Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Hata mimi naona kama watampiga chini ili kuendeleza utamaduni wa Kiingereza kwa kuhofia Mwarabu kuleta mambo mengi ndani ya klabu..Manchester United ibebeba utamaduni wa Kiingereza.
London Asilimia Kubwa ni Biashara za Qatar, Dubai, Saudi na India. Unless Mashabiki wanaoenda kwenye Mechi wakatae watampa timu. Mwisho wa Mwezi tutajua nani na nani wapo kwenye mbio
 
HAWA FA MBONA WANATUCHELEWESHEA KUONGOZA LIGI
Screenshot_20230220_201836_All%20Goals.jpg
 
Mkumbuke anayeiuza hiyo timu sio muingereza na ni mfanyabiashara.
Kuna mambo mengi ukitoa mmiliki (mmuzaji) na mnunuzi. Manchester United ni biashara ipo ndani ya UK. United ni nembo ya soka la Uingereza, tumeshaona nguvu ya serikali kwa club kama Chelsea na mmiliki wao aliyepita ni ishu za kisiasa ndiyo zilifanya auze timu kwa lazima. Hili suala siyo la matajiri tu serikali na siasa zake pia watajichomeka hapa.

Mimi nataka timu apewe muarabu bila kizuizi chochote na sisi tufaidi "oil money"
 
Hata mimi naona kama watampiga chini ili kuendeleza utamaduni wa Kiingereza kwa kuhofia Mwarabu kuleta mambo mengi ndani ya klabu..Manchester United ibebeba utamaduni wa Kiingereza.
Haya mambo magumu sana, kwanza muarabu akipewa timu itabidi akubali timu yake ishiriki The Rainbow Laces campaign ambayo ni lazima kila mshiriki wa Premier League a-support LGBTQ community.

Sasa kwa ule mtiti walioleta Qatar kwenye World Cup kupiga vita LGBTQ bado wanataka wapewe timu ambayo inaenda kinyume na wanachokiamini.

Hapa ndiyo ile kauli ya "maisha bila unafiki hayaendi" itabidi itumike.
 
Tuna Struggle sana Bila Case na Eriksen, Fred na Sabitzer sio wa Kuanza pamoja, Quality zao zinafanana, kama jana isingekua De Gea 1st half ni majanga,

Kama ulikuwa unamuona ETH jana alimind sana muda wote anatingisha kichwa.

Dirisha lijalo nahisi mbio za FDJ zitaanza tena.
Inabidi kuwe na backup ya DeJong kama akija kuzingua tena.

Hatuwezi kimbiza mchezaji mmoja dirisha zima halafu tunakuja ambulia patupu.

Tuwe na options kama 3 hivi.
 
Tuna Struggle sana Bila Case na Eriksen, Fred na Sabitzer sio wa Kuanza pamoja, Quality zao zinafanana, kama jana isingekua De Gea 1st half ni majanga,

Kama ulikuwa unamuona ETH jana alimind sana muda wote anatingisha kichwa.

Dirisha lijalo nahisi mbio za FDJ zitaanza tena.
Mkuu , ile apk ulituwekea hapa ili lazimisha nii update sasa baada ya hapo iyo mpya ina matangazo kama takataka. Kwa niaba naomba update yake au utupatie chimbo zinapopatikana ili tuwe tunadownload
 
Haya mambo magumu sana, kwanza muarabu akipewa timu itabidi akubali timu yake ishiriki The Rainbow Laces campaign ambayo ni lazima kila mshiriki wa Premier League a-support LGBTQ community.

Sasa kwa ule mtiti walioleta Qatar kwenye World Cup kupiga vita LGBTQ bado wanataka wapewe timu ambayo inaenda kinyume na wanachokiamini.

Hapa ndiyo ile kauli ya "maisha bila unafiki hayaendi" itabidi itumike.
Qatar na nchi zote za kiarabu hawajawahi kuwa na shida na hao mashoga wakiwa nje ya nchi zao.

Wao wanakuzingua ukileta ushoga ndani ya mipaka ya nchi zao.

PSG inamilikiwa na hao waarabu na mambo ya kishoga wanayafanya mbona?

Newcastle, Man City hakuna aliezuiliwa kufanya huo ushoga.

Ila huruhusiwi kupeleka habari zako za kishoga ndani ya nchi zao.

Still, kutowapa timu hakuleti mantiki kama hakuna sababu ya maana.
 
Mkuu , ile apk ulituwekea hapa ili lazimisha nii update sasa baada ya hapo iyo mpya ina matangazo kama takataka. Kwa niaba naomba update yake au utupatie chimbo zinapopatikana ili tuwe tunadownload
Kuna forum Fulani ya Ukraine inaitwa Mobilism mkuu App zozote za kuchakachua huwa zinapatikana huko.


Hio hapo sema uwe na Adblocker wakati unadownload.

Ukishindwa nitadownload nikuwekee mediafire ama Google drive
 
Unahisi kwa sasa tunafanana uchezaji na Liverpool ya Salah na Mane waki-shine kuliko striker wao Firmino?
kwa huu muda mfupi niliomsoma Eth ni kwamba jamaa hana Formula, anatumia Alichonacho halazimishi, Tofauti na Pep na Klopp. Sasa hivi Liver wanazingua ila Klopp bado anakomaa tu na 4-3-3 yake.

Utofauti uliopo ni kwamba Wout ni mkabaji wakati Firmino ni mtengenezaji, Sisi chance zetu zinatoka kwa midfield na Bruno popote alipo, Wakati Klop midfield zake hazina kazi ya kutengeneza Chance zinatoka kwa Full back na wa mbele. Pia naona Eth no 10 kwake ana Experiment sana, Anapenda kumtumia Bruno toka pembeni, Sometime 10 anacheza Wout, Fred, Sancho huwa hapana mtu maalum pale. Hivyo kwa muono wangu ni Mifumo miwili tofauti.
 
Back
Top Bottom