Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Sema jana tuliupiga mwingi sana hayo mengine makosa ya kawaida tu tulishindwa wenyewe kuua game kwa nafasi tulizopata.

Muhimu tuna uwezo wa kurudisha goal wakitutangulia sio kipindi cha rangnick tukiwekwa tu goal ujue nitolee io.
Kama mnajipa credit kwa mpira mliocheza dhidi ya Leeds basi mna safari ndefu sana.

Leeds ni moja kati ya timu mbovu kwa sasa kwenye EPL, ikifuatiwa na Crystal Palace, both offensively and defensively.

Hata baada ya kuongoza 2-0, sikutegemea kama wataweza kushikilia bomba mpaka mwisho, nilijua tu either watapoteza mechi au wata draw kwa namna ya uchezaji wao. Ni wabovu haswa!

Lakini nashangaa humu kuna watu wanachukulia mechi na Leeds kama kipimo. So sad! Manyumbu mnatia huruma.
 
We mbona umefumuliwa malinda na Everton, nasisi tumetulia kimya tu kama hakijatokea kitu, unadhani hatuna habar yako?
 
Hatukatai kama ni wabovu, sema kuna game na game wanakua vizuri ndio kama jana, waliipania ile game na wakatushangaza kweli.
 
Jana ngapi ngapi mkuu?
 

*****
 
Everton kamfunga arsenal, unaweza kuwabeza arsenal kisa kafungwa na everton?? Leeds ni wabovu, wametimua kocha so kocha mpya lzma aje na hamasa na morali ya wachezaji huwaga inaongezeka na hiko ndo kilichotokea jana..
Ilikua ni suprise kwa man u coz ten hag gemu aliichukulia poa sn
 
Guardiola ndio kocha ambaye anafanya vizuri kwenye kukomesha ubinafsi kwa wachezaji kwa asilimia kubwa timu zote kwa vipindi alivyofundisha tabia hiyo ipo kwa asilimia ndogo sana na mara nyingi wachezaji wake wanapenda kupasiana hata wakiwa kwenye nafasi clear za kufunga.
 
Mkuu umewaza kama mimi. Mara nyingi ni ngumu sana au ni mara chache sana kocha anayechukua nafasi ya kocha aliyetimuliwa akapoteza mechi yake ya kwanza ni nadra sana. Niliposikia Leeds wamefukuza kocha nikaanza kupata mashaka ya kuwa gemu yetu itakuwa ngumu maana tutakamiwa na wachezaji watakao pewa nafasi na kocha mpya, na ndicho kilichotokea yaan kabla hatujakaa vizuri wakafanya yao mapema ili tupaniki na hayo ni maelekezo waliyopewa nadhani na kocha wao kwamba wapate goli mapema ngoma iwe ngumu. Hata na hivyo yapaswa tuwapongeze wachezaji wetu ile ngoma jana ilikuwa tunalala na viatu.
 
Uache kuangalia mechi za timu yako tu. Gnonto ni wa kawaida tu hadi nikashangaa jana anavyowapa shida
 
Leeds walikua wana press sn na kucheza kwa nidham ya hali ya juuu mala nying beki zetu zilkua zinapiga back pass..
Leed walkua more intense kuliko sisi, second balls nyng walkua wana win wao..
Kipnd cha pili kidogo hali ilibadilka..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…