Abdul Nondo
JF-Expert Member
- Oct 28, 2016
- 515
- 2,875
Kwako Mh.Joshua Nassar ,
Pole kaka yangu kwa changamoto zote ambazo umepitia na hongera kwa kupata mtoto Mungu ampe afya njema na amkuze.
Pia pole kwa kuvuliwa ubunge najua namna unavyojisikia vibaya ,inauma sana .
Ila nimesikia mkutano wako wa vyombo vya habari (Press conference), umeongea vizuri sana hasa ulipojishusha na kuomba Mh.Spika arejee maamuzi yake kwa busara kama mlezi.
Mh.Nassar najua sio muda huu wa kukulaumu ila ni muda wa kuambiana kuwa wapi ulijisahau kidogo na wapi uliteleza kidogo ,kwani kupitia kujua ulipoteleza ndio mwanzo wa kufahamu wapi pakutokea na kujifunza kwa wabunge wengine na kuishi kwa tahadhari.
Ni kweli kabisa ,Mh.Spika Ndugai alipaswa atumie busara kama mzazi na mlezi wa Bunge ,ila na wewe pia Mh.Nassari ulipaswa kuwa na tahadhari kwa kuangalia namna ulivyokuwa vocal critics bungeni ,kwa kuangalia aina ya spika na kalba yake,kwa kujiangalia wewe ni mbunge wa chama gani mpinzani au Chama tawala ,kwa kuangalia pia namna upinzani unavyokumbana na changamoto .Hayo yote yangekupa fahmu ya kujua tahadhari ipi ulipaswa kuchukua.
Mkutano wako na vyombo vya habari uliacha maswali kadhaa ambayo hayakujibika hasa ulipokataa maswali ,labda ni kwa sababu zako muhimu.
Mh.Nassar uongozi au kazi ya kuhudumia wananchi haina maana ya kuacha kuhudumia au kuuguza familia hapana hata kidogo,ila kuna taratibu zake za kufuata ,huku wajibu wa msingi wa kuhudumia au kuuguza familia ukabaki nao na usiathiriwe.
Mh.Nassar ,Spika labda na yeye hakutumia busara ila hata na wewe kuna majukumu fulani uliyaruka ,ukasau kuyafanya aidha kwa mawazo ya kuuguza shemeji yetu au kwa kusahau.
1. Mh.Nassar wewe ofisi yako ni Bunge la jamhuri katika taratibu mlezi na bosi wako ni spika wa bunge ,ulipaswa kuandika barua ukaipeleka au ikapelekwa na mtu kwaniaba yako kwa despatch book ,sababu kutokuhudhuria vikao sio jambo dogo ni swala nyeti ,Mh.Lema angekupelekea bungeni kwa despatch au mbunge yeyote unaye muamini hivyo ungekuwa na ushahidi wa kutosha leo.
Ila Mh.Nassar unasema ulimuomba msaidizi wa spika email ya spika ,Mh.Nassar ni kweli email au barua pepe iko kundi moja na registered mail, DHL, EMS n.k. Kwenye zote hizi, proof ya kupokea ni utumaji. Once sent, it's deemed to have been delivered.
Ila hofu yetu ni kuwa vipi kama aliyekupa email ya spika alitoa email ambayo sio active kwa makusudi ? ,vipi kama Mh.Spika aliona email yako ila akasema hajaona kwa makusudi au hajaiona kweli ? ,vipi kama mh.spika akiikana kwa makusudi email uliyotumia kuwa sio yake na akadai aliyekupa amekudanganya ?.
Turudi kwa hoja ya awali kuwa ulipaswa kupeleka au mtu akakupelekea barua ofisi ya spika kwa despatch book leo ungekuwa unatuonesha saini ya kupokea barua sio texts za whaatsp za msaidizi wa spika.
Pia ulisema Bunge la mwanzo wa January mwaka jana na Novemba mwishoni 2018 ,hukuwepo ,huku ukisema uliandika barua January hii ya 2019 ila hujasema huko nyuma ,kama ulitoa taarifa kwa spika au laa .
2.Mh.Nassar wewe ulikuwa unawakilisha wananchi wa Arumeru mashariki waliokuchagua kwenda bungeni ,hivyo wewe ulikuwa Agent kwao na wao kwako ni principal, hivyo wewe ulikuwa unawajibika kwao, sababu bungeni haukuwa unaenda chukua posho ila kuwawakilisha wao ,ulipaswa kutoa taarifa ya kiofisi (Ofisi ya Mbunge ) kwenda kwa wananchi kuwa hautakuwepo bungeni kutokana na changamoto za kuuguza ,hakika matatizo yameumbiwa binadamu ,wananchi wako wangekuelewa na wangekuwa wanakuombea dua na baraka kwa Mungu.
3.Mh.Nassar ,wewe ulipita kupata uwakilishi kupitia Chama chako ,Bungeni kuna ofisi ya Kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani (KUB) ,ofisi ya party whip ambaye kaimu ni Mh.Selasini pia katika chama chako kuna uongozi Katibu au ofisi ya mwenyekiti .Hawa walipaswa kupata barua yako ya kutohudhuria bungeni kutokana na changamoto za afya ya shemeji yetu (Mke wako) na Afya ya shemeji yetu ilikuwa na uzito mkubwa hakuna ambaye angekataa ,ungepata pia baraka za chama chako na viongozi wako ,hata nakala ya barua ambayo ungetuma kwa spika ingetosha tuu kuwatumia na wao.
Leo Kaka yangu Nassar ungekuwa na utetezi kutoka pande zote ,watu wameumia na wanasikitika ila kuna sehemu nyingi uliteleza ukajisahau ndio maana wanashindwa wasimame kutetea namna gani.
Ushauri wangu kwako kaka yangu.
1.kaa pamoja na wanasheria wako uwasilikize kama kuna ushihidi wa kutosha (Evidences ) na (Vithibitisho) exhibits vya msingi ambavyo vitasaidia kama ukifungua kesi kupinga haya maamuzi ,simama imara pinga bila kuvunjika moyo kutafuta haki yako na ya wananchi wako.
2.Ila kama kweli wanasheria wameona hakuna ushahidi na vithibiti vya kutosha ,Nakuomba ujadiliane na viongozi wako kwenda kuongea na ofisi ya spika ,busara yake itumike hapa kama mzazi na mlezi wa wabunge wote .
Aguswe na afya ya shemeji yetu ,aguswe na changamoto ulizopitia na ukiri kuwa kweli ulikosea kutokana na changamoto za kuuguza shemeji yetu (Mke wako ) ,na usiache pia kumuomba Mungu akuvushe katika kipindi hiki kigumu hakika Mungu atakujalia ,na hakika Mungu atampa busara zaidi Mh.Spika katika kuangalia maamuzi yake upya .
Pole sana kaka yangu,Mungu ampe afya njema mdogo wetu na mama huko nyumbani ,awape uvumilivu wa kutosha katika kipindi hiki kigumu.
Abdul Nondo.
abdulnondo10@gmail.come
Sent using Jamii Forums mobile app
Pole kaka yangu kwa changamoto zote ambazo umepitia na hongera kwa kupata mtoto Mungu ampe afya njema na amkuze.
Pia pole kwa kuvuliwa ubunge najua namna unavyojisikia vibaya ,inauma sana .
Ila nimesikia mkutano wako wa vyombo vya habari (Press conference), umeongea vizuri sana hasa ulipojishusha na kuomba Mh.Spika arejee maamuzi yake kwa busara kama mlezi.
Mh.Nassar najua sio muda huu wa kukulaumu ila ni muda wa kuambiana kuwa wapi ulijisahau kidogo na wapi uliteleza kidogo ,kwani kupitia kujua ulipoteleza ndio mwanzo wa kufahamu wapi pakutokea na kujifunza kwa wabunge wengine na kuishi kwa tahadhari.
Ni kweli kabisa ,Mh.Spika Ndugai alipaswa atumie busara kama mzazi na mlezi wa Bunge ,ila na wewe pia Mh.Nassari ulipaswa kuwa na tahadhari kwa kuangalia namna ulivyokuwa vocal critics bungeni ,kwa kuangalia aina ya spika na kalba yake,kwa kujiangalia wewe ni mbunge wa chama gani mpinzani au Chama tawala ,kwa kuangalia pia namna upinzani unavyokumbana na changamoto .Hayo yote yangekupa fahmu ya kujua tahadhari ipi ulipaswa kuchukua.
Mkutano wako na vyombo vya habari uliacha maswali kadhaa ambayo hayakujibika hasa ulipokataa maswali ,labda ni kwa sababu zako muhimu.
Mh.Nassar uongozi au kazi ya kuhudumia wananchi haina maana ya kuacha kuhudumia au kuuguza familia hapana hata kidogo,ila kuna taratibu zake za kufuata ,huku wajibu wa msingi wa kuhudumia au kuuguza familia ukabaki nao na usiathiriwe.
Mh.Nassar ,Spika labda na yeye hakutumia busara ila hata na wewe kuna majukumu fulani uliyaruka ,ukasau kuyafanya aidha kwa mawazo ya kuuguza shemeji yetu au kwa kusahau.
1. Mh.Nassar wewe ofisi yako ni Bunge la jamhuri katika taratibu mlezi na bosi wako ni spika wa bunge ,ulipaswa kuandika barua ukaipeleka au ikapelekwa na mtu kwaniaba yako kwa despatch book ,sababu kutokuhudhuria vikao sio jambo dogo ni swala nyeti ,Mh.Lema angekupelekea bungeni kwa despatch au mbunge yeyote unaye muamini hivyo ungekuwa na ushahidi wa kutosha leo.
Ila Mh.Nassar unasema ulimuomba msaidizi wa spika email ya spika ,Mh.Nassar ni kweli email au barua pepe iko kundi moja na registered mail, DHL, EMS n.k. Kwenye zote hizi, proof ya kupokea ni utumaji. Once sent, it's deemed to have been delivered.
Ila hofu yetu ni kuwa vipi kama aliyekupa email ya spika alitoa email ambayo sio active kwa makusudi ? ,vipi kama Mh.Spika aliona email yako ila akasema hajaona kwa makusudi au hajaiona kweli ? ,vipi kama mh.spika akiikana kwa makusudi email uliyotumia kuwa sio yake na akadai aliyekupa amekudanganya ?.
Turudi kwa hoja ya awali kuwa ulipaswa kupeleka au mtu akakupelekea barua ofisi ya spika kwa despatch book leo ungekuwa unatuonesha saini ya kupokea barua sio texts za whaatsp za msaidizi wa spika.
Pia ulisema Bunge la mwanzo wa January mwaka jana na Novemba mwishoni 2018 ,hukuwepo ,huku ukisema uliandika barua January hii ya 2019 ila hujasema huko nyuma ,kama ulitoa taarifa kwa spika au laa .
2.Mh.Nassar wewe ulikuwa unawakilisha wananchi wa Arumeru mashariki waliokuchagua kwenda bungeni ,hivyo wewe ulikuwa Agent kwao na wao kwako ni principal, hivyo wewe ulikuwa unawajibika kwao, sababu bungeni haukuwa unaenda chukua posho ila kuwawakilisha wao ,ulipaswa kutoa taarifa ya kiofisi (Ofisi ya Mbunge ) kwenda kwa wananchi kuwa hautakuwepo bungeni kutokana na changamoto za kuuguza ,hakika matatizo yameumbiwa binadamu ,wananchi wako wangekuelewa na wangekuwa wanakuombea dua na baraka kwa Mungu.
3.Mh.Nassar ,wewe ulipita kupata uwakilishi kupitia Chama chako ,Bungeni kuna ofisi ya Kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani (KUB) ,ofisi ya party whip ambaye kaimu ni Mh.Selasini pia katika chama chako kuna uongozi Katibu au ofisi ya mwenyekiti .Hawa walipaswa kupata barua yako ya kutohudhuria bungeni kutokana na changamoto za afya ya shemeji yetu (Mke wako) na Afya ya shemeji yetu ilikuwa na uzito mkubwa hakuna ambaye angekataa ,ungepata pia baraka za chama chako na viongozi wako ,hata nakala ya barua ambayo ungetuma kwa spika ingetosha tuu kuwatumia na wao.
Leo Kaka yangu Nassar ungekuwa na utetezi kutoka pande zote ,watu wameumia na wanasikitika ila kuna sehemu nyingi uliteleza ukajisahau ndio maana wanashindwa wasimame kutetea namna gani.
Ushauri wangu kwako kaka yangu.
1.kaa pamoja na wanasheria wako uwasilikize kama kuna ushihidi wa kutosha (Evidences ) na (Vithibitisho) exhibits vya msingi ambavyo vitasaidia kama ukifungua kesi kupinga haya maamuzi ,simama imara pinga bila kuvunjika moyo kutafuta haki yako na ya wananchi wako.
2.Ila kama kweli wanasheria wameona hakuna ushahidi na vithibiti vya kutosha ,Nakuomba ujadiliane na viongozi wako kwenda kuongea na ofisi ya spika ,busara yake itumike hapa kama mzazi na mlezi wa wabunge wote .
Aguswe na afya ya shemeji yetu ,aguswe na changamoto ulizopitia na ukiri kuwa kweli ulikosea kutokana na changamoto za kuuguza shemeji yetu (Mke wako ) ,na usiache pia kumuomba Mungu akuvushe katika kipindi hiki kigumu hakika Mungu atakujalia ,na hakika Mungu atampa busara zaidi Mh.Spika katika kuangalia maamuzi yake upya .
Pole sana kaka yangu,Mungu ampe afya njema mdogo wetu na mama huko nyumbani ,awape uvumilivu wa kutosha katika kipindi hiki kigumu.
Abdul Nondo.
abdulnondo10@gmail.come
Sent using Jamii Forums mobile app
Wasalaam!! Kwa mara ya kwanza naomba nimpongeze Spika Ndugui na uongozi wote wa bunge kwa hatui hii waliyochukua. Baada ya kumsikiliza Nassari na sababu zake za kitoto za kutokuhudhuria vikao vitatu mfululizo nimemdharau sana. Sisi ni watanzania na wengi tumeajiriwa au tumejiajiri.
Ni boss gani atakayekuvumilia zaidi ya miezi mitatu eti mwanaume unasubiri mkeo ajifungue? Huwezi angalau kwenda kwazini hata siku mbili kwa mwezi kisa unasubiri mkeo ajifungue? Nassari ni daktari?
Nassari alishindwa nini hata kumtuma mama mkwe wake kumuangalizia mkewe wakati akiwa kalazwa ili angalau atimize sehemu ya majukumu yake? (Kwatamaduni zetu za kiafrica inakubaliwa). Hata Magufuli mama yake yuko ICU lakini anafanya kazi. Watanzania tuache kulea ujinga kama wa huyu anayejiita dogo janja.
Nassari angekuwa mfanyabiashara angekaa hosipitali miezi zaidi ya mitatu kisa mke anasubiri kujifungua mtoto? Ungekuta hizo biashara? Mbona tunajipa majukumu ambayo sio yakwetu? Spika Ndugai nakupa Kongole uko sahihi. Watanzania tuache kuendekeza upuuzi kisa mazoea ya kujiona sisi tu na kwasababu tuna machozi basi tuishi kwa mazoea. Nasema Noooooo!!!!
Juzi walikutana msibani na Mh. DC na Mzee Sarakikya bila aibu akatamka yuko nje kuwatafutia wananchi wake misaada. Sasa leo hizo sababu kazitoa wapi? Naomba afuatilie suala la Makonda na makontena yake. Na pia sio kazi yake kuomba misaada ya hii nchi kwa wahisani. Yeye anatakiwa kuiambia serikali matatizo ya wananchi wake serikali itekeleze na sio kuzurura na kupiga picha nje kwa matanuo yake.
Naomba hili liwe fundisho kwa wawakilishi ngazi zote.
Na sisi watanzania tuache kuwaonea huruma wapinzani kwa baadhi ya mambo yao ya kipuuzi ambayo yatatutia aibu. Kama wapinzania wanapigania sheria na wawe tayari kuhakikisha hata wao na wafuasi wao wanafuata sheria na taratibu nyingine za nchi ambazo zimetungwa kwa mujibu wa sheria na katiba yetu.
Asanteni Nawasilisha
Sheria na kanuni za Bunge zipo.Sioni watetezi wa Nasari wakija na reference za kisheria na kanuni zaidi ya kupiga ramli.mukutano mitatu maana yake miezi tisa.Bunge la bajeti hakuhudhuria, lile la November ka sikosei hakuhudhuria na la January hakuhudhuria. Kwamba huyu mbunge alikua na dharula mikutano yote mitatu na hakuweza kupata nafasi hata kidogo kuomba ruhusa?Kwamba baada ya KUKOSA bunge la bajeti ambalo linachukua miezi mitatu hakupata hata muda wa kuja kuclear kuwa alikua na shida?November pia dharula ikaendelea, January kama kawaida. Inawezekanaje?
Kuna kanuni yyt inamtaka speaker amuite mbunge na ajitetee kwanini hajahudhuria mikutano mitatu bira ruhusa?Speaker kataja vifungu, mbona yeye na watetezi wanaongea maneno matupu?Huko mahakaman ataenda kusimamia vifungu vipi ambavyo huku nje ameshindwa kuvitaja kuonesha hajatendewa HAKI?
Mwisho niseme Nasari anawageuza watu Mazombie.
The problem with the world is that the intelligent people are full of doubts, while the stupid ones are full ofconfidence.
Nianze kwa kusema kua,nimekua nikimfuatilia sana na kwa ukaribu Joshua Nasari,akiwa bungeni na Jimboni. Joshua anajua kujenga hoja,anajua kuipangilia hoja yake na akaeleweka na wenye akili. Kwale wakuunga mkono kila kitu huwa inakua ngumu kidogo kumuelewa Nasari.
Jimboni kwake nimepita mara nyingi,huwezi kumsema vibaya ukaeleweka. Anasifika kwa uchapakazi wake,na kuhudumia wananchi wake,na alikua kiongozi anayeongoza na kufuatwa na anaowaongoza siyo kwakua walimuogopa,hapa,kwakua tu walimkubali na kumuamini.
Nasari alikosea hapa,1.kulewa sifa,akadhani tupo kwenye zama zile.,2.kujisahau,na hili ni tatizo la wabunge karibu wote,wanakujaga kugutuka yakiwakuta kama hili la Nasari au kuanza kukataliwa majimboni kabla hata ya uchaguzi.
Mfano mzuri ni mkuu mmoja wa mkoa sasahivi,alienda msibani mwaka 2015,alikua hajawahi kufika eneo hilo tangu uchaguzi wa 2010,alichoambiwa na wafiwa ni"ondoka tuzike,maiti imegoma kutoka ndani mpaka uondoke",aliondoka kwa aibu mno.
3.Nasari alijawa na kiburi na dharau. Kwa mtu yoyote aliyeajiriwa,ukiomba ruhusa huondoki eneo la kazi bila kuhakikisha umeruhusiwa,vinginevyo utakua umejiruhusu.
Eneo lingine aililokosea Nasari,ni kudhani kuna huruma kwenye sheria,Ndugai anaweza kuwa na huruma,ila siyo sheria anazozisimamia. Nimesoma posts nyingi na comments nyingi humu JF,wengi wanamtukana Ndugai na kusahau kuwa siyo yeye,ni sheria.
Wanasema za mwizi ni 40,jitahidi kuhesabu,zikifika 38 tulia kidogo,kwamaana Nasari alipaswa kuwa anaenda bungeni japo mara mojamoja.
Alipokosea tena ni kubase tatizo lake na tatizo la mkewe,alokua anajifungua na mke,siyo yeye,ana dada zake,ana mama yake,mke ana ndugu zake wa kike,walitosha sana kuwa watu wa karibu mke wake,yeye alitakiwa awe kuhenya kutafuta nguo za mtoto na chakula cha mzazi. Sawa,ndoa inakiapo chake,sikatai,ila sometimes hawa tunaoapa nao ndo wasaliti wakubwa wa viapo hivyo,mwanaume uchague sahihi.
Lingine ni kulia mbele za kamera. Mwanaume halii hata sikumoja chozi likaonekana,labda msibani,nako kuna watu wa kukuambia"vumilia,jikaze,wewe ni mwanaume". Huambiwi haya kwa bahati mbaya,ni kukumbusha kuwa,uwe na ngozi ngumu. Unaanguka,unasimama tena.
Mwisho,sioni logic ya yeye kwenda mahakamani. Kufanya nini?,kumshtaki nani?,ili iweje?,katiba inasemaje?,ana barua ipi iliyomruhusu kutokuhudhuria vikao?,anataka kumfurahisha nani kuwa ameenda kuitafuta haki ila imeshindikana?
Yote haya,jibu lake ni kujisumbua,bunge ni muhimili mwingine,mahakama na serikali ni muhimili mwingine.
Pia,asome tu alama za nyakati.
WAASALAM.