Manji: Nchi yangu hainithamini

yy aache ujanjaujanja afuate taratibu na kanuni, aache ku lobby na kununua maeneo ya wazi kwa kutumia udhaifu wa maafisa ardhi na manispaa. Akifanya hivyo hawezi kuwa na malalamiko . Hapo kazi tuu

 
Japo sikufahamu nakupa hongera kwa kusimama kidete kuupinga uovu mkubwa saana "UBAGUZI" unaopigwa vita ulimwenguni, katika biashara, makazini, michezo NK. Hatukatai kuna ubaguzi lakini hauna kabila, rangi,dini au jinsia hilo ni suala la mtu binafsi maana lipo katika kila kabila na ni lazima tulipige vita.

Suala la Ndugu Manji ni mtanzania tutake tusitake, kama walivyo watanzania wengi nchi za nje waliochukua uraia wa nchi tofauti wanaitwa wamarekani, waingereza, wajerumani nk. Wengi ni wafanyabiashara, wafanyakazi, na hata wapo wezi na wavuta unga lakini haifuti wao kuitwa kuwa ni wamarekani, wajerumani au waingereza kwa matendo yao.
 
Last edited by a moderator:
Idd Amin Dada anahusika na maamuzi yake kwa kina Manji wote naona JPM yupo njiani kuelekea kwa IAD
 
Haya ndio matatizo ya google bila kutumia weledi, Nyerere mnamchukia waislamu wafuasi wa Mohamed Saidi kwa chuki zenu za kidini tu hamna lolote na wala hamjui kitu.

Nyerere aliongoza serikali iliyowapa fursa wahindi na hata mzungu alikuwa kwenye baraza lake la mawaziri na hata yule mama muingereza aliendelea kuwa PS wa Nyerere mpaka anakufa.

Ninachokifahamu mimi TRA imeundwa na Benjamini Mkapa sasa kama kabla ya hapo palikuwa na TRA hilo ni jipya, ningeomba utupe ushahidi ni wapi na katika sheria ipi waarabu na wahindi wanazuiwa kisheria na kikatiba kujiunga na majeshi yetu?

Hatuna tofauti yoyote na Kenya, Kinana ni msomali na amepewa madaraka makubwa tu mpaka leo ndio katibu mkuu wa ccm,sioni logic wala point yako katika hili, waangalie kina Bashe, Rage wote ni wasomali angalia bunge letu lina wabunge hadi masingasinga tumekosa mbilikimo tu lakini hadi maalbino wamo pia hadi kwenye cabinet, so what is ur point?
 


Kwa hyo kenya wanatuzidi nini kwa huo mchanganyiko unaousema wewe.... Tukiondoa Dar es salaam na Nairobi nitajie mikoa mingine ya kenya inayoweza kupambana na Mwanza, arusha, tanga, mbeya au hata dodoma..... ukweli unaujua mwenyewe....

Mbona china sio rainbow state lakin inakimbiza vibaya mpaka kutishia hata uchumi wa huyo mmarekani.... Penye ukweli tuwe wakweli tuache kuongea vitu kinadharia zaid ya uhalisia wenyewe....

Hivi sisi watanzania tukisema tuishi maisha wanayoishi hawa wenzetu wahindi nchi itakarika au huo umoja wa kitaifa utakuwepo... Hawa wenzetu hatujawahi kuwatenga hata siku moja ila wao naturally ni watu wa kujitenga ndi maana hata zamani walikuwa na maeneo yao yanaitwa uzunguni.....

Unasema eti ni policy kutokuwaajiri wahindi.. Hivi unafaham maana ya policy kweli??? yaani sera????.. Tanzania hakuna sera yoyote iliyoidhinishwa na bunge kutokuwaajiri hawa wenzetu. ila kinachowasumbua wenzetu ni roho za kibaguzi... Hivi unadhani muhindi anaweza kwenda kufanya kazi ofisi ya kata huko kibaigwa ndani kushughulikia migogoro ya ndoa ya mgogo na mmasai???
Wanatuida GOLO kawailize maana yake ni nini... Maana yake ni nyani weusi.... Uliza wanaouza maduka ya wahindi ndio utajua kuwa hawa wenzetu tuko nao kimwili ila kiroho wapo india...
 

Policy ya africanazation ilikuwepo na haijafutwa usiwe mbishi.
Kuhusu wahindi mawaziri hao wana historia yao ya familia zao kujitolea kifedha kuchangia uhuru....walipo ondoka ndio tukafunga kitabu.
Kuhusu uwepo wao bungeni ni ukweli uso pingika utajiri wao ndio unawapeleka huko. Bila ya fedha zao na kujitolea sana wasinge iona dodoma.
Wengine ni kutoka znz sio watanganyika ambako issue hii ndo tatizo.

Kinana alitaka kugombea urais akaambiwa ikaanza kampeni kubwa kuwa huyu msomali...juu ya kutumikia jeshino walimchafua
Kuwapo ccm sasa sio kama watu wanaridhia hawapendi ila ni kikwete ndo aloona atawasaidia.
TRA ni jina tu ..kinachokusudiwa ni mamlaka ya kodi ..walio kua wahini wengi.
Alokua mkuu wa trafic hata aliehusika na kutoa leseni za driving...uzuri hakukuwa na leseni feki mitaani.
Hao kina rage huwa hawaachi kujichanganya lkn hawachi kupigwa vita... waliongoza FAT bila msaada na tulipta vikombe angalau vya east afrika na simba kufika fainali caf lkn wapi damu ya kunguni...
Hao kina bashe nao ni hayo hayo watajipendekeza lkn si hasha utasikia huyo kwanza msomali sio raia...
Kuhusu policy ya ajira...hio ya ubaguzi ilikuwepo na haikufutwa hivyo bado ndo elekezi. Policy hii ya africanasation ilikua na lengo la kuwapa waafrika nafasi za kazi zote za serikali kwa kuwaondoa wasio wafrika makazini...
Kuhusu huyo mzungu wa ikulu siri ya kuwapo kwake anaijua alie muajiri kwani hakua mtanzamia.
 

Acha kupotosha watu pimbi wewe. Unajua historia ya Tanzania!? Au wewe ndio mmoja wa hao wenye passport mbili mbili.
Wala huelewi hapa mada ni nini unarukia tu Angalia usikukwame.
 
Acha kupotosha watu pimbi wewe. Unajua historia ya Tanzania!? Au wewe ndio mmoja wa hao wenye passport mbili mbili.
Wala huelewi hapa mada ni nini unarukia tu Angalia usikukwame.

Hebu tupe darsa kidogo ya historia ya tanzania...
Tufahamishe wahindi na waraabu walikua vp kabla ya uhuru...
Tunasubiri ya maalim
 
La kuvunda halina ubani, ukiona mtu anamsifu hadi Rage basi hapo kuna tatizo hujui hata Historia ya mpira ni nani waliovuruga soka la Bongo, Ndolanga na Rage kwenye serious walikuwa ni watu wa kupigwa risasi hadharani na tapeli aliyekuwa anawafuga kwa kuwapa kiburi ni Sepp Blatter na kuwadi wake wa ukanda huu Asheflod Mamelodi wa Botswana.
 

Ball ni vikombe..bila ya vikombe muulize morinyo
 
Hebu tupe darsa kidogo ya historia ya tanzania...
Tufahamishe wahindi na waraabu walikua vp kabla ya uhuru...
Tunasubiri ya maalim
Ukitaka Historia uliza Historia ya Tanganyika au Zanzibar, Tanzania haina Historia zaidi ya usanii na magumashi tu.
 
Sasa ili usionekane mjinga, fanya utafiti kwenye vyombo vyetu vyote vya ulinzi na usalama kuna muhindi hata mmoja? au unadhani India hawana jeshi kwamba wahindi wa hapa hawawezi kutumikia jeshi? Idd Amin he was perfect.

Labda turudi 1900 mpaka sasa tuangalie uzalendo kwa vitendo ( sio kwa rangi)
Maendeleo yalofanywa na waafrika na wahindi..maendeleo yalogusa kila mtu....haya yakiwa secta ya
Elimu
Afya
Michezo
Kilimo
Makaazi
Ulipaji kodi zaidi
Misaada ya kibinadamu
Usafi wa miji

Tujadili haya kwa kujipima ...then ndo tuwanyoshee vidole...Ujiangalie umeifanyia nn tanzania sio kuchochea ubaguzi.
Kuanzia naanza na Muhimbili hospital imejengwa mhindi ..endelea upande wa pili
 

uraia hakuupora alikidhi vigezo na kuhusu kodi si kunaamlakabzilimchukulia hatua gani?
 
Anatudanganya kwenye tangazo eti ni Kama moyo wake upo hapa wakati upo India.
 
Allen Kilewella njoo ujibu hili Swali ....Jamal alizikwa wapi!?
Tofauti kati ya mazishi ya watu siyo kigezo cha utaifa wao. Daudi Balali ni mtu wa huku Iringa sehemu moja inaitwa Malangali, lakini kazikwa Marekani. Kuna mahujaji hufia Makkah na huzikwa huko huko Makkha. Mazishi ya mtu kufanyika mahala inategemea na mapenzi ya mtu. Nenda Arusha kuna watu lukuki ambao kwa asili ni "watanzania" lakini wamezikiwa Nairobi kenya.

Kuna watu wana imani kwamba wakifa wasisafirishwe kwenda kuzikiwa kwingine, hao nao wasafirishwe kuja kuzikiwa Tanzania kwa hofu kwamba wakizikiwa huko wataonekana kuwa si watanzania!! Kuna watu hapo hapo Dar huzikiwa Makaburi ya Kisutu na wengine hata iweje ni lazima wazikiwe Makaburi ya Kinondoni.Mahali anapozikwa mtu inategemeana na utashi wake au wa familia yake baada ya kifo kutokea na wala haihusiani na utaifa wa mtu. Kuna watanzania wengi tu wamezikwa nchi za nje ingawa uwezo wa kuleta maiti zao ulikuwepo!!


Matola mimi hoja yangu ni kwamba hamuwezi kuundoa utanzania wa Manji eti kwa sababu tu ni mhindi au kama mnavyosema ni fisadi. Kuna makabila hapa tanzania wanapiga sana wake zao, wengine wanauana sana, lakini huwezi sema kwamba si watanzania kwa kuwa tu wana tabia hizo. Manji ahukumiwe kwa makosa yake lakini asishutumiwe kutokana na asili yake!!
 
Si uliwadhulumu waislam viwanja wewe
Na hio coco pia dhulumu si una hela wewe?
Lolote waweza kufanya c ndio? Haya Kyle ulimfunga ponda
Na viwanja ukadhulumu sasa mfunge mzee makomeo uibe a coco beach
Usojijua mja wa laana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…