Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Sijui kwanini sitaki Kane ajiunge na man United.

Nikiangalia umri na fedha watakayotaka Spurs nadhani tungetafuta option nyingine.
Naona kununuliwa kwa Kane kunapigiwa chapuo na vyombo vya habari vya Uingereza zaidi kuliko mahitaji halisi ya kocha.
Ukiwauliza kwanini Kane na sio damu changa watakwambia EPL proven player,hakuna la ziada
 
Heshima sana,

Bora leo tumeshinda tunaweza kujadiliana pasipo bugudha.

Nakubaliana na wewe Kane ni Bonge la striker lakini ule UK wake unampandisha sana bei bila kusahau Chairman wa Spurs ni mtu wa vurugu nyingi katika masuala ya usajili.

Nadhani ni muda muafaka sasa tukajenga Team ya kesho na keshokutwa.

Ningependa sana kama tungempata mshambuliaji wa kati ya miaka 20 to 26.Mshambuliaji wa umri huu unaweza kukaa naye hata miaka 10 na bado ukamuuza.Ukimchukua leo Kane huwezi ku muuza tena ana miaka 3 hadi 5 tu.
Kane ndiyo option nzuri, hao watoto wa 20s ndiyo sitaki hata kuwasikia. Ni wachezaji wachache sana kwenye early 20s wanakuwa wamekomaa kiakili.

Kane suala la umri siyo la msingi sana ila kile atakachoongeza kwenye safu yetu ya ushambuliaji. Kane ni 'a complete striker' anafunga na kutengeneza nafasi: ata-partner vizuri sana na Rashford.

United mfumo wetu hauhitaji poacher, wingers wetu hawachezi kutengeneza nafasi. Tunahitaji striker atakayeweza ku-drop deep na kucheza kama namba 10 kuweza ku-create chances kwa mtu kama Rashford.

Umri na pesa isiwe kigezo cha kumkosa Kane. Hawa ndiyo watu wa kazi tunawakosa kwenye timu, baada ya Kane tunaweza sasa kutafuta kijana atakayepikwa kwa matarajio ya baada ya misimu 3 aongose safu ya ushambuliaji.
 
Kane ndiyo option nzuri, hao watoto wa 20s ndiyo sitaki hata kuwasikia. Ni wachezaji wachache sana kwenye early 20s wanakuwa wamekomaa kiakili.

Kane suala la umri siyo la msingi sana ila kile atakachoongeza kwenye safu yetu ya ushambuliaji. Kane ni 'a complete striker' anafunga na kutengeneza nafasi: ata-partner vizuri sana na Rashford.

United mfumo wetu hauhitaji poacher, wingers wetu hawachezi kutengeneza nafasi. Tunahitaji striker atakayeweza ku-drop deep na kucheza kama namba 10 kuweza ku-create chances kwa mtu kama Rashford.

Umri na pesa isiwe kigezo cha kumkosa Kane. Hawa ndiyo watu wa kazi tunawakosa kwenye timu, baada ya Kane tunaweza sasa kutafuta kijana atakayepikwa kwa matarajio ya baada ya misimu 3 aongose safu ya ushambuliaji.
Kane atauzwa 100 Million 🙏.Budget yaweza kuwa 110 Milion.

Bado tunahitaji kiungo,Beki wa kulia na winger wa kulia na ikiwezekana kipa.

Kwa uchache tunahitaji five new players.
 
Hivi vitoto vinafanya tujione wazee. 😄
18 & 16 wanatarajia kupata mtoto.
20230430_203415.jpg
 
Binafsi nikiona shabiki wetu anamu-attack Ten Hag huwa napata sana mashaka nae. Tulipokuwepo mpaka sasa ni hatua kubwa tena kuna watu humu wanajitoa ufahamu hakuna mtu aliyetupa nafasi hata ya kumaliza top 4 msimu huu.

Msimu uliopita tulishinda michezo 20 tu msimu mzima ila mpaka sasa tumeshinda michezo 37. Barani ulaya ktk ligi 5 kubwa ni sisi na Man City tulioshinda michezo mingi msimu huu (37).

Pia tulikuwa na clean sheets 8 tu ktk mechi 38 ila msimu huu tunazo 15 ktk mechi 32 EPL kuliko timu yoyote ile tukifwatiwa na Newcastle wenye 13 ktk mechi 33. Naamini tupo ktk njia sahihi ni swala la muda Ten Hag akijenga timu yake kamili tutarudi ktk reli.
Kheee kumbe huyu jasusi ten hag unajua mpaka kiswahili?
 
Martial amekuja hapo Manchester hakiwa na miaka 21 tu Mpaka leo katufanyia nini cha maana ni heli tupate Kane tumtumie hata misimu mitatu au minne tu.
Huyo Kane ukimnunua leo ukitaka muuza kesho huwezi tena.
 
Usisahau Ronaldo alikuja akiwa na miaka mingapi.

Wakati wa Jose alishapendekeza tumuuze Martial wenye Team wakamgomea.

Sijakataa Kane ni mzuri lakini fedha yake ingetumika vyema tungeweza kupata washambuliaji wawili.

Tatizo letu ukilitaza utagundua team ina passengers wengi sana.leo wakiumia Rashford,Bruno au Casemiro tunapoteza mwelekeo kabisa.Dirisha dogo tumchukua kwa mkopo ngongoti hana uwezo wa kukaa na mpira,hana uwezo wa kutoa pasi za uhakika,hana uwezo wa kufunga,hana uwezo wa kuokoa jahazi team inapokuwa katika wakati mgumu.Ukweli ni very average player hasiyestahili kuvaa uzi wa Man.

Kwanini Ngongoti alisajiliwa badala world class striker,jibu ni rahisi sana fedha nyingi zilitumika kunsajili Anthony.
Wasiwasi wangu tunaweza kutumia fedha nyingi kumsajili Kane tukaacha maeneo mengine mengi yanayohitaji usajili wa maana ikiwemo mlinzi wa kati,kulia na eneo la kiungo.
Unatoa 100M kununua striker atakaeumia mnarudi kwenye default settings.
 
Kane atauzwa 100 Million .Budget yaweza kuwa 110 Milion.

Bado tunahitaji kiungo,Beki wa kulia na winger wa kulia na ikiwezekana kipa.

Kwa uchache tunahitaji five new players.
Kutoa 100M kumchukua Kane lazima kuwe na 400M nyingine pembeni ya kuziba hizo nafasi zilizobaki.
 
Muache kumlaumu kocha, katutoa mbali....na anafanya kazi kubwa tuwe bora zaidi....mm naamini akisajili tena atakuwa na sub nzur, na atafany vizuri....na aliahidi msimu wa tatu mmudai ubingwa either EPL au UEFA....TRUST THE PROCESS.
Ana maamuzi ya kijinga sn haswa upande wa sare kuna mechi km tatu sub zake zimefanya tumetoka sare.. angalia gem kama na sevilla ila tupo home rejea pia gem ya spurs
 
Back
Top Bottom