Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Timu huhami kizembe huoni bado anajileta humu? Kama yule anayejifanya yupo nyukesto ila kila siku yumo jukwaa la Arsenal
Ni mapito tu haya. Timu ikianza kufanya vizuri utamuona tena. Hata labyrinth anafurahi sana tukishinda ila huwa anajificha na kusherekea pembeni. Tukiendelea kushinda zaidi na zaidi atarejea mazima.
 
Ninachoshukuru angalau nimepata namna ya kuacha kuangalia mechi za Manchester, mwaka mmoja nyuma haikuwa inawezekana kabisa hata niwe wapi lazima niangalie game hata msiba wa bibi nilitoka nikaenda kucheki game.

Leo aaah nalala zangu safii moyo wangu unatulia tulii sio kudunda dunda dakika 90. Kuacha kuishabikia siwezi ila nitaangalia matokeo tu basi.
Nitaiga hii😀
 
20231109_162718.jpg
 
Hii timu inahitaji Mwalimu aina Xavi ama Arteta wa kukaa na timu muda mrefu ili a-implement falsafa yake na apewe muda na resources.

Hata Olegunar angevumiliwa angeifikisha mbali timu.

Hata Kocha wetu Mzee Wenger wakati anafika klabuni alipewa muda ndiyo timu ikaanza kuperfom.

Hata Pep wakati anafika Etihad alipewa muda na fedha ndiyo akaanza kukusanya vikombe.

Ila huyu Ten hug ni kama hana Falsafa inayoeleweka.

Nashauri avunjiwe Mkataba ili apewe kazi kocha mwingine.

All in all Poleni Mashetani Wekundu
 
Kuna kipindi inatokea unatamani international breaks kama hizi ili vijana/wachezaji wapate muda wa kujiuliza au sisi mashabiki tujidai kusahau kama kuna klabu ya mpira inaitwa mashetani wekundu.
 
Back
Top Bottom