Nani kakwambia sio shot stopper?
Mbona akiwa Ajax na Inter hajaruhusu bao nyingi na msimu ulioisha ndio kipa aliyeruhusu bao chache kuliko wote Champions League na cleansheets za kutosha.
Huyu aliyekuwa anaruhusu bao 6,7,5 hata 4 ndio stopper mzuri eeh?

Kazi ya Kipa Duniani kote inajulikana na ukiona kasimama golini ujue anafanya kazi yake la sivyo tungekuwa tunaona makipa wanaruhusu bao 5+ week in week out.
Kuhusu uchezaji wake eti kufanya makosa inaonekana kuna kitu hukifahamu,modern goalkeepers ndio style yao na ni mara chache kufanya makosa waangalie Ederson na Allison namna wanavyozirahisishia timu zao kutengeneza mashambulizi pia wana uwezo wa kuhimili pressing ya washambuliaji wa opponent team ,wakipiga mipira mirefu inaenda kwa malengo.
Haya huyu De Gea ambaye stopper nadhani unaonaga maboko anayochoma miguuni akibutua mpira mbele unaenda nje au anagawa bure kwa wapinzani yaani anapiga bila vision.
Na kuhusu nidhamu hilo kwa Onana hilo kazi ua kocha kudeal nalo na ishu ya kufukuzwa mwaka jana kambi ya Cameroon kuna vitu nyuma ya lile sakata ambayo haviingiliani na nidhamu yake hizo unazosikia ni stori za kufungwa.
Kafuatilie kama ana historia ya matatizo ya kinidhamu(lile la kutumia madawa yasiyoruhusiwa lisiwepo).
Soka limebadilika