Maoni na Ushauri kwa Joshua Nassari

Maoni na Ushauri kwa Joshua Nassari

Mie najiuliza tu, makosa madogo kama haya,(kama ni kweli) ni uzembe .... sasa unawezaje kufanywa na vijana wanaoitwa wasomi na pengine chama kikishika hatamu wawe viongozi wa juu serikalini, watatufikisha kweli?
Wanakwenda kushika hatamu kama waitara hawana subira wanahama chombo
 
Ni hivi, hakuna haja ya kupoteza muda kutafsiri sheria, Nassari kashachukua pesa ya ccm, na huyo spika anaujua mchezo mzima. Nassari ataishia kuzungumza utoto tu. Eti mke wake kajifungua kwa shida, anajifanya anajua kupenda sana. Pumbavu kabisa
 
Jiwe ,Ndugai wamemwingiza mkenge kwa hasira ya kuwaumbua wakati wa manunuzi ya madiwani .fikra tu lakini .
 
Mkuu unadhani sababu za Nassary zina Mashiko? Kutoka moyoni sema tu.
Si trahisi kujua hali ya mkewe ilikuwa critical namna gani? Sijui kwa nini ofisi ya spika haikumjibu barua yake ya kuomba ruhusa. Machozi ya Nasari yanaweza kuwa na maana ya kina zaidi zaidi kuliko uwezo wa yeyote kati yetu kuimagin.
 
johnthebaptist ,

..Asante kwa kuni-tag.

..hata mimi hoja yako imeendelea kunifikirisha.

..mimi ni mhenga lakini sina kumbukumbu ya mbunge kuvuliwa nafasi yake kama ilivyotokea kwa Nassari.

..pia sina kumbukumbu ya mbunge aliyeadhibiwa bila kupewa nafasi ya kujitetea.

..hata wabunge watukutu kama dada yetu Mh.Mdee siku zote wamekuwa wakipewa nafasi kujitetea.

..inashangaza kwamba adhabu hii ya KIHISTORIA Spika ameitoa bila kufanya consultations ambazo wengi walitarajia. Kwa mfano, kwanini hakumshirikisha KUB, au Chief Whip wa upinzani?

..lingine ni kwamba, Spika Ndugai amekuwa akitibiwa mara kwa mara, tena kwa gharama kubwa kwelikweli. Sasa inastaajabisha anapokuwa very inconsiderate, na wakati mwingine mkatili, wabunge wa upinzani wanapokuwa wagonjwa au wanapouguza.

..rejea suala la TL, au suala la Kubenea kuburutwa ktk kamati ya nidhamu akiwa kwenye wheelchair, na sasa Nassari.
 
Kuna wakati nawashangaa sana wanasiasa. Wamekuwa kama wanamazingaombwe. Wanacheza na hisia za watu
 
Sijaamini utetezi alioutoa Nassari kwasababu kadhihirisha kabisa kua anajua alivunja sheria na ndio maana ni kama anaomba Ndugai atoke kuwa spika afanye kazi za maparoko na wachungaji bila kujua siasa ni kazi ya kaisari na ukizingua unahukumiwa kikaisari. Kwa hili Nassari katudanganya ila hata kama ni kweli alikua busy kushughulkia afya ya mke na mwanae, asishangae siku anagundua mtoto aliemfanya kumwaga chozi mbele ya kamera kumbe ni wa Lema au jirani yake. Life is full of surprises, never take anything for granted
 
Pascal Mayalla ushauri wako juu ya DOGO janja Mh.Nassar ukoje Tafadhali.
Mimi niliisha mshauri kabla, kwa vile Chalii bado ni dogo na bado ana safari ndefu mbele yake, Kama anatakaa kuendelea kuwa na future kwenye the game of politics, then, there is no any other options zaidi ya kuunga mkono juhudi. Ushauri huu niliutoa siku nyingi kabla.

Kiukweli kabisa, DC Jerry Murro, yuko vizuri!, ni visionary leader mwenye vision, mission, uwezo na kipaji. Anastahili kuwa RC, atakuwa kama Mtaka!. - JamiiForums

Na ushauri huu sii kwa Nasari tuu peke yake, lakini ni political landscape yote ya the political game ya nchi yetu, Magufuli is a game changer, amechange game yote, hivyo niliwashauri wapinzani wenye kuona mbali, the choice is one and only, kujiunga CCM

Trend Reading: Wanaohamia CCM wasibezwe! Wanaona mbali, 2020 Majimbo yote kurejeshwa. Je tunarejea nchi ya Chama kimoja? - JamiiForums
P
 
Sijaamini utetezi alioutoa Nassari kwasababu kadhihirisha kabisa kua anajua alivunja sheria na ndio maana ni kama anaomba Ndugai atoke kuwa spika afanye kazi za maparoko na wachungaji bila kujua siasa ni kazi ya kaisari na ukizingua unahukumiwa kikaisari. Kwa hili Nassari katudanganya ila hata kama ni kweli alikua busy kushughulkia afya ya mke na mwanae, asishangae siku anagundua mtoto aliemfanya kumwaga chozi mbele ya kamera kumbe ni wa Lema au jirani yake. Life is full of surprises, never take anything for granted
Ahaaaaaaaaaaaaaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
IMG_20190317_225332.jpg
 
..wewe inawezekana huna mke.

..au kama una mke, haujapitia MTIHANI wa kujaribu kupata mtoto na ikashindikana kwa muda mrefu.

..unazungumzia biashara?!! Kuna watu wanafilisika kwa mtihani wa kupata mtoto.

..mbona Spika alikaa nje ya nchi muda mrefu akijiuguza?
Ka-mtu kenu kajinga tu! Nahisi kalilengesha azaliwe huko kwa matumaini kwamba akikuwa, ataomba awe raia wa US. Hapo ndo utaona kwamba tuna wasio na akili ndani ya Bunge. Analipwa mshahara kwa kazi ya ubunge. Hiyo ndo ajira yake. Ni ajira ya kiapo cha kuwatumikia wananchi. Sasa yeye anakuja na hadithi za kusema eti familia yake ni bora kuliko ajira! Kwa maana nyingine familia yake ni bora kuliko wananchi anaowawakilisha. Soo low!

Ni mmoja wa vijana walsiojitambua kama wewe unayelinganisha Mbunge Ndugai na mke wa Nasari. MKe wa Nasari ni mbunge?
 
Sheria na kanuni za Bunge zipo.Sioni watetezi wa Nasari wakija na reference za kisheria na kanuni zaidi ya kupiga ramli.mukutano mitatu maana yake miezi tisa.Bunge la bajeti hakuhudhuria, lile la November ka sikosei hakuhudhuria na la January hakuhudhuria. Kwamba huyu mbunge alikua na dharula mikutano yote mitatu na hakuweza kupata nafasi hata kidogo kuomba ruhusa?Kwamba baada ya KUKOSA bunge la bajeti ambalo linachukua miezi mitatu hakupata hata muda wa kuja kuclear kuwa alikua na shida?November pia dharula ikaendelea, January kama kawaida. Inawezekanaje?

Kuna kanuni yyt inamtaka speaker amuite mbunge na ajitetee kwanini hajahudhuria mikutano mitatu bira ruhusa?Speaker kataja vifungu, mbona yeye na watetezi wanaongea maneno matupu?Huko mahakaman ataenda kusimamia vifungu vipi ambavyo huku nje ameshindwa kuvitaja kuonesha hajatendewa HAKI?

Mwisho niseme Nasari anawageuza watu Mazombie.

The problem with the world is that the intelligent people are full of doubts, while the stupid ones are full ofconfidence.
 
Sijaamini utetezi alioutoa Nassari kwasababu kadhihirisha kabisa kua anajua alivunja sheria na ndio maana ni kama anaomba Ndugai atoke kuwa spika afanye kazi za maparoko na wachungaji bila kujua siasa ni kazi ya kaisari na ukizingua unahukumiwa kikaisari. Kwa hili Nassari katudanganya ila hata kama ni kweli alikua busy kushughulkia afya ya mke na mwanae, asishangae siku anagundua mtoto aliemfanya kumwaga chozi mbele ya kamera kumbe ni wa Lema au jirani yake. Life is full of surprises, never take anything for granted
Hata wa Jiwe pia huwezi jua
 
Ila kusema ukweli, dogo janja ametokota vibaya sana. Japo siipendi CCM lakini dogo janja ndiye aliyetengeneza mazingira yanayohalalisha yeye kuvuliwa ubunge. Walichokifanya mahasimu wake ni kutumia tu fursa hiyo ya kumvua ubunge kama ilivyojitokeza. Ushauri wangu kwa chadema ni kuwa, kwenye uchaguzi wa marudio wasimamishe mtu mwingine. Kama dongo janja atachukia na kwenda kuunga mkono juhudi za mkuu basi aachwe tu aende maana impact yake ni ndogo sana hata hivyo.
 
Back
Top Bottom