Maneno matamu ya Barua za Kale...

Maneno matamu ya Barua za Kale...

Slave

JF-Expert Member
Joined
Dec 6, 2010
Posts
5,313
Reaction score
2,651
Salam,

Ama baada ya salamu, mimi ni mzima wa afya njema. Mie ni ndege nipo angani na nimetafuta mti wa kutua kila pembe ya dunia lakini sijaupata bado. Je naweza nikatua kwako?

Nyingine;

Silli silali nakuwaza wewe.. Nikinywa maji nakuona ndani ya kikombe.

Nyingine;

Kutoka kwa akupendae
S.L.P. Mimi na wewe tupendane.


Wakuu hebu niambieni nyingine mlio wahi ona, ama andika/andikiwa. Mnazikumbuka?
 
Hizi hapa mkuu.....

attachment.php
attachment.php
 

Attachments

  • 563211_472428406158305_1580917099_n.jpg
    563211_472428406158305_1580917099_n.jpg
    19.7 KB · Views: 2,156
my father ana barua za wachumba wake woote ,halafu wamama wengine ni wa hapo hapo mtaani.tulikuwa tunasoma na mama tunacheka kweli
kuna mmoja alimwambia nakupenda kama kiazi,basi tunataniana na baba huwa tunachekaje?

Hebu kama zipo karibu chukua moja utunakilie hapa mdogo wangu. Mie nazipenda saana. Lol
 
Mhhm hebu ngoja nizikumbuke...

Nakuridhiya kwa kila hali ujuwe nakupenda kweli :A S shade:

Tuishi milele tusifanye kelele:A S shade:
 
Hebu kama zipo karibu chukua moja utunakilie hapa mdogo wangu. Mie nazipenda saana. Lol
Ngoja nikienda home moshi pasaka my sis !
sina hapa by the way,
salamu sana,je hujambo? baada ya salamu, salamu zikufikie kama mchanga wa bahari wewe ulie mbali na upeo wa macho yangu
 
Ngoja nikienda home moshi pasaka my sis !
sina hapa by the way,
salamu sana,je hujambo? baada ya salamu, salamu zikufikie kama mchanga wa bahari wewe ulie mbali na upeo wa macho yangu
au waweza hitisha kwa "mpende akupendae"
 
Cheka unenepe,
Ukinuna utakonda,
Vumilia Mpenzi,
Mapenzi kuoana,
 
Ngoja nikienda home moshi pasaka my sis !
sina hapa by the way,
salamu sana,je hujambo? baada ya salamu, salamu zikufikie kama mchanga wa bahari wewe ulie mbali na upeo wa macho yangu

Usitie shaka kabisa kipenzi Smile.

Mie mzima kabisa wa afya, hofu na mashaka ni juu yako ulie mbali na uwepo wa macho yangu kama ilivyo kwa utosi na unyayo na kunifanya kujisikia kuumwa kila nikumbushwapo jina lako lililotawala kupitia smile ya wapendwa wangu wote. Natamani waendelee tu kununa. Lol

Miss you so much like Obama misses Osama.
 
Mpende akupendae, asiekupenda achana nae, P.O.Box Sahani moja kula nae.
 
Kijiji cha kupenda
S.L.P MAPENZI.
MOYONI
...
Kwako dada mpendwa

YAH:KUTOA NI MOYO SI UTAJIRI
Salaam ama baada ya salamu mi sijambo ila mawazo tele.Naandika barua hii kwako nikiwa chini ya kivuli,mbele yangu kuna bahari ya mapenzi nataka unikaribishe mie samaki niogelee juu ya mwili wako,,
......Usiogope kama ulivyosema jana maana kupeana mapenzi sio kosa letu bali la adamu na Eva waliokula tunda.Kesho tukutane kisimani saa 10 jioni ili uso wako utoe moyo wangu kifungoni.
.....Mengine mengi sisemi uamuzi nakuachia wewe ambae penzi lako limenipiga shavu la uso.
Ni mimi NIKUPENDAE KWA LUGHA ZOTE
 
Salaam ama baada salaam mimi ni mzima hofu na mashaka ni juu yako wewe uliyembali na upeo wa macho yangu..


Dhumuni,au lengu, au kusudio la kipande hiki cha karatasi...........

Afu unaandika kwa pen ya kunukia then unachora maua na kopa, kipindi hicho hakuna stickers
 
he he he, nakupenda sana AshaDii, kila nikikuwaza namaliza kichane cha ndizi.

Ewe dada mwenye macho ya gololi na shingo ya pingili pingili, umeurarua moyo wangu kama simba araruavyo mwana swala.

🙂 🙂 🙂 🙂 those days lol

Barua za hivi Kongosho, DARKCITY, Mtambuzi na Bujibuji ndiyo hasa wadau wake. :wink:
 
Last edited by a moderator:
he he he, nakupenda sana AshaDii, kila nikikuwaza namaliza kichane cha ndizi.

Ewe dada mwenye macho ya gololi na shingo ya pingili pingili, umeurarua moyo wangu kama simba araruavyo mwana swala.

🙂 🙂 🙂 🙂 those days lol

Ha ha ha! Hii nimeipenda... Pamoja na kutoelewa kwangu kote chane za ndizi zina mahusiano gani... Lol
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom