Maneno matamu ya Barua za Kale...

Maneno matamu ya Barua za Kale...

Salam,

Ama baada ya salamu, mimi ni mzima wa afya njema. Mie ni ndege nipo
angani na nimetafuta mti wa kutua kila pembe ya dunia lakini sijaupata
bado. Je naweza nikatua kwako?

Nyingine;

Silli silali nakuwaza wewe.. Nikinywa maji nakuona ndani ya kikombe.

Nyingine;

Kutoka kwa akupendae
S.L.P. Mimi na wewe tupendane.


Wakuu hebu niambieni nyingine mlio wahi ona, ama andika/andikiwa.
Mnazikumbuka?

Hahahaha! Kuna mmoja alimtumia mpenzi wake card ya harusi kwa kuwa ilikuwa na maua mazuri.
 
kula zabibu rudisha majibu daaa nazikumbuka sana maana nilikua kusema siwezi kabisa ziliniokoa kiasi flani hahahaha
 
hahahahaha! Khaa ''mwenye shingo ya pingili pingili''....kashakuwa muwa tena!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom