huwa Hazitoshi, Bali Zinatosheshwa ...

Pasco
Pasco,
Hao watu unaosema wa Mwinyi Mkuu hawapo Zanzibar.
Wangekuwapo wangekuwa wanapiga kura kupata ushindi.

Hao watu wa Mwinyi Mkuu wangekuwapo wangepiga kura
ya maoni kukataa serikali ya Umoja wa Kitaifa.

Hao watu wa Mwinyi Mkuu wako katika fikra zako za kubuni.
 
Pasco
Mkuu Sahim, hii simulizi ya Mzee Sukari ameisimulia katika BBC Swahili, ipo na unaweza kuifuatilia na kuisikia kwa masikio yako!.
Baada ya mapinduzi Zanzibar - BBC Swahili - BBC.com
Zanzibar na miaka 51 ya Mapinduzi - BBC Swahili

Naomba link nisikilize simulizi ya Amani Thani na Ali Barwani ili nami nisikie kwa masikio yangu ili kuepuka kulishwa urongo?!.

Pasco
Pasco,
Hivi maneno yako mengi ubishi usiokwisha kumbe hata Aman Thani
humjui?

Ndiyo nakuambia huna elimu ya kutosha kufanya mjadala huu.

Ingia mohammedsaid.com utasoma na kusikiliza mengi katika historia
ya Zanzibar.
 
Pasco,
Hao watu unaosema wa Mwinyi Mkuu hawapo Zanzibar.
Wangekuwapo wangekuwa wanapiga kura kupata ushindi.

Hao watu wa Mwinyi Mkuu wangekuwapo wangepiga kura
ya maoni kukataa serikali ya Umoja wa Kitaifa.

Hao watu wa Mwinyi Mkuu wako katika fikra zako za kubuni.
Mkuu Maalim Mohamed Said, usemayo ndio ukweli wako kudhani kuwa watu wa Mwinyi Mkuu hawapo tena Zanzibar kutokana na ulivyoaminishwa na Sultan kuwa alikwisha waangamiza wote kabisa kwa ku wa wipe out wote toka kwenye uso wa dunia!. Hata mti ukiukata tuu bila kungoa mizizi, uka relax kuwa umemaliza kazi, kutaibuka kitu kinachoitwa machipukizi, haya huwa mengi na hutapakaa kote kila kwenye mizizi!.

Sultani kwa kudhani amewatekeza ukoo wote wa Mwinyi Mkuu ili visiwa vile viwe mali yake milele!, hakujua kuwa alikata tuu shina, machipukizi ya Mwinyi Mkuu ndio hayo yaliyomuondoa kwa kumshtukiza bila kutegemea!.

Endeleeni kujifariji kuwa Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yalifanywa na mamluki toka Kipumbini, hivyo wanaoyalinda mapinduzi hayo na kuyaenzi nao pia ni mamluki?!. Unaweza kusaidiwa kuleta ukombozi kama alivyosaidia John Okello, lakini anayeimba kibwagizo cha "Mapinduzi Daima" ni Okelo?!, anayeyalinda Mapinduzi na kuyaenzi ni Okelo na watu wa Kupwembini?!.

Ukiona mtu anajibu hoja kwa negation kuwa kitu fulani hakipo, ujue huyo ni mtu aliyefilisika hoja!.
Hapa kwenye uzi huu, hoja kubwa ni Sultani na Waarabu hawakufukuzwa Zanzibar baada ya yale Mapinduzi Matukufu, bali walikimbia wenyewe!. Kwa kawaida hoja za msingi zikiisha uzi unakuwa hauchangiwi tena unamalizika!, kama bado kuna hoja, leta, kama hakuna tena hoja, acha uzi ujimalizie zake, usije kutuponza tukaja kuapizana humu ati na sisi tuonjeshwe adha ya Mapinduzi!.

Pasco
 
Mkuu Sahim, hii simulizi ya Mzee Sukari ameisimulia katika BBC Swahili, ipo na unaweza kuifuatilia na kuisikia kwa masikio yako!.
Baada ya mapinduzi Zanzibar - BBC Swahili - BBC.com
Zanzibar na miaka 51 ya Mapinduzi - BBC Swahili

Naomba link nisikilize simulizi ya Amani Thani na Ali Barwani ili nami nisikie kwa masikio yangu ili kuepuka kulishwa urongo?!.

Pasco
Pasco mm sina asili ya ubishi na sina asili ya kupenda kuitwa mshindi.
Na siamini kwa uwelewa wako na taaluma kuwa bado hujamsikia mzee Thani au mzee mzee Baruwani.
Nahisi unataka ushindani kwa mambo yasio hitaji ushindani.
Huku nyuma nilikuambia napenda kuelimika na kuelimishwa sipendi kushindana.
Mzee sukari kasema waarabu hawakufukuzwa bali waliondoka mm sina ubishi na hilo.
Lakini waswahili wanamsemo wao AKUFUKUZAE HAKUAMBII TOKA.
Mzee sukari amesama anayo yajua lakini kuna wengi tu walio tamka zaidi ya mzee sukari.
Mm nakushauri usipende kushinda kwa vitu visivyo hitaji mshindi.
Mm ni muislam naamini maandiko niliyo yakuta ya dini yangu bila kuwasikia walio andika.
Naamini na ww ni mkiristo unaamini maadiko yako bila kupata link ya alie andika.
Tukianza kuamini sauti za watu bila kuamini maandiko tutakuwa hatufiki tunapo pahitaji.
Pasco kama umeweza kuamini maneno ya Mwinyi mkuu karne zilizo pita bila link ya sauti yake vipi hutaki kuamini ya watu kama mzee AMANI THANI NA MZEE BARWANI WALIOFARIKA JUZI TU?
 
Mohamed Said umebanwa kwenye pembe ya ukuta, hoja ya Pasco umeshindwa kuijibu.
Fakalava,
Labda tunasoma post tofauti.

Anachosema Pasco ni kutaka kumsikiliza Aman Thani.
Mimi nimempa zaidi ya Aman Thani.

Nimemwambia aingie katika blog yangu atapata mengi
zaidi ya Aman Thani katika historia ya Zanzibar.

Ikiwa kuna jambo maalum wewe unataka nifanye sema
maana Pasco kanielewa na ndiyo maana yuko kimya.

Jaribu na wewe kuingia: mohammedsaid.com
 
Mkuu Maalim Mohamed Said, usemayo ndio ukweli wako kudhani kuwa watu wa Mwinyi Mkuu hawapo tena Zanzibar kutokana na ulivyoaminishwa na Sultan kuwa alikwisha waangamiza wote kabisa kwa ku wa wipe out wote toka kwenye uso wa dunia!. Hata mti ukiukata tuu bila kungoa mizizi, uka relax kuwa umemaliza kazi, kutaibuka kitu kinachoitwa machipukizi, haya huwa mengi na hutapakaa kote kila kwenye mizizi!.

Sultani kwa kudhani amewatekeza ukoo wote wa Mwinyi Mkuu ili visiwa vile viwe mali yake milele!, hakujua kuwa alikata tuu shina, machipukizi ya Mwinyi Mkuu ndio hayo yaliyomuondoa kwa kumshtukiza bila kutegemea!.

Endeleeni kujifariji kuwa Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yalifanywa na mamluki toka Kipumbini, hivyo wanaoyalinda mapinduzi hayo na kuyaenzi nao pia ni mamluki?!. Unaweza kusaidiwa kuleta ukombozi kama alivyosaidia John Okello, lakini anayeimba kibwagizo cha "Mapinduzi Daima" ni Okelo?!, anayeyalinda Mapinduzi na kuyaenzi ni Okelo na watu wa Kupwembini?!.

Ukiona mtu anajibu hoja kwa negation kuwa kitu fulani hakipo, ujue huyo ni mtu aliyefilisika hoja!.
Hapa kwenye uzi huu, hoja kubwa ni Sultani na Waarabu hawakufukuzwa Zanzibar baada ya yale Mapinduzi Matukufu, bali walikimbia wenyewe!. Kwa kawaida hoja za msingi zikiisha uzi unakuwa hauchangiwi tena unamalizika!, kama bado kuna hoja, leta, kama hakuna tena hoja, acha uzi ujimalizie zake, usije kutuponza tukaja kuapizana humu ati na sisi tuonjeshwe adha ya Mapinduzi!.

Pasco
Pasco,
Mimi swali langu ni dogo sana.

Nakuuliza kuwa mbona CCM Zanzibar imeshindwa kila uchaguzi
kwa jumla chaguzi tano toka mwaka wa 1995?

Inakuwaje CCM Zanzibar haiwezi kushinda uchaguzi ilhali wajukuu
wa Mwinyi Mkuu wapo?
 
Fakalava,
Labda tunasoma post tofauti.

Anachosema Pasco ni kutaka kumsikiliza Aman Thani.
Mimi nimempa zaidi ya Aman Thani.

Nimemwambia aingie katika blog yangu atapata mengi
zaidi ya Aman Thani katika historia ya Zanzibar.

Ikiwa kuna jambo maalum wewe unataka nifanye sema
maana Pasco kanielewa na ndiyo maana yuko kimya.

Jaribu na wewe kuingia: mohammedsaid.com

Fakalava,
Ingia hapa:
Mohamed Said: AMAN THANI ANAMWELEZA MANDERA NA MATESO YA KUNG'OA KUCHA 9
 
Pasco,
Mimi swali langu ni dogo sana.

Nakuuliza kuwa mbona CCM Zanzibar imeshindwa kila uchaguzi
kwa jumla chaguzi tano toka mwaka wa 1995?

Inakuwaje CCM Zanzibar haiwezi kushinda uchaguzi ilhali wajukuu
wa Mwinyi Mkuu wapo?
Hapa sasa naona unachanganya mada!. kwenye sheria ya uchaguzi, mshindi ni anayetangazwa!, hivyo japo kila siku wajukuu wa Sultani ndio wanaochaguliwa, anayetangazwa mshindi siku zote ni mjukuu wa Mwinyi Mkuu!. Hao ndio wenye Zanzibar yao!. Maadam anayetangazwa mshindi ni CCM, then mshindi ni CCM mara zote tano, CUF ndio kashindwa mara zote 5!.

Pasco
 
Hapa sasa naona unachanganya mada!. kwenye sheria ya uchaguzi, mshindi ni anayetangazwa!, hivyo japo kila siku wajukuu wa Sultani ndio wanaochaguliwa, anayetangazwa mshindi siku zote ni mjukuu wa Mwinyi Mkuu!. Hao ndio wenye Zanzibar yao!. Maadam anayetangazwa mshindi ni CCM, then mshindi ni CCM mara zote tano, CUF ndio kashindwa mara zote 5!.

Pasco
Pasco,
Unalosema si jipya sote tunalijua.

Hayo ndiyo yanayoeleza ukweli wa historia ya Zanzibar kuwa
serikali iko madarakani lakini hawana ridhaa ya wananchi.
 
Ni bila ridhaa ya wageni wakaazi, na sio wananchi.

P.
Pasco,
Hujui historia ya Zanzibar.

Hayo unayosema mbele ya wajuzi ni kichekesho kwa kuwa
unazungumza historia ya watu waliokuja Zanzibar 1700s na
makaburi ya baba wa babu wa babu yako pale na ukipenda
utaonyeshwa.

Wako pia waliokuja 1900s kutoka Tanganyika na leo hii kwao
kunafahamika kuwa ni Kisarawe au Mbeya nk.

Lakini hawa wote ni Wazanzibari maana huyo wa Kisarawe na
Mbeya pengine baada ya miaka 100 hana kumbukumbu yoyote
ya kwao.

Anakokujua yeye ni Zanzibar Kiembe Samaki au Kikwajuni.

Ni ujinga uliopea kudhani kuwa hawa wa Kisarawe na Mbeya
wana haki zaidi ya huyu kitukuu wa Muomani aliyefika Zanzibar
1700 na akachanganya damu na Muafrika.

Hakika ni ujinga uliopea hiki kitukuu chenye damu ya Kiarabu
na Kinyamwezi kumbagua na kumuita ati ni mgeni mkazi.

Lakini kubwa hawa ni Waislam yule mwenye asili ya Oman na
huyo mwenye asili ya Kisarawe na Mbeya.

Hawa wote wanajua Allah nini kasema kuhusu ubaguzi.

Hiki ni kisa cha kweli na wewe ukishughulisha akili yako utawajua
ni nani hawa niliowakusudia na wako wengi Zanzibar kila ukoo wapo
wale waliokuja 1700 na wale waliokuja miaka ya karibuni.

Hiyo hapo chini ni kijiji cha mmoja Wazanzibari ambacho mababu
zake walitoka na kuja Zanzibar sasa zaidi ya miaka 400.

Picha hiyo nimeipiga mimi na aliponitembeza kijijini kwao nilipata
picha ya Zanzibar Stone Town.

Alinichukua na kwenda kunionyesha asili yao na kunambia kuwa
anayo hadi majina ya waliotoka kijiji hicho kuja Zanzibar babu yake
akiwa mmojawao.

Kinachofurahisha ni kuwa ukiwaangalia wale ndugu zake katika
hicho kijiji wao wamebaki na Uarabu wao huyu rafiki yangu yeye
ni Mwafrika kuanzia unyayo hadi nywele zake lakini nduguze bado
wanamtambua kuwa ni ndugu yao.

Hii ndiyo historia ya Oman na Zanzibar.


upload_2016-5-16_16-58-48.png
 
Pasco,
Hujui historia ya Zanzibar.

Hayo unayosema mbele ya wajuzi ni kichekesho kwa kuwa
unazungumza historia ya watu waliokuja Zanzibar 1700s na
makaburi ya baba wa babu wa babu yako pale na ukipenda
utaonyeshwa.

Wako pia waliokuja 1900s kutoka Tanganyika na leo hii kwao
kunafahamika kuwa ni Kisarawe au Mbeya nk.

Lakini hawa wote ni Wazanzibari maana huyo wa Kisarawe na
Mbeya pengine baada ya miaka 100 hana kumbukumbu yoyote
ya kwao.

Anakokujua yeye ni Zanzibar Kiembe Samaki au Kikwajuni.

Ni ujinga uliopea kudhani kuwa hawa wa Kisarawe na Mbeya
wana haki zaidi ya huyu kitukuu wa Muomani aliyefika Zanzibar
1700 na akachanganya damu na Muafrika.

Hakika ni ujinga uliopea hiki kitukuu chenye damu ya Kiarabu
na Kinyamwezi kumbagua na kumuita ati ni mgeni mkazi.

Lakini kubwa hawa ni Waislam yule mwenye asili ya Oman na
huyo mwenye asili ya Kisarawe na Mbeya.

Hawa wote wanajua Allah nini kasema kuhusu ubaguzi.

Hiki ni kisa cha kweli na wewe ukishughulisha akili yako utawajua
ni nani hawa niliowakusudia na wako wengi Zanzibar kila ukoo wapo
wale waliokuja 1700 na wale waliokuja miaka ya karibuni.

Hiyo hapo chini ni kijiji cha mmoja Wazanzibari ambacho mababu
zake walitoka na kuja Zanzibar sasa zaidi ya miaka 400.

Picha hiyo nimeipiga mimi na aliponitembeza kijijini kwao nilipata
picha ya Zanzibar Stone Town.

Alinichukua na kwenda kunionyesha asili yao na kunambia kuwa
anayo hadi majina ya waliotoka kijiji hicho kuja Zanzibar babu yake
akiwa mmojawao.

Kinachofurahisha ni kuwa ukiwaangalia wale ndugu zake katika
hicho kijiji wao wamebaki na Uarabu wao huyu rafiki yangu yeye
ni Mwafrika kuanzia unyayo hadi nywele zake lakini nduguze bado
wanamtambua kuwa ni ndugu yao.

Hii ndiyo historia ya Oman na Zanzibar.


View attachment 348183


Shukrani sana mzee wetu kwa darasa hizi labda hawa jamaa wataelewa , kama watafikiri wakiwa nje ya box
 
Back
Top Bottom