El Tiger
Senior Member
- Aug 15, 2018
- 142
- 785
UMEMALIZA JAMAA..Amin kiongozi kwenye mpira kila mtu lazima awe na impact kwenye kutafuta matokeo Antony kwa sasa hana end product nzuri offensively kuliko product yake kama ball carrier and interceptive in a defective role huyu jamaa anatupaga balance flani kwenye mpira unaona kuna equilibrium ya upambanaji kama grelish wa man city jamaa hafungi sana wala kutoa assist ila ni mapafu ya mbwa ana pokonya mipira kupeleka mbele
Upande wa midfield yetu kuna kitu ambacho tulikiona mwanzoni ila tulijua akita last muda mrefu na hii ndio fimbo wanayoitumia rivalry fans wetu kutu adhibu ni umri
Casemiro + Eriksen hawana physicabilities compare tu rice + kai upande wa kupeleka mipira mbele hamiss anasema tumepiga pass 200+ kurudi nyuma ni kweli sababu watu walipo nyuma mostly ni vijana na wana composture nzuri ya ku control Mpira at the back dalot Martinez lindelof awb wote hawa wana weza tawa kwa nyuma na kufanya mpinzani asiwe na intensity yakuwaingilia na ndio maana zikawa successful back 200 pass zilizo being counted kwenye ball possession sasa shida ni nini hizi pass 200+ zisiingie kati hapo kati umri wao hauwaruhus kufanya hivo watakuwa exposed ukilinganisha na mpizani watu wake kati wako vizur composture on the ball
Na hii ikapelekea huduma kuwa mbovu upande wa mbele tunategemea counter hatuwez kuwa vital on attack kama kati hakuna waku submerge the control into the final third ku creat a threat
UTD Mobility kwenye MD ni ndogo mno na hakuna Ball Progressive CM mzuri na Hapa ndo anaingia Amrabat ni Hybrid 6&8, Mobility ya CM's wa Arsenal ni kubwa sana na kama unavyosema wengi ni damu Changa, kama ingekuwa Casa ndo yupo Nyuma ya Ode + Rice Arsenal wangekuwa na Hatari zaidi tokea kati mana Ode angekuwa juu zaidi sehemu ambapo anakuwa na Madhara {Ni shooter mzuri na Excellent Vision} na Rice anaweza kuwa Ball Carrier, Nje ya hapo unaona Arsenal nafasi wanatengeneza zaidi tokea Pembeni Silaha Saka + Martinelli.
UTD jana haikuwa fully force kuna Varane, Shaw, Mount na Possible Amrabat, Hojlund nae ni first 11! Media zetu inafikirisha sana kuhusu Uchambuzi wanafanya, Amrabat wanasema ni WC Player!! Sarri akiwa Chelsea alitaka Ongezewa Barella akiwa bado Cagliari na Amrabat akiwa kwa Mkopo Hellas Verona, Nilikuwa Shabiki sana wa Napoli ya Sarri na nilihisi kina Higuain Ulikuwa mwaka wao ila Serie A ina changamoto ya Officials sana japo ni wazuri ukifananisha na EPL. {Jorginho, Amrabat + Barella (Ingekuwa Trio nzuri sana)}
De Gea alikuwa Mzigo UTD, Timu kama UTD haitakiwi itegemee miujiza ya Goalie, Ni kati ya Best Shot Stopper ever, ila Mpira umebadilika sana asee, Jaribu waza Onana ndo awe kwa Ramsdale ambae jana alikuwa akifatwa kwa Pressure kubwa anapiga High balls ambazo ni za kuuza, Onana angefanya wawe na Turnover nyingi sana sababu ya Mobility ya Players wake wengi. {PFA wamemlinda Ramsdale sababu mtoto wa Nyumbani ila ni Muda mwafaka RAYA kuchukua nafasi} Kingine Mshahara mkubwa sana Onana inasemekana anachukua 1/3 ya kile alokuwa anakula De Gea,De Gea anatukosti kwenye suala la kutawala eneo lake kwa miguu
EPL wanajua kabisa Officials wao ni Averages sana ndo mana walikataa "Semi Automated Offside Technology" Ligi nyingi zinatumia hii sasa. Ingawa ni suala la Muda tu wataungana nayo kama System ya Kuokoa Muda ulopotea waloamua kuja nayo. EPL wahafidhina sana hata VAR waliikataaga awali.
