Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Amin kiongozi kwenye mpira kila mtu lazima awe na impact kwenye kutafuta matokeo Antony kwa sasa hana end product nzuri offensively kuliko product yake kama ball carrier and interceptive in a defective role huyu jamaa anatupaga balance flani kwenye mpira unaona kuna equilibrium ya upambanaji kama grelish wa man city jamaa hafungi sana wala kutoa assist ila ni mapafu ya mbwa ana pokonya mipira kupeleka mbele

Upande wa midfield yetu kuna kitu ambacho tulikiona mwanzoni ila tulijua akita last muda mrefu na hii ndio fimbo wanayoitumia rivalry fans wetu kutu adhibu ni umri
Casemiro + Eriksen hawana physicabilities compare tu rice + kai upande wa kupeleka mipira mbele hamiss anasema tumepiga pass 200+ kurudi nyuma ni kweli sababu watu walipo nyuma mostly ni vijana na wana composture nzuri ya ku control Mpira at the back dalot Martinez lindelof awb wote hawa wana weza tawa kwa nyuma na kufanya mpinzani asiwe na intensity yakuwaingilia na ndio maana zikawa successful back 200 pass zilizo being counted kwenye ball possession sasa shida ni nini hizi pass 200+ zisiingie kati hapo kati umri wao hauwaruhus kufanya hivo watakuwa exposed ukilinganisha na mpizani watu wake kati wako vizur composture on the ball
Na hii ikapelekea huduma kuwa mbovu upande wa mbele tunategemea counter hatuwez kuwa vital on attack kama kati hakuna waku submerge the control into the final third ku creat a threat
UMEMALIZA JAMAA..

UTD Mobility kwenye MD ni ndogo mno na hakuna Ball Progressive CM mzuri na Hapa ndo anaingia Amrabat ni Hybrid 6&8, Mobility ya CM's wa Arsenal ni kubwa sana na kama unavyosema wengi ni damu Changa, kama ingekuwa Casa ndo yupo Nyuma ya Ode + Rice Arsenal wangekuwa na Hatari zaidi tokea kati mana Ode angekuwa juu zaidi sehemu ambapo anakuwa na Madhara {Ni shooter mzuri na Excellent Vision} na Rice anaweza kuwa Ball Carrier, Nje ya hapo unaona Arsenal nafasi wanatengeneza zaidi tokea Pembeni Silaha Saka + Martinelli.

UTD jana haikuwa fully force kuna Varane, Shaw, Mount na Possible Amrabat, Hojlund nae ni first 11! Media zetu inafikirisha sana kuhusu Uchambuzi wanafanya, Amrabat wanasema ni WC Player!! Sarri akiwa Chelsea alitaka Ongezewa Barella akiwa bado Cagliari na Amrabat akiwa kwa Mkopo Hellas Verona, Nilikuwa Shabiki sana wa Napoli ya Sarri na nilihisi kina Higuain Ulikuwa mwaka wao ila Serie A ina changamoto ya Officials sana japo ni wazuri ukifananisha na EPL. {Jorginho, Amrabat + Barella (Ingekuwa Trio nzuri sana)}

De Gea anatukosti kwenye suala la kutawala eneo lake kwa miguu
De Gea alikuwa Mzigo UTD, Timu kama UTD haitakiwi itegemee miujiza ya Goalie, Ni kati ya Best Shot Stopper ever, ila Mpira umebadilika sana asee, Jaribu waza Onana ndo awe kwa Ramsdale ambae jana alikuwa akifatwa kwa Pressure kubwa anapiga High balls ambazo ni za kuuza, Onana angefanya wawe na Turnover nyingi sana sababu ya Mobility ya Players wake wengi. {PFA wamemlinda Ramsdale sababu mtoto wa Nyumbani ila ni Muda mwafaka RAYA kuchukua nafasi} Kingine Mshahara mkubwa sana Onana inasemekana anachukua 1/3 ya kile alokuwa anakula De Gea,

EPL wanajua kabisa Officials wao ni Averages sana ndo mana walikataa "Semi Automated Offside Technology" Ligi nyingi zinatumia hii sasa. Ingawa ni suala la Muda tu wataungana nayo kama System ya Kuokoa Muda ulopotea waloamua kuja nayo. EPL wahafidhina sana hata VAR waliikataaga awali.
 
Hapa rashford sijui alichokuwa ana waza rooney na ronaldo ktk counter kama hizi huponi walikuwa wakiwaza magoli kwa ajili ya timu hapa rashford alijiwazia yy tu
IMG_0889.jpg
 
Sasa Martinez Kama kaumia ulitaka aendelee kucheza?
Ila ndio football lakin the one with quality ata decided the match ... Yani tunatoa Martinez na lindelof kwa john evans na Maguire mpaka hapo mashabik wa man utd tulijua mshashinda
Sababu hatuna quality bench compare na wao

Sababu za kufungwa ni upangiliaje mchezo wa kocha martial mzito sana...sub ikitokea ya Antony unajua uwanja utainama maana jamaa anajua kurudi kufanya ball carrier kupokonya mipira kupeleka mbele...kuhusu center back ndio itilafu Martinez hawez cheza mechi nzima kawa pancha sana + varane pia hi duo sasa hivi ni hospital mates
 
Kosa la glazer ni lipi?

Wamempa pesa huyo jasusi kaenda kusajili wahuni tu.

Onana ana kipi cha kumzidi degea?View attachment 2738231
Ety kosa la glazers ni lipi, unaleta utani kwa mambo yaliyo serious, kwa akili yako unafikiri degea Ana kipi! Cha kumzidi onana au unafikiri mpira wa sasa utahitaji makipa walio shot stoper tu.

Hao glazers hukumbuki interview ya Cristiano Ronaldo.
 
Pamoja kupoteza mechi lakini team inazidi kubadilika.

Mosi ni suala muda tu huyu dogo number 9 akizoea mfumo ni hatari sana.urefu wake na skill ni tatizo kubwa kwa team pinzani zs baadae.

Onana katengeneza confidence kubwa back 4 isipokuwa tupunguze mipira ya nyuma.

Baada ya mechi za kimataifa tutaanza kuona Man.
 
Mkuu mimi hili suala la VAR linanichanganya kila siku. Hawa waamuzi wa VAR wakiwa wanarudia utaona kabisa mstari sio perpendicular ila kama unatengeneza angle aidha ndogo kuliko nyuzi 90 au kubwa kuliko nyuzi 90 halafu wanahitimisha kuwa ni offside au la. Mfano mzuri ni offside ya goli la Garnacho,mstari haukuwa nyuzi 90 bali ulilala ndio maana maamuzi yalikuja vile refa alivyotaka.

Hata hii picha yako mkuu asahd mstari haukunyooka ila umelala kidogo kumfuata beki wa mwisho wa arsenal,labda kama mstari wa pembeni haiko sawa sana.

Hata uwe gk bora namna gani? Mbele yako wakiwekwa mabeki kama wale lazima uumie
 
IMG_0897.jpg



Hapa kuna mtu sijui sasa rashford na anthony kama wataweza kwenda nae sambamba wakiacha ubinafsi hili ni tatizo pale mbele ni moto haswaa kuna beki jana kaacha mpira kamdaka mwili mzima kwenye 18

Rasmus Højlund
 
Hii nafasi ilikua goli kabisa jamaa huwa simkubali sababu ya uselfish na utoto wake.
Rasmus alimaind kwenye hii move. Baada ya Rashid kupiga ule mpira ukaishia kwa mabeki akarusha mikono juu kwa hasira,yaan ingekuwa inawezekana kuingia ndani ya Tv basi jana ningeingia nkampige mawe yule umbwa Rashid
 
Back
Top Bottom