Annie X6
JF-Expert Member
- Mar 16, 2023
- 725
- 1,377
Safishasafisha inaendelea.Habar za leo ndugu zangu, leo naomba nichangie kidogo kwenye hili jukwaa baada ya kimya kirefu.
Kitu cha kwanza ambacho inabidi tukubali ni kwamba kwa sasa tupo nyuma sana na washindani wetu wakubwa kwenye Ligi achia mbali UEFA, na ni ngumu kupata timu ya kugombea ubingwa kwa msimu ujao( kama tutaendeleaa kuwa chini ya Glazer). Kama Muarabu atachukua timu safari yetu itakuwa fupi,
Maelzo yangu ni assumption kama timu haitaenda kwa mwarabu kabla diriaha halijafungwa
Kwa dirisha hili la usajili kwangu naona litakuwa limekwenda vizuri endapo tutakuwa tumepunguza wachezaji mizigo( wasio na msaada) kuliko hata kusajili wachezaji wapya wengi.
Wachezaji kama Wanbissaka(Sababu Dalot katoka kupewa mkataba) ,Maguire,Mctominay,Martial,Elanga,Brandon Williams,Van de beek unaweza ukawauza kwa pesa za nyanya ukakusanya ukapata mchezaji mmoja au wawili wanaoweza kuwa na impact kubwa kuliko kundi kubwa la wachezaji wasio na faida.
Kwangu ni bora kubaki na Maino na Zidan kuliko kumtegema Mctominay auu Fred.
Kwa mtazamo wangu natamani tungepata kipa zaidi ya Degea, ila kwa bajeti hii ya maandazi sioni hili likitokea. Kwa hiyo Dean angerudi ili agombanie namba na De gea,(uzuri wa Ten Hag) ana uwezo wa kumuweka benchi mchezaji yoyoye ambaye ana under perfom. Ila ili uweze kumuweka benchi ni lazima unaye mpa nafasi awe bora kuliko unaye muweka benchi. ( hii ingeleta chamgamoto chanya kwenye nafasi ya golkipa) tungeweza kusogea kidogo.
Halafu hela zote zile zitazopatikana kwa kuuza wachezaji wa mafungu zingeelekezwa kwenye nafasi ya Ushambuliaji (Tungepata Striker mmoj wa maana) na mchezaji kiraka mmoja mfano wa Caicedo. Ukipata mchezaji kama huyu unakuwa ni kama una wachezaji wawili au watatu. Anaweza kucheza kwa ufasaha zaidi ya nafasi mbili.
Binafsi naona Ten Hag amefanya kazi nzuri kwa msimu wake wa kwanza ila kama hatapewa support ya dhati tutarud pale pale kwamba kocha hafai.
Kaeni kwa kitulia










Casemiro: “In Brazil, we always say that your first line of defence is your number nine, or your striker. In modern football, you defend with all 11 players, and you attack with all 11 too. That is how football is nowadays.”