Forgotten
JF-Expert Member
- Jul 20, 2018
- 3,630
- 11,098
Usiamini sana maneno ya kocha na kikosi chake.Soma hapa chini ni makocha wawili, mmoja licha ya kubeba europa na kumaliza nafasi ya pili bado alihitaji at least wachezaji wapya watano, Huyu mwingine licha ya kupewa fuko la goli saba bila na looser fool, kapigwa sita na manshity still anakuambia ameridhika na kikosi chake
Imagine huyu ndio kocha tunategemea aturudishe kwenye glory days
View attachment 2690656View attachment 2690657
Ninachokumbuka mara ya mwisho mtu kuongea ukweli kwenye media "Ralf Rangnick" alitimuliwa na Glazers.
EtH ni muajiriwa, pamoja na mapenzi yake na football anatafuta pesa. Usitegemee atoke hadharani aanze kusema sitaki hawa wachezaji hawanifai au awaseme wamiliki hawatoi pesa, ukisema hivyo maana yake mwajiri atatafuta competent candidate kuendana na mazingira ya kazi maana wewe umeshindwa.
Wachezaji ni binadamu, kama kocha kazi ya kwanza ni kuhakikisha wana imani na wewe. Sasa ukisema hawakufai inapaswa uwe umejiandaa kuwaondoa.
Chukulia mfano wewe ni mchezaji na una mkataba na timu halafu kocha anaenda kwenye media kusema hauna uwezo wa kufanya naye kazi. Wewe kama binadamu hiyo kauli utaipokeaje?