Weghorst alifanya kila kitu muhimu second half hasa alipocheza kama second striker.
Tupate historia fupi ya mtoto wa tajiri Wout Weghorst.
Agosti 7, 1993 mama Astrid Weghorst alikuwa amejifungua mtoto wa 3 Wout Weghorst kwa ushirika na kibopa Bw. Frans pale Borne Uholanzi.
Hawa ni wazazi wa watoto 4 ambao wote ni wa Kiume! Katika familia ya watu hawa hakujawahi kutokea mchezaji na hata Wout alipowaambia anataka kuwa mchezaji alipuuzwa na kutakiwa kusoma Biashara aje aendeleze utajiri.
Tangu utotoni alipenda sana mpira na licha ya kukosolewa kuanzia nyumbani mpaka kwenye klabu ya mtaani ya NEO akionekana 'kilaza' zaidi bado hakukata tamaa.
Licha ya wazazi kumgombeza aache mpira ila alikaidi na wakamruhusu acheze lakini asikose shule! Yeye aliamini shule atasoma akishindwa mpira! 2010 alijiunga na timu ya Deto lakini hakudumu sana kwani alionekana ni mrefu asiye na kipaji!
Mama yake aliamua kutumia ushoga wake na Mke wa C.E.O wa klabu ya Willem II Bw. Jan Van Esch na kumuombea nafasi mwanae atulize nafsi kwenye klabu hiyo! Alifanikiwa ila bado watu walisema ana mabavu, mkaidi na hana hatari.
AZ Alkmaar ilimsajili 2015 na licha ya kupingwa mwanzoni aliwasuta waliompinga kwa kufunga magoli 68 na assists 25 kwenye mechi 197.
2018 akasainiwa na Wolfsburg ya Ujerumani alikofunga magoli 74 kwenye mechi 127 na assists 21 kabla ya 'Disko lake kuingiliwa na Masai' alipotua Burnley! Mambo yalikuwa magumu kwani alifunga goli 2, assists 3 kwenye mechi 20 na wakamtoa kwenda Beşiktaş alikofunga goli 9 na assists 4 kwenye games 18.
Ndiye aliyewalamba chuma 2 Argentina kwenye World Cup juzi juzi! Ana futi 6.6 na ni mrefu zaidi pale United na wa pili baada ya Van De Sar!
'Va'uti Veghost' ni mmaliziaji mzuri ingali ana 'Footwork' mbovu tu kama walivyo waviziaji wengi duniani! Anaenda kuongeza 'Vurugu' ya United kwenye boksi la wapinzani.
Shida yake kubwa ni kutolinda kiwango chake na ukaidi! Akiwa kwenye ubora wake ni ongezeko la faida mno! Ni mume wa mrembo mwenye akili kubwa, Nikki Van Esch na hudaiwa kufikiria sana mechi! Siku 2 kabla ya mechi hujitenga chumba na mkewe... Pia hapendi bugdha!
Ana Masters ya Biashara! Anacheza mpira kwa furaha zaidi! Familia yao kwa sasa ina petrol station za mafuta zaidi ya 130! Kiufupi sana!
Credit: Nazareth Upete