Kwa mara ya kwanza, naanza kuwa na mashaka na Moyes. Bado naamini katika yeye kupewa muda, lakini imani inaanza kushuka kwa kasi sana. Na inazidi kuwa ngumu kuendelea kuwa na imani hiyo.
Kafanya upuuzi sana katika kufanya subs. Pamoja na makosa ya refa, United ilipokuwa 2-0 down, Moyes alipaswa kufanya sub. Anakuja kufanya subs dakika za lala salama, anamtoa Fellaini na kumwingiza Tom. Anamwacha RvP ndani, aliyekuwa kivuli tu, na kuacha kumwingiza Shinji.
Timu iliyoanza leo, ilikuwa ni the strongest katika msimu huu. Sasa naamini, shida yaweza kuwa ni kwenye tactics za Moyes.
Game ya J5 hakika inaweza kuamua fate ya Moyes pale OT.
Anyway, msimu huu, tayari nimeshaweka silaha chini. Ngoja msimu uishe, tuone kama bodi itamwamini kwa kumpa mamilioni ya paundi kujenga timu, ama katika bodi kutakuwa na mtu mwenye kifua cha kumwambia SAF ulichemsha, na tunahitaji kocha mpya.
Ngumu sana kumeza kwa kufungwa na loserfools.