Manji anakwepa hukumu ya EPA?

pole yake coz ni binadamu mwezetu lakini sipendi kabisa mambo yake,japanis income support na madudu mengine mengi tu aliyoyafanya hayanifuraishi kabisa.
Aliwahi ku gombea ubunge ki gamboni sasa sijui kama tejanga angeweza kuwkilisha wana kigambonino,rafiki yake manyuzi sijui naye tejanga?maana waswahili wa pemba wajuana kwa vilemba.
 
Pia huyu jamaa ni mfisadi lakini Watanzania sijui tumeumbwa vipi hivyo viji centi anavyotoa yanga vinatufanya tumuone kama Mungu vile na kusahau kuwa ni sawa na vibaka wanao iba cheni au simu na kuchomwa moto na raia wenye hasira kali.
 
Wakati naweka hii habari hapa, watu waliibeza, nadhani JF tujifunze uvumilivu. Na tujue kuwa humu JF kuna watu wa kila aina na mara nyingi JF imekuwa ya kwanza

Mkuu nimekukubali, endelea kutuhabarisha

Ushi wa Rombo
 
Niliambiwa kwamba amekwenda South Africa kwa matibabu, lakini katika system za Mwalimu Nyerere International Aiport, jina la Yusuf Mehboob Manji, aliyezaliwa Oktoba 14, 1975, mwenye pasi namba AB 052416 ya Tanzania, halijaonekana, labda kama kasafiri kwa ndege ya kukodi na pasi yake ya Marekani ama kimoja wapo. Patamu hapo.
i stand to be corrected,ina maana birthday yake ndo tarehe aliyofariki Mwalimu?
 
Pia huyu jamaa ni mfisadi lakini Watanzania sijui tumeumbwa vipi hivyo viji centi anavyotoa yanga vinatufanya tumuone kama Mungu vile na kusahau kuwa ni sawa na vibaka wanao iba cheni au simu na kuchomwa moto na raia wenye hasira kali.

Mkuu fikiria angekuwa anaifadhiri SIMBA ungesema hivyo?
Kunya anye KUKU akinya BATA kahalisha.
 
Mkuu fikiria angekuwa anaifadhiri SIMBA ungesema hivyo?
Kunya anye KUKU akinya BATA kahalisha.
Mkuu Fidel80,

Kwanza nirudie kuwapo mkono wa pongezi wana Yanga kwa ushindi wenu 'finyu' dhidi yetu.

Mimi ni shabiki mkubwa wa Simba (kama spika Sitta :) ) lakini naomba kuna mambo wakuu tukubaliane kuwa si ya kukumbatia.

Ufadhili wa Manji kwa Yanga usiwazibe macho mkasahau kuwa jamaa huyu anaitumia Yanga kujitangaza! Jamaa huyu habari nyingi ninazopata juu yake huwa haziridhishi, mara anajidunga madawa, mara anachapisha note fake, n.k. Kwakuwa zinakuwa zinakosa proof japo ni fununu toka kwa watanzania wengi nachelea kuzithibitisha.

Kikwetu wanasema "lisemwalo lipo... kama halipo linakuja".

Nitaingia mtaani kusaka data zaidi nikizinyaka nitawapa facts zaidi na zaidi juu ya mfadhili wenu huyu.
 
Mungu ni Mwenye-enzi,
Anajua mawazo, maneno na matendo yetu.
Anajua kulala kwetu na kuamka kwetu.
Anajua mabaya na mema yote tuyatendayo.
Mungu ni Mwenye-enzi.
 
Kwa dhambi wanazotufanyia na uovu wanaotutenda, wataangamizwa kwa jiwe la kombeo kama Goliati pasipo kujali wala kuogopa nguvu za giza walizonazo. Mungu ibariki Tanzania.
 
Labda ndo staili yake ya kukwepa Rungu la JK kwa mafisadi wa EPA. Au Rungu la EPA ndo limemchanganya hadi akabwia dozi kubwa ya ungwa.
HASWA nimetonywa ilikuwa mtu wa mwanzo kuwekwa korokoroni.nimetonywa kisha paa majuu
 
HASWA nimetonywa ilikuwa mtu wa mwanzo kuwekwa korokoroni.nimetonywa kisha paa majuu

Hajaruka na leo alikuwa ICU, lakini watu wana wasiwasi kwamba inaweza kuwa janja yake ya kukwepa mkono wa sheria na ndio maana sasa inawashangaza watu ilikuwaje watu wake wawe wa kwanza kuwaita waandishi waone bosi wao akichanganyikiwa!!! Nakwambia Watanzania tumezugwa na tutazugwa sana.
 
Mkuu fikiria angekuwa anaifadhiri SIMBA ungesema hivyo?
Kunya anye KUKU akinya BATA kahalisha.

Mkuu Fidel80,

Kwanza nirudie kuwapo mkono wa pongezi wana Yanga kwa ushindi wenu 'finyu' dhidi yetu.

Mimi ni shabiki mkubwa wa Simba (kama spika Sitta :) ) lakini naomba kuna mambo wakuu tukubaliane kuwa si ya kukumbatia.

Ufadhili wa Manji kwa Yanga usiwazibe macho mkasahau kuwa jamaa huyu anaitumia Yanga kujitangaza! Jamaa huyu habari nyingi ninazopata juu yake huwa haziridhishi, mara anajidunga madawa, mara anachapisha note fake, n.k. Kwakuwa zinakuwa zinakosa proof japo ni fununu toka kwa watanzania wengi nachelea kuzithibitisha.

Kikwetu wanasema "lisemwalo lipo... kama halipo linakuja".

Nitaingia mtaani kusaka data zaidi nikizinyaka nitawapa facts zaidi na zaidi juu ya mfadhili wenu huyu.

Mod, nadhani kwa kauli ya Fidel80 unaweza kujua jinsi sisi Watanzania tulivyo watu wa ajabu. Kitu muhimu kwetu ni kupata pesa tu. Hebu angalia kauli
hizi:-
Mh. Membe juu ya kauli yake kuwa Tupokee pesa/Misaada tu hata kama ni ya Shetani! Yaani what ever comes kuhusu IOC mradi tupate pesa na misaada tu! Changanya na kauli ya Fidel80 kwamba kwa kuwa Yanga wanafaidika na pesa chafu za Manji basi ni sawa tu mradi Yanga wanapata pesa! Ukija wakati wa Uchaguzi WaTz tunawachagua tu, mradi wametupa pesa zao zinazonuka na mwisho wa siku tunaona kuwa walichotupa ni senti tano katika bilioni walizotuibia!

Tujipe moyo, tutafika tu, si mbali!
 
Hapa nashindwa kuamini, bila shaka huku kuchanganyikiwa kuna harufu ya EPA! Kama ni madawa angechanganyikiwa siku nyingi,iweje zibaki siku 3 tu kurudisha pesa za EPA ndio achanganyikiwe?Watanzania wa sasa si wavivu kufikiri kama wao wafikirilivyo.
 
Hapa nashindwa kuamini, bila shaka huku kuchanganyikiwa kuna harufu ya EPA! Kama ni madawa angechanganyikiwa siku nyingi,iweje zibaki siku 3 tu kurudisha pesa za EPA ndio achanganyikiwe?Watanzania wa sasa si wavivu kufikiri kama wao wafikirilivyo.


All goes round Comes round. Staili ya kuugua na kwenda ulaya kutibiwa imepitwa na wakati. JK Watanzania wanasubiri masaa haya yaliyobakia tuone utafanya nini,,, kama janja ya nyani tutaona,,,,remember 2010 is just around the corner!
 
Hivi Watanzania tutaendelea kuzugwa hadi lini? Sasa wanasema amepelekwa Nairobi kwa matibabu.... Ama kweli na sasa huku nyuma yule aliyekuwa anamtuma kulipa fedha za Kagoda naye anahaha kulipa fedha, na hivi tunavyozungumza amepeleka mabilioni.......

Date::10/29/2008
Manji wa Yanga sasa alazwa chumba uangalizi maalum hospitalini
Na Mwandishi Wetu

HALI ya mfadhili Mkuu wa Yanga, Yusuf Manji bado haijaimarika na sasa amepelekwa chumba cha wagonjwa mahututi, ICU, katika Hospitali ya Aga Khan jijini Dar es Salaam.

Habari ambazo Mwananchi imezipata jana jioni kutoka hospitalini hapo, zinasema kuwa hali yake ilibadilika ghafla jana mchana na uamuzi uliofikiwa na madaktari ni kumpeleka katika chumba cha uangalizi maalum.

“Manji hajarejea katika hali ya kawaida, amekuwa akizungumza maneno yasiyoeleweka, lakini inawezekana ni malaria kali iliyopanda kichwani…bado hali haijatengemaa, wasiwasi umekuwa mkubwa lakini tunaimani atapata nafuu,” kilisema chanzo cha habari.

Mwananchi iliwasiliana na Mwenyekiti wa Yanga, Iman Madega kutaka kufahamu hali ilivyo kwa mfadhili huyo, na kusema hali yake bado haijaimarika. Hata hivyo Madega hakutaka kuzungumza zaidi suala hilo.

“Nimepata taarifa kuwa hali yake bado haijatengemaa, nilikwenda hospitali lakini sikuweza kumuona na nilizungumza na msaidizi wake, Sabas Kiwango mambo ya Yanga na baadaye nikaondoka hospitali…kwa kweli siwezi kulisemea zaidi, lakini hali ndiyo hiyo,” alisema Madega.

Habari zaidi kutoka hospitalini hapo zinasema kuwa hakuna mtu yeyote anayeruhusiwa kumwangalia Manji isipokuwa watu wa karibu tu na tayari yuko katika chumba hicho cha wagonjwa mahututi.

Manji alipatwa na kilichoelezwa kuwa ni malaria kali siku moja baada ya timu yake kuichapa Simba bao 1-0, katika mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom, mchezo uliofanyika kwenye Uwanja Mkuu wa Tanzania. Baada ya kuugua na kuanguka ghafla, alikimbizwa Hospitali ya Aga Khan kwa matibabu.

Ilielezwa kuwa Manji alipatwa maradhi hayo juzi wakati akijitayarisha kwenda kazini majira ya saa tatu asubuhi lakini ghafla alianguka. “Unajua inawezekana ni furaha za ushindi na kuwa bize inawezekana kulimfanya apatwe na hali hiyo…inawezekana alikuwa na malaria ya muda mrefu na kutokana na kuwa bize na mchezo ndipo ikaibuka.

"Baada ya kufanyiwa vipimo Aga Khan aligundulika kuwa na malaria kali na uchovu, mwili ulikuwa umechoka kwa mawazo akapewa dawa na kumpumzika nyumbani, lakini baadaye majira ya saa 11 alfajiri akatoka nyumbani bila ya kueleweka akielekea maeneo ya Viwanja vya Gymkhana, lakini walinzi wake walimfuata na kumrudisha tena hospitali," alisema Madega alipozungumza na gazeti hili juzi.

Madega alisema hali ya mfadhili huyo ilikuwa inaendelea vizuri baada ya kuchomwa sindano ya kumtuliza lakini baadaye hali yake ilibadilika ghafla.

Juzi Madega aliwataka Wanayanga kutulia katika kipindi hiki ambacho mfadhili wao anasumbuliwa na maradhi na kumuombea aendelee vema na matibabu.

SOURCE:
Mwananchi Read News
 
Hi ya kulazwa ICU nimeiona. lakini does this make us believe that he is that serious? au baada ya masaa kuwa machache. And also remember he is in Aga Khan Hosp. another indian Institution!
 
Hi ya kulazwa ICU nimeiona. lakini does this make us believe that he is that serious? au baada ya masaa kuwa machache. And also remember he is in Aga Khan Hosp. another indian Institution!

Mod, baada ya kuona hii sasa inanukia harufu ya EPA ama ufisadi mwingine, ingehamishiwa katika siasa ili watu wajadili zaidi
 
Manji ana hela za EPA na ndo kama mweka hazina wa CCM na anafanya biashara kwa niaba ya chama cha mafisadi(CCM)na kikwete alimwomba Manji aisadie yanga kwasababu Yanga ni ya CCM na ndio ya Serikali na pia Manji now anawajengea uwanja utaochukua watu kama 20,000 na hoteli ya 4 star,huu ni ufala wa hali ya juu kikwete anafanya maana itakuwa vp kama wapenzi wa simba wakiamua kukipigia kura chama kingine???na ndo mana ata TBL walidhamini both Simba na yanga koz walijua simba hawatakunywa bia zao!!!lakini kwasababu kikwete kazungukwa na washauri wabovu ili hawezi lijua ata kidogo!!kama mbwai ni mbwai basi mwambie Rostam nae aidhamini Simba mana yule ni mpenzi wa simba na ana hela za EPA...
 
Mod, baada ya kuona hii sasa inanukia harufu ya EPA ama ufisadi mwingine, ingehamishiwa katika siasa ili watu wajadili zaidi

Manji ana hela za EPA na ndo kama mweka hazina wa CCM na anafanya biashara kwa niaba ya chama cha mafisadi(CCM)na kikwete alimwomba Manji aisadie yanga kwasababu Yanga ni ya CCM na ndio ya Serikali na pia Manji now anawajengea uwanja utaochukua watu kama 20,000 na hoteli ya 4 star,huu ni ufala wa hali ya juu kikwete anafanya maana itakuwa vp kama wapenzi wa simba wakiamua kukipigia kura chama kingine???na ndo mana ata TBL walidhamini both Simba na yanga koz walijua simba hawatakunywa bia zao!!!lakini kwasababu kikwete kazungukwa na washauri wabovu ili hawezi lijua ata kidogo!!kama mbwai ni mbwai basi mwambie Rostam nae aidhamini Simba mana yule ni mpenzi wa simba na ana hela za EPA...

Arsenal kwa maneno yako hapo juu, tunarudi kwenye ushauri wangu kuihamisha hii topic maana umesema EPA, JK, CCM......!!!!
 
Back
Top Bottom