Cash Money Forever
JF-Expert Member
- Mar 16, 2019
- 726
- 1,310
Naunga mkono hoja hapo kwenye uwe na watu sahihi kwenye maamuzi na utendaji. Chelsea tuliingia sokoni kusajili mazagazaga mengi kujaza kwenye timu.300m sokoni inatosha kabisa kwa kuanzia, kikubwa uwe na watu sahihi wa Michezo na wafahamu mahitaji ya timu.
TODD Mazungumzo yake ya awali aliotelea Mfano Liverpool kufanya vyema uwanjani huku akiwa anatengeneza faida kwenye mauzo ya wachezaji [aliamua kuchukua kila jina linalotajwa sana sokoni umri mdogo + mkataba wa miaka mingi, hapa Mawakala wengi walimuuza]. Alichofeli hakufahamu kama tayari wenzao wana AINA yao ya uchezaji, {Swali rahisi kwako, Mpaka sasa unajua CFC Inataka chezaje??}
Ukisikiliza Mahojiano ya Mourinho na RIO, anakwambia kabla hujanunua Samani Mpya lazima usafishe Nyumba akiwa na maana kuna wachezaji wa kuuzwa wengi UTD, fikiria mpaka sasa kuna wachezaji wa tangu Fergie, na kibaya kuhusu UTD inatumika na mawakala inawafunga Wachezaji na mikataba Mikubwa mpaka wanakuwa hawauziki.
Jaribu fikiria De Gea mpaka leo hana timu, UTD ni timu ya Pili kwa Bili kubwa ya Mishahara nyuma ya CITY na ilikuwa ya Kwanza kabla {Kwa kipi wanachofanya uwanjani!}
300m unaweza pata "Premium" kama 4 kwa 70m+, ukapata "Potential" kama 6 kwa 50m+ ama "Established" kama 5/6 kwa 55m+. {kwa kuanzia inatosha ukichukua wachezaji muhimu na kuwa "Smart" kwenye makubaliano ya Bei. {Kuna chaguo la mkopo na kipengele cha kununua mbeleni, Benfica wanaipenda hii}
Mpaka leo THE BLUES hatuna style of play, tunacheza bila P.o BOX bora liende.

