fuentte
JF-Expert Member
- Jul 30, 2015
- 3,210
- 9,205
Umenena vema mkuu ila kuna kitu kimoja hujakigusia, MAMLAKA kwa mwalimu na hiyo timu ya nyuma ya pazia.300m sokoni inatosha kabisa kwa kuanzia, kikubwa uwe na watu sahihi wa Michezo na wafahamu mahitaji ya timu.
TODD Mazungumzo yake ya awali aliotelea Mfano Liverpool kufanya vyema uwanjani huku akiwa anatengeneza faida kwenye mauzo ya wachezaji [aliamua kuchukua kila jina linalotajwa sana sokoni umri mdogo + mkataba wa miaka mingi, hapa Mawakala wengi walimuuza]. Alichofeli hakufahamu kama tayari wenzao wana AINA yao ya uchezaji, {Swali rahisi kwako, Mpaka sasa unajua CFC Inataka chezaje??}
Ukisikiliza Mahojiano ya Mourinho na RIO, anakwambia kabla hujanunua Samani Mpya lazima usafishe Nyumba akiwa na maana kuna wachezaji wa kuuzwa wengi UTD, fikiria mpaka sasa kuna wachezaji wa tangu Fergie, na kibaya kuhusu UTD inatumika na mawakala inawafunga Wachezaji na mikataba Mikubwa mpaka wanakuwa hawauziki.
Jaribu fikiria De Gea mpaka leo hana timu, UTD ni timu ya Pili kwa Bili kubwa ya Mishahara nyuma ya CITY na ilikuwa ya Kwanza kabla {Kwa kipi wanachofanya uwanjani!}
300m unaweza pata "Premium" kama 4 kwa 70m+, ukapata "Potential" kama 6 kwa 50m+ ama "Established" kama 5/6 kwa 55m+. {kwa kuanzia inatosha ukichukua wachezaji muhimu na kuwa "Smart" kwenye makubaliano ya Bei. {Kuna chaguo la mkopo na kipengele cha kununua mbeleni, Benfica wanaipenda hii}
Tangu Rashford aibuliwe na LvG akachukuliwa kama upcomimg big talent, ingawa alikuwa anaonyesha dalili zote za kufikia kikomo cha ukuaji kisoka ila kila mwalimu aliyekuwa anakuja alikuwa anamweka kwenye first eleven yake, namba yake uwanjani haifanyiwi usajili wa kumpa changamoto. Bado kuna issue ya Martial pale Mou alipotaka auzwe wenye timu wakaamua vingine
Kwa trend hii madhani kulikuwa na maelezo toka juu kuhusu bwana Rashford,Martial na waingereza wengine wengi tu kama alivyowahi kuropoka Eric Baily kuwa kuna baadhi ya wachezaji wanapewa upendeleo wa makusudi bila kujali kiwango chao nyakati husika.
Pale united pamegeuka uswahilini sana kiasi kwamba unapewa cheo lakini mamlaka hupewi hivyo unakuwa umefungwa mikono tu wakati uko ulingoni.
