Hashil Seif Hashil: Mmoja wa wazalendo walioshiriki katika Mapinduzi ya Zanzibar mwaka 1964

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,920
30,261
1698438004522.jpeg

Nimepokea hivi punde kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Hashil Seif Hashili mmoja katika wazalendo walioshiriki katika mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka wa 1964.

Naomba niweka hapo chini kama kumbukumbu yangu kwake yale ambayo niliandika baada ya kusoma kitabu chake:

''Mimi, Umma Party na Mapinduzi ya Zanzibar.''

Hashili Seif baada ya kunisoma alinipigia simu kunishukuru na kusema kuwa kapendezewa na yote niliyoandika kuhusu yeye na kitabu alichoandika.

KITABU KATIKA KUMBUKUMBU YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

MIMI, UMMA PARTY NA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

Kuandika historia ya ukombozi katika nchi za Kiafrika kunahitaji ujasiri mkubwa sana na sababu yake ni kuwa Afrika ina historia rasmi.

Historia hii rasmi ni ile ambayo imepitishwa na kukubalika na watawala.

Historia hii ikishaandikwa ndiyo mwisho kwani haitoi nafasi ya kuwapo kwa historia nyingine itakayokwenda kinyume na hiyo.

Hii ni moja ya sifa ya siasa katika Afrika.

Historia rasmi ndiyo hiyo itakayokuwa katika mitaala kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu.

Hatari yake ni kuwa inasababisha na pengine kwa miaka mingi sana kusomeshwa historia yenye upungufu hadi pale atakapotokea mtu jasiri akaandika ukweli.

Wako watu bado wa hai na pengine wapo hapa ukumbini wanaijua historia ya mapinduzi ya Zanzibar kwa kuyaona mapinduzi yenyewe na kwa kushiriki lakini hawajanyanyua kalamu kuandika wala kufungua mdomo kuihadithia na watakwenda kaburini na watazikwa na historia zao ambazo laiti wangeliziandika nchi ingenufaika pakubwa.

Hashil Seif Hashil anastahili pongezi kwa ujasiri huu wa kutuandikia kitabu na kutueleza historia ya Zanzibar ambayo si wengi wanaijua khasa vijana waliozaliwa baada ya mapinduzi mwaka wa 1964 ambao kwa sasa ni watu wazima.

Kuiandika historia ya mapinduzi ya Zanzibar ni kazi inayohitaji, ushujaa kwani si rahisi kuieleza na ukakosa kuwaudhi baadhi ya watu na wengine watu wako wa karibu sana.

Afrika tuna utamaduni wa kuzifanya historia zetu kuwa kitu nyeti kwa hiyo iogopwe na isiguswe kwa kuigeuzageuza kutaka kujua undani wake.

Hashil Seif ni mwandishi jasiri na mtu huwezi kustaajabu kwa huu ujasiri wake utakapoijua historia yake binafsi.

Hashil Seif mwaka wa 1962 akiwa kijna mdogo kabisa wa umri wa miaka 26 alitoroka Zanzibar pamoja na wenzake wapatao 20 kwenda Cuba kupata mafunzo ya vita kwa nia ya kurejea Zanzibar na kupindua serikali na kuweka utawala wa Ki-Marxist.

Hili la kwanza na kaeleza katika kumbukumbu hizi.
Pili, Hashil Seif hajasita hata mara moja katika kitabu hiki kueleza kuwa yeye alikuwa mwanachama wa ZNP, maarufu kwa jina la ‘’Hizbu.’’

Katika historia ya Zanzibar baada ya mapinduzi neno, ‘’Hizbu,’’ lilikuwa linatisha na kuna watu na si wadogo hadi leo bado wana hofu kubwa ya kunasibishwa na historia yao katika Hizbu.

Katika kumbukumbu hizi Hashil Seif anaeleza historia yake ndani ya chama hiki na mchango wake kama kijana katika Youth Own Union (YOU) bila hofu wala wasiwasi wowote na hadi leo katika umri mkubwa wa miaka 80 bado ni komredi na hajabadili fikra zake za siasa za mrengo wa kushoto.

Katika kitabu hiki Hashil Seif anaeleza fikra zake kama bado yuko katika Zanzibar ya miaka ya 1960 bila ya kuongeza wala kupunguza nukta.

Hii ni moja ya mambo yanayokifanya kitabu hiki kiwe kiongozi katika kuijua historia ya mapinduzi na wanasiasa wake wa nyakati zile.

Ili kitabu kiwe kitabu ni lazima kiwe kina elimu mpya ambayo kabla haikuwa inajulikana.

Wazanzibari wengi, ukimtoa Dr. Harith Ghassany: ‘’Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru,’’ (2010), walioandika historia ya mapinduzi wote wamepita mle mle katika historia rasmi.

Msomaji hapati jipya isipokuwa tofauti ya jalada, jina la kitabu na la mwandishi.

Unapoanza kumsoma Hashil Seif mwanzoni tu unakuwa mfano wa mtu aliyekuwa kalala usingizi fofofo na ghafla anatokea mtu akammwagia maji baridi usoni na kwa maji yale akashtuka kutoka usingizini na pengine kwenye ndoto akawa karejea katika dunia ya kweli.

Hashil Seif anakifungua kitabu kwa majina ambayo hutayakuta katika historia tuliyoizoea ya mapinduzi ya Zanzibar.

Hashil Seif katika kitabu hiki kataja majina ambayo yalifutika katika historia ya Zanzibar na kama utayakuta basi yatakuwa yemetajwa, ‘’in passing,’’ kama Waingereza wasemavyo, yaani majina hayo yatakuwa yametajwa kijuujuu.

Nitatoa mfano kwa uchache.

Hashil anawataja mara kadhaa katika kitabu Abdulrahman Babu, Khamisi Abdallah Ameir, Ali Sultan Issa na Badawi Qullatein katika siasa za kupigania uhuru wa Zanzibar.

Ahmed Rajab mmoja wa makomredi, ambae kaupitia mswada wa kitabu hiki ameniandikia na kunifahamisha kuwa Khamis Abdallah Ameir kama ‘’Theoretician,’’ sifa hii hutaisoma katika kitabu lakini katika mawasiliano yangu na Ahmed Rajab hili kanieleza na akasema kuwa Khamis Abdallah Ameir hakuwa mwanachama wa kawaida katika harakati zile.

Hili lilidhihirika baada ya mapinduzi kwa Khamis Abdallah Ameir kuwa memba wa Baraza la Kwanza la Mapinduzi.

Khamis Abdallah Ameir sikupatapo kumsikia kabla mpaka nilipomuona hapa katika ukumbi huu katika muhadhara wa Abdallah Kassim Hanga na sasa kaletwa tena na Hashil Seif.

Babu, Ali Sultan na Badawi Qullatein hawahitaji maelezo.

Bahati mbaya sana kuwa kitabu hakikuwekwa faharasha yaani ‘’index,’’ lakini laiti ingekuwapo faharasha msomaji angeweza kuona umihumu wa wazalendo hawa waliotajwa katika kitabu hiki kwa kuangalia ni mara ngapi majina yao yametajwa katika historia hii.

Huu ni mfano mmoja tu katika majina mengi ambayo hayajatajwa katika historia ya Zanzibar lakini Hashil Seif ameyarejesha na kueleza historia za watu hao katika kupigania uhuru wa Zanzibar.

Msomaji atamsoma Ali Sultan Issa aliyekuwa Mkomunisti ndani ya ZNP, Badawi Qulattein, Salim Rashid aliyekuwa katibu wa kwanza wa Baraza la Mapinduzi.

Wazalendo hawa historia zao zina mvuto wa pekee kabla na baada ya mapinduzi.

Ali Sultan ndiye aliyetengezeza mpango mzima wa kuwapeleka vijana wa ZNP, Cuba kwa mafunzo ya kijeshi kujitayarisha kwa mapinduzi.

Haya ndiyo msomaji atakutananayo katika kitabu hiki na ikiwa ni hivi ndivyo hali ilivyokuwa wakati wa kupigania uhuru wa Zanzibar haiwi tabu kuelewa sifa za makomredi katika uongozi na mchango wao katika mapinduzi.

Tunamuomba Allah amsamehe ndugu yetu na amweke mahali pema peponi.

Amin.
 

Nimepokea hivi punde kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Hashil Seif Hashili mmoja katika wazalendo walioshiriki katika mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka wa 1964.

Naomba niweka hapo chini kama kumbukumbu yangu kwake yale ambayo niliandika baada ya kusoma kitabu chake:

''Mimi, Umma Party na Mapinduzi ya Zanzibar.''

Hashili Seif baada ya kunisoma alinipigia simu kunishukuru na kusema kuwa kapendezewa na yote niliyoandika kuhusu yeye na kitabu alichoandika.

KITABU KATIKA KUMBUKUMBU YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

MIMI, UMMA PARTY NA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

Kuandika historia ya ukombozi katika nchi za Kiafrika kunahitaji ujasiri mkubwa sana na sababu yake ni kuwa Afrika ina historia rasmi.

Historia hii rasmi ni ile ambayo imepitishwa na kukubalika na watawala.

Historia hii ikishaandikwa ndiyo mwisho kwani haitoi nafasi ya kuwapo kwa historia nyingine itakayokwenda kinyume na hiyo.

Hii ni moja ya sifa ya siasa katika Afrika.

Historia rasmi ndiyo hiyo itakayokuwa katika mitaala kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu.

Hatari yake ni kuwa inasababisha na pengine kwa miaka mingi sana kusomeshwa historia yenye upungufu hadi pale atakapotokea mtu jasiri akaandika ukweli.

Wako watu bado wa hai na pengine wapo hapa ukumbini wanaijua historia ya mapinduzi ya Zanzibar kwa kuyaona mapinduzi yenyewe na kwa kushiriki lakini hawajanyanyua kalamu kuandika wala kufungua mdomo kuihadithia na watakwenda kaburini na watazikwa na historia zao ambazo laiti wangeliziandika nchi ingenufaika pakubwa.

Hashil Seif Hashil anastahili pongezi kwa ujasiri huu wa kutuandikia kitabu na kutueleza historia ya Zanzibar ambayo si wengi wanaijua khasa vijana waliozaliwa baada ya mapinduzi mwaka wa 1964 ambao kwa sasa ni watu wazima.

Kuiandika historia ya mapinduzi ya Zanzibar ni kazi inayohitaji, ushujaa kwani si rahisi kuieleza na ukakosa kuwaudhi baadhi ya watu na wengine watu wako wa karibu sana.

Afrika tuna utamaduni wa kuzifanya historia zetu kuwa kitu nyeti kwa hiyo iogopwe na isiguswe kwa kuigeuzageuza kutaka kujua undani wake.

Hashil Seif ni mwandishi jasiri na mtu huwezi kustaajabu kwa huu ujasiri wake utakapoijua historia yake binafsi.

Hashil Seif mwaka wa 1962 akiwa kijna mdogo kabisa wa umri wa miaka 26 alitoroka Zanzibar pamoja na wenzake wapatao 20 kwenda Cuba kupata mafunzo ya vita kwa nia ya kurejea Zanzibar na kupindua serikali na kuweka utawala wa Ki-Marxist.

Hili la kwanza na kaeleza katika kumbukumbu hizi.
Pili, Hashil Seif hajasita hata mara moja katika kitabu hiki kueleza kuwa yeye alikuwa mwanachama wa ZNP, maarufu kwa jina la ‘’Hizbu.’’

Katika historia ya Zanzibar baada ya mapinduzi neno, ‘’Hizbu,’’ lilikuwa linatisha na kuna watu na si wadogo hadi leo bado wana hofu kubwa ya kunasibishwa na historia yao katika Hizbu.

Katika kumbukumbu hizi Hashil Seif anaeleza historia yake ndani ya chama hiki na mchango wake kama kijana katika Youth Own Union (YOU) bila hofu wala wasiwasi wowote na hadi leo katika umri mkubwa wa miaka 80 bado ni komredi na hajabadili fikra zake za siasa za mrengo wa kushoto.

Katika kitabu hiki Hashil Seif anaeleza fikra zake kama bado yuko katika Zanzibar ya miaka ya 1960 bila ya kuongeza wala kupunguza nukta.

Hii ni moja ya mambo yanayokifanya kitabu hiki kiwe kiongozi katika kuijua historia ya mapinduzi na wanasiasa wake wa nyakati zile.

Ili kitabu kiwe kitabu ni lazima kiwe kina elimu mpya ambayo kabla haikuwa inajulikana.

Wazanzibari wengi, ukimtoa Dr. Harith Ghassany: ‘’Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru,’’ (2010), walioandika historia ya mapinduzi wote wamepita mle mle katika historia rasmi.

Msomaji hapati jipya isipokuwa tofauti ya jalada, jina la kitabu na la mwandishi.

Unapoanza kumsoma Hashil Seif mwanzoni tu unakuwa mfano wa mtu aliyekuwa kalala usingizi fofofo na ghafla anatokea mtu akammwagia maji baridi usoni na kwa maji yale akashtuka kutoka usingizini na pengine kwenye ndoto akawa karejea katika dunia ya kweli.

Hashil Seif anakifungua kitabu kwa majina ambayo hutayakuta katika historia tuliyoizoea ya mapinduzi ya Zanzibar.

Hashil Seif katika kitabu hiki kataja majina ambayo yalifutika katika historia ya Zanzibar na kama utayakuta basi yatakuwa yemetajwa, ‘’in passing,’’ kama Waingereza wasemavyo, yaani majina hayo yatakuwa yametajwa kijuujuu.

Nitatoa mfano kwa uchache.

Hashil anawataja mara kadhaa katika kitabu Abdulrahman Babu, Khamisi Abdallah Ameir, Ali Sultan Issa na Badawi Qullatein katika siasa za kupigania uhuru wa Zanzibar.

Ahmed Rajab mmoja wa makomredi, ambae kaupitia mswada wa kitabu hiki ameniandikia na kunifahamisha kuwa Khamis Abdallah Ameir kama ‘’Theoretician,’’ sifa hii hutaisoma katika kitabu lakini katika mawasiliano yangu na Ahmed Rajab hili kanieleza na akasema kuwa Khamis Abdallah Ameir hakuwa mwanachama wa kawaida katika harakati zile.

Hili lilidhihirika baada ya mapinduzi kwa Khamis Abdallah Ameir kuwa memba wa Baraza la Kwanza la Mapinduzi.

Khamis Abdallah Ameir sikupatapo kumsikia kabla mpaka nilipomuona hapa katika ukumbi huu katika muhadhara wa Abdallah Kassim Hanga na sasa kaletwa tena na Hashil Seif.

Babu, Ali Sultan na Badawi Qullatein hawahitaji maelezo.

Bahati mbaya sana kuwa kitabu hakikuwekwa faharasha yaani ‘’index,’’ lakini laiti ingekuwapo faharasha msomaji angeweza kuona umihumu wa wazalendo hawa waliotajwa katika kitabu hiki kwa kuangalia ni mara ngapi majina yao yametajwa katika historia hii.

Huu ni mfano mmoja tu katika majina mengi ambayo hayajatajwa katika historia ya Zanzibar lakini Hashil Seif ameyarejesha na kueleza historia za watu hao katika kupigania uhuru wa Zanzibar.

Msomaji atamsoma Ali Sultan Issa aliyekuwa Mkomunisti ndani ya ZNP, Badawi Qulattein, Salim Rashid aliyekuwa katibu wa kwanza wa Baraza la Mapinduzi.

Wazalendo hawa historia zao zina mvuto wa pekee kabla na baada ya mapinduzi.

Ali Sultan ndiye aliyetengezeza mpango mzima wa kuwapeleka vijana wa ZNP, Cuba kwa mafunzo ya kijeshi kujitayarisha kwa mapinduzi.

Haya ndiyo msomaji atakutananayo katika kitabu hiki na ikiwa ni hivi ndivyo hali ilivyokuwa wakati wa kupigania uhuru wa Zanzibar haiwi tabu kuelewa sifa za makomredi katika uongozi na mchango wao katika mapinduzi.

Tunamuomba Allah amsamehe ndugu yetu na amweke mahali pema peponi.

Amin.
Mkuu Maalim Mohamad said , asante sana kwa taarifa hii. RIP Shujaa huyu.

Katika maadhimisho ya miaka 60 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, natamani washiriki wote wa Mapinduzi Matukufu hayo walio hai, waenziwe, na waliotangulia mbele ya haki, watajwe na familia zao zipokee chochote, as just a token of appreciation!.

Wana bodi, japo tuko kwenye harakati za kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge, kuna swali linanitatiza kuhusu Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, ambapo majibu yake sahihi, pia yanaweza kuwa ni kiashiria tosha cha mshindi wa urais wa Zanzibar, iwapo uchaguzi utakuwa huru na wa haki.

Swali hili lahusu ukweli haswa kuhusu Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya Januari 12, 1964, baada ya kuibuka kwa kitabu kingine kiitwacho "Kwaheri Ukoloni, Kwaheri Uhuru"
View attachment 2077603
kilichoandikwa na Mwanazouni wa Zanzibar, Dr. Harith Ghassany, kama kilivyofanyiwa mapitio na mwandishi Mohamed Said kwenye gazeti la Al-Nuur la leo.

Ghasanny anasema kumbe Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yalitekelezwa na askari mamluki wa Kimakonde (Wakata Mkonge) ambao waliongozwa na Mzee Mohamed Omar Mkwawa (Tindo) chini ya Amiri Jeshi wa jeshi la mamluki hao Victor Mkello (RIP). (kumbe amiri jeshi hakuwa Mganda John Okello pekee, bali pia Mkello yumo?!.

Mamluki hao walitumia zana zao za kukatia mkonge, zile sime za makali kuwili, walizisunda kwenye nguo zao za ndani na kusafirishwa kwa mitumbiwi usiku usiku kupitia Kipumbwi. Jee wale mashuhuda wa Mapinduzi yale Matukufu ya Zanzibar, wanayakubali haya?.

Pia mwandishi anamalizia kwa kusema hata mauaji ya Karume, hayakutekelezwa na wapinga Mapinduzi, bali ni miongoni mwa hao hao wanamapinduzi, baada ya kupishana kauli fulani fulani za uendeshaji wa Zanzibar baada ya Mapinduzi.

Nimesoma kitabu cha John Okello kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar,
View attachment 2077618
yeye anasema yake, vitabu kadhaa vya waandishi wazungu wanasema yao, historia tukuka ya Mapinduzi Matukufuya ya Zanzibar nayo nayo inasema kivyake, hivi hakuna any straight line yoyote kuhusu Mapinduzi hayo, ya Zanzibar?.
Jee yalipangwa na nani? Yalitekelezwaje?.
Nini haswa kilichotokea usiku ule wa Januari 11?.
Nani alifanya nini wapi?
Na mwisho tuzungumzie wafaidika wa Mapinduzi hayo Matukufu ya Zanzibar na bila kuwasahau wahanga wa Mapinduzi hayo ambao kwako yatakuwa sio Matukufu, ni kina nani haswa?, na kama kuleta amani na utangamano wa Zanzibar kuhusu Mapinduzi hayo kutahitajika kuundwa kwa Tume ya Ukweli na Upatanisho, "Truth and Reconciliation Commission" ili waliohasimiana kutokana na Mapinduzi hayo, wapatanishwe kwa maslahi mapana ya Zanzibar?.

Majibu ya maswali haya yatasaidia kujua mustakabali wa matokea ya uchaguzi wa Zanzibar kudhirihisha kuwa Wazanzibari ni wamoja, hakuna kundi la walishiriki Mapinduzi ndio wenye uhalali zaidi kuitawala Zanzibar kuliko wasioshiriki, after all kumbe Mapinduzi yenyewe, yametekelezwa na askari mamluki wa Kimakonde, toka mashamba ya mkonge Tanga!.

Pasco
Rejea za Mwandishi huyu kuhusu Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar
  1. Miaka 50 Ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, Bado Kuna Maswali Bila Majibu -1
  2. Neno "Matukufu" Katika Mapinduzi ya Zanzibar, Lilitoka Wapi, na Yana Utukufu Gani?!,
  3. Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar: Kumbe Waarabu Hawakufukuzwa! Walikimbia Wenyewe - Mzee Sukari
Tarehe kama ya leo 11/01/1964 miaka 60 iliyopita, ndio Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yalifanyika!. Alfajiri ya Tarehe 12 Januari, 1964 ilikuwa ni kutangazwa tuu!.

Nawatakia maadhimisho mema ya miaka 60 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Paskali
 
A

Nimepokea hivi punde kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Hashil Seif Hashili mmoja katika wazalendo walioshiriki katika mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka wa 1964.

Naomba niweka hapo chini kama kumbukumbu yangu kwake yale ambayo niliandika baada ya kusoma kitabu chake:

''Mimi, Umma Party na Mapinduzi ya Zanzibar.''

Hashili Seif baada ya kunisoma alinipigia simu kunishukuru na kusema kuwa kapendezewa na yote niliyoandika kuhusu yeye na kitabu alichoandika.

KITABU KATIKA KUMBUKUMBU YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

MIMI, UMMA PARTY NA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

Kuandika historia ya ukombozi katika nchi za Kiafrika kunahitaji ujasiri mkubwa sana na sababu yake ni kuwa Afrika ina historia rasmi.

Historia hii rasmi ni ile ambayo imepitishwa na kukubalika na watawala.

Historia hii ikishaandikwa ndiyo mwisho kwani haitoi nafasi ya kuwapo kwa historia nyingine itakayokwenda kinyume na hiyo.

Hii ni moja ya sifa ya siasa katika Afrika.

Historia rasmi ndiyo hiyo itakayokuwa katika mitaala kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu.

Hatari yake ni kuwa inasababisha na pengine kwa miaka mingi sana kusomeshwa historia yenye upungufu hadi pale atakapotokea mtu jasiri akaandika ukweli.

Wako watu bado wa hai na pengine wapo hapa ukumbini wanaijua historia ya mapinduzi ya Zanzibar kwa kuyaona mapinduzi yenyewe na kwa kushiriki lakini hawajanyanyua kalamu kuandika wala kufungua mdomo kuihadithia na watakwenda kaburini na watazikwa na historia zao ambazo laiti wangeliziandika nchi ingenufaika pakubwa.

Hashil Seif Hashil anastahili pongezi kwa ujasiri huu wa kutuandikia kitabu na kutueleza historia ya Zanzibar ambayo si wengi wanaijua khasa vijana waliozaliwa baada ya mapinduzi mwaka wa 1964 ambao kwa sasa ni watu wazima.

Kuiandika historia ya mapinduzi ya Zanzibar ni kazi inayohitaji, ushujaa kwani si rahisi kuieleza na ukakosa kuwaudhi baadhi ya watu na wengine watu wako wa karibu sana.

Afrika tuna utamaduni wa kuzifanya historia zetu kuwa kitu nyeti kwa hiyo iogopwe na isiguswe kwa kuigeuzageuza kutaka kujua undani wake.

Hashil Seif ni mwandishi jasiri na mtu huwezi kustaajabu kwa huu ujasiri wake utakapoijua historia yake binafsi.

Hashil Seif mwaka wa 1962 akiwa kijna mdogo kabisa wa umri wa miaka 26 alitoroka Zanzibar pamoja na wenzake wapatao 20 kwenda Cuba kupata mafunzo ya vita kwa nia ya kurejea Zanzibar na kupindua serikali na kuweka utawala wa Ki-Marxist.

Hili la kwanza na kaeleza katika kumbukumbu hizi.
Pili, Hashil Seif hajasita hata mara moja katika kitabu hiki kueleza kuwa yeye alikuwa mwanachama wa ZNP, maarufu kwa jina la ‘’Hizbu.’’

Katika historia ya Zanzibar baada ya mapinduzi neno, ‘’Hizbu,’’ lilikuwa linatisha na kuna watu na si wadogo hadi leo bado wana hofu kubwa ya kunasibishwa na historia yao katika Hizbu.

Katika kumbukumbu hizi Hashil Seif anaeleza historia yake ndani ya chama hiki na mchango wake kama kijana katika Youth Own Union (YOU) bila hofu wala wasiwasi wowote na hadi leo katika umri mkubwa wa miaka 80 bado ni komredi na hajabadili fikra zake za siasa za mrengo wa kushoto.

Katika kitabu hiki Hashil Seif anaeleza fikra zake kama bado yuko katika Zanzibar ya miaka ya 1960 bila ya kuongeza wala kupunguza nukta.

Hii ni moja ya mambo yanayokifanya kitabu hiki kiwe kiongozi katika kuijua historia ya mapinduzi na wanasiasa wake wa nyakati zile.

Ili kitabu kiwe kitabu ni lazima kiwe kina elimu mpya ambayo kabla haikuwa inajulikana.

Wazanzibari wengi, ukimtoa Dr. Harith Ghassany: ‘’Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru,’’ (2010), walioandika historia ya mapinduzi wote wamepita mle mle katika historia rasmi.

Msomaji hapati jipya isipokuwa tofauti ya jalada, jina la kitabu na la mwandishi.

Unapoanza kumsoma Hashil Seif mwanzoni tu unakuwa mfano wa mtu aliyekuwa kalala usingizi fofofo na ghafla anatokea mtu akammwagia maji baridi usoni na kwa maji yale akashtuka kutoka usingizini na pengine kwenye ndoto akawa karejea katika dunia ya kweli.

Hashil Seif anakifungua kitabu kwa majina ambayo hutayakuta katika historia tuliyoizoea ya mapinduzi ya Zanzibar.

Hashil Seif katika kitabu hiki kataja majina ambayo yalifutika katika historia ya Zanzibar na kama utayakuta basi yatakuwa yemetajwa, ‘’in passing,’’ kama Waingereza wasemavyo, yaani majina hayo yatakuwa yametajwa kijuujuu.

Nitatoa mfano kwa uchache.

Hashil anawataja mara kadhaa katika kitabu Abdulrahman Babu, Khamisi Abdallah Ameir, Ali Sultan Issa na Badawi Qullatein katika siasa za kupigania uhuru wa Zanzibar.

Ahmed Rajab mmoja wa makomredi, ambae kaupitia mswada wa kitabu hiki ameniandikia na kunifahamisha kuwa Khamis Abdallah Ameir kama ‘’Theoretician,’’ sifa hii hutaisoma katika kitabu lakini katika mawasiliano yangu na Ahmed Rajab hili kanieleza na akasema kuwa Khamis Abdallah Ameir hakuwa mwanachama wa kawaida katika harakati zile.

Hili lilidhihirika baada ya mapinduzi kwa Khamis Abdallah Ameir kuwa memba wa Baraza la Kwanza la Mapinduzi.

Khamis Abdallah Ameir sikupatapo kumsikia kabla mpaka nilipomuona hapa katika ukumbi huu katika muhadhara wa Abdallah Kassim Hanga na sasa kaletwa tena na Hashil Seif.

Babu, Ali Sultan na Badawi Qullatein hawahitaji maelezo.

Bahati mbaya sana kuwa kitabu hakikuwekwa faharasha yaani ‘’index,’’ lakini laiti ingekuwapo faharasha msomaji angeweza kuona umihumu wa wazalendo hawa waliotajwa katika kitabu hiki kwa kuangalia ni mara ngapi majina yao yametajwa katika historia hii.

Huu ni mfano mmoja tu katika majina mengi ambayo hayajatajwa katika historia ya Zanzibar lakini Hashil Seif ameyarejesha na kueleza historia za watu hao katika kupigania uhuru wa Zanzibar.

Msomaji atamsoma Ali Sultan Issa aliyekuwa Mkomunisti ndani ya ZNP, Badawi Qulattein, Salim Rashid aliyekuwa katibu wa kwanza wa Baraza la Mapinduzi.

Wazalendo hawa historia zao zina mvuto wa pekee kabla na baada ya mapinduzi.

Ali Sultan ndiye aliyetengezeza mpango mzima wa kuwapeleka vijana wa ZNP, Cuba kwa mafunzo ya kijeshi kujitayarisha kwa mapinduzi.

Haya ndiyo msomaji atakutananayo katika kitabu hiki na ikiwa ni hivi ndivyo hali ilivyokuwa wakati wa kupigania uhuru wa Zanzibar haiwi tabu kuelewa sifa za makomredi katika uongozi na mchango wao katika mapinduzi.

Tunamuomba Allah amsamehe ndugu yetu na amweke mahali pema peponi.

Amin.
Asante Mohamed nimeongeza kitu.
 
Mkuu Maalim Mohamad said , asante sana kwa taarifa hii. RIP Shujaa huyu.

Katika maadhimisho ya miaka 60 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, natamani washiriki wote wa Mapinduzi Matukufu hayo walio hai, waenziwe, na waliotangulia mbele ya haki, watajwe na familia zao zipokee chochote, as just a token of appreciation!.


Tarehe kama ya leo 11/01/1964 miaka 60 iliyopita, ndio Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yalifanyika!. Alfajiri ya Tarehe 12 Januari, 1964 ilikuwa ni kutangazwa tuu!.

Nawatakia maadhimisho mema ya miaka 60 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Paskali
Lkn mapinduzi yalifanyika usiku wa saa tisa alfajiri.

Yalichukua muda mfupi sana lkn athari zake zimedumuna huenda zikadumu kwa miaka mingi
 
Back
Top Bottom