Glazzer wanataka 7B, sasa hivi kila Bilionea tunahusishwa nae.
Mkuu tutabishana sana hapa, akinunua Newcastle 12 baada ya miaka 12 anapata zaidi ya 20B![]()
Saudi Arabia wants its investors to own Manchester United and Liverpool
Sports minister Prince Abdulaziz bin Turki Al-Faisal revealed the countrys latest sporting ambitions in an interview with Sky News - with the sovereign wealth fund already owning Newcastle and now funding LIV Golfwww.skysports.com
Kama nilivyosema mwanzo.
Man Utd ni hot cake.
Mtu akiinunua kwa £7bn akiongeza thamani, miaka 10 ijayo ataiuza si chini ya £12bn.
Boss, pengine hauko informed sana juu ya hili.City imenunuliwa kwa pesa kidogo na mmiliki ame invest kama $1B to $2B Thamani ya City na UTD haina utofauti.
Boss, kumbuka tunaongelea first world country hapa. Acha hizi story za shithole countries.Glazzer alikuwa hawana hela ya kununua United, kwanini Bank iwape makapuku kama hawa pesa ndefu yote hio kuinunua United? Lazima kuna deal la chini ya kapeti wameingia ili Bank ifaidike, matokeo yake timu ambayo haikuwa na deni kwa zaidi ya miaka 100 imelipa Riba matrilioni ndani ya muda mfupi.
Kwani mkuu miaka 15 ama 20 iliopita Man city si alikuwa anacheza Championship?
Halafu cha ajabu leo Ronaldo kawa MoTM!Bruno Fernandes’ last 4 games for Portugal:
vs. Czech Republic
vs. Spain
vs. Nigeria
vs. Ghana
#RonaLdoFinallYOUT
#GlazerOUT
#GGMU
man utd |
Hiyo sio investment strategy ya kila mtu.Mkuu tutabishana sana hapa, akinunua Newcastle 12 baada ya miaka 12 anapata zaidi ya 20B
hoja hii sijaikataa, ndio mtu anaweza nunua Man U kwa ajili ya prestige, ama hata kwa long term business in case huna haraka na faida, ila mtu anaengalia faida ya sasa haimake sense kununua UTD.Hiyo sio investment strategy ya kila mtu.
Kuna watu wanapigana vikumbo wanunue formula 1 teams ili tu iwe prestige kwao na hauzi kirahisi ili apate hela. Na unajua hizo formula 1 teams zinavyokula hela kila msimu.
So, sio kila investor anaenunua timu ya michezo ni kwa ajili ya fedha (capital growth or dividend). Roman Abramovich aliinunua Chelsea just for prestige mpaka alipolazimishwa kuiuza na hakua na mpango wa kuiuza.
Wamarekani mara nyingi wanaangalia faida ndo maana watu hawawapendi. Angalia Liverpool, Man Utd au Arsenal. Timu zimeyumba kwasababu hakuna significant investment wanaiweka baada ya kununua timu. Wao wanasubiria dividends tu.
Man Utd ya sasa ni dhahabu kwenye tope. Inunue Man Utd, jenga uwanja wa kisasa, weka facilities zinazohotajika, weka watu wa mpira wa kufanya maamuzi sahihi. Ndani ya misimu 10 thamani ina double.
kitu gani Exactly kisichojulikana? Bilioni moja pound iliotoka UTD kwenda Bank? dividends wanazochukua kina Glazzer? deni ambalo halilipwi mwaka wa 15? haya mambo mkuu yanaongelewa kila siku, yamejaa vyombo vyote vya habari wala sio siri.Boss, kumbuka tunaongelea first world country hapa. Acha hizi story za shithole countries.
Kwa miaka waliyokaa Glazers na underground movements dhidi ya Glazers, ingekuwa hivyo, ingejulikana mapema sana. Kuna Mancunians wapo pale kazi yao ni kufuatilia kila step ya Glazers; wangeyaona hayo mapema mno.
Pili, financial integrity kwa nchi za dunia ya kwanza ni kubwa mno kwa hilo kutojulikana.
tatizo nyie mnaongea ushabiki. ni simple math mimi nakupa 7B iwekeze, una option ya kununuaBoss, pengine hauko informed sana juu ya hili.
Ebu angalia hapa: The World’s Most Valuable Soccer Teams 2022: Real Madrid, Worth $5.1 Billion, Is Back On Top
4.6B vs. 4.25B; halafu angalia operating income. Hapo kumbuka United hana kikombe wala mafanikio makubwa sana uwanjani kwa karibu miaka 10 sasa. Shitty pamoja na mafanikio yao, bado wanalag behind kwa thamani, na operating income yao siyo kubwa kihivyo kuzidi United.
Haya yanasema kitu tofauti na ulichokisema hapo.
Nothing illegal hapo mzee! Hii ni kutokana tu na a bad ownership deal na ujanja wa kibiashara wa Glazers.kitu gani Exactly kisichojulikana? Bilioni moja pound iliotoka UTD kwenda Bank? dividends wanazochukua kina Glazzer? deni ambalo halilipwi mwaka wa 15? haya mambo mkuu yanaongelewa kila siku, yamejaa vyombo vyote vya habari wala sio siri.
Unatanua goli sasa. Umeambiwa hayo mawazo yako ni ya mfanyabiashara asiye na pesa.tatizo nyie mnaongea ushabiki. ni simple math mimi nakupa 7B iwekeze, una option ya kununua
1. uinunue Man U pekee
2. ununue timu ndogo 22 kwa 300m
baada ya miaka 10 biashara ipi itakupa return zaidi? na kwa nini?
Alieinunua Man City au PSG unadhani wakiiuza leo wataziuza kwa kiasi gani?tatizo nyie mnaongea ushabiki. ni simple math mimi nakupa 7B iwekeze, una option ya kununua
1. uinunue Man U pekee
2. ununue timu ndogo 22 kwa 300m
baada ya miaka 10 biashara ipi itakupa return zaidi? na kwa nini?
Nahitaji waarabuManchester United ipo Sokoni
Baada ya miaka 17 ya umiliki wa Glazers family, iliyokumbwa na mikiki ya kukataliwa na mashabiki, sasa rasmi wameamua kuiweka klabu ya Man Utd Sokoni. Hili limetangazwa tarehe 22/11/2022.
Katika "statement" iliyotolewa na Bodi ya Man Utd na baadaye ikathibitishwa na Avram Glazer, wamiliki wa Man United wameamua kuweka milango wazi kwa wawekezaji wapya kuja kuwekeza (Glazers wakiendelea kuwa wamiliki) au kuiuza (kupata mmiliki mpya) au kuruhusu biashara katika klabu ili kuongeza pato la uwekezaji. Hata hivyo, inatajwa chaguo la kuinunua/kuiuza ndio chaguo lenye nguvu zaidi.
Kwanini Glazers wameamua kuiuza Manchester United?
1. Muendelezo wa mashabiki wa Man Utd kuwakataa Glazers kuwa wamiliki kwa miaka yote 17 ya umiliki wao
2. Glazers kukosa fedha za kuirudisha klabu kuwa klabu tishio kama ilivyokuwa miaka ya nyuma
3. Glazers kukosa fedha za kuisasisha miundombinu ya uwanja wa Old Trafford na Carrington kuwa ya kisasa kama vilabu vingine vinavyofanya (Man City, Real Madrid wameboresha Sana miundombinu yao hivi karibuni)
4. Mgogoro wa kiuchumi duniani kumewanyima Glazers family fursa ya kupata mikopo yenye masharti nafuu kwa ajili ya kuwekeza Manchester United
5. Anguko la Super League ambapo limesababisha uhusiano wa Glazers family na mashabiki kuzorota zaidi na pia umeinyima familia hiyo fursa ya mapato makubwa kutoka Super League.
Man Utd inauzwa bei gani?
Inatajwa kuwa Glazers wapo tayari kukabidhi timu kwa mtu/kampuni ambayo ipo tayari kulipa kiasi cha kati ya paundi bilioni 5 - 9. Hii itaifanya Man Utd kuwa klabu ya michezo ghali zaidi duniani, klabu inayoshika rekodi ni Denver Broncos klabu ya American Football (sio soka) iliyouzwa kwa paundi bilioni 3.9. Tusisahau Chelsea imeuzwa hivi karibuni kwa poundi bilioni 2.5 na Liverpool ipo sokoni kwa gharama ya paundi bilioni 2.7.
Je Mahojiano ya Ronaldo ndio yamesababisha Glazers kuamua kuiuza Man Utd?
HAPANA. Maamuzi ya familia kuhusu kuiuza Yanga yamefanyika kabla ya mahojiano ya Piers Morgan na Cr7. Taarifa ya kuiuza Man Utd ilitoka masaa 4 baada ya Cr7 kufanya mahojiano yale. Haiwezekani ndani ya masaa 4, familia ikae, kisha bodi ikae halafu watangaze maamuzi ya kuiuza klabu.
Lini Man Utakuwa imeshauzwa?
Haiwezi kuwa kabla ya Januari na kama kila kitu kitakuwa sawa bila complications zozote, zoezi hilo litakamilika kabla msimu huu kuisha (May/June 2023). Kutazama time frame ya ununuzi wa Chelsea inaweza kukupa picha ya lini Man Utd itakuwa imeshauzwa.
Nani Wanaotajwa kuwa Wanaimendea Man Utd?
Matajiri wengi wanatajwa, kati yao ni: -
1. Sir Jim Ratcliffe, mfanyabiashara tajiri zaidi Uingereza ambaye pia ni shabiki wa Man Utd. Thamani ya utajiri wake inatajwa kuwa ni paundi bilioni 10.9
2. Matajiri wa mafuta kutoka Saudi Arabia na Dubai
3. Wawekezaji kutoka Mamarekani
4. Amancio Ortega tajiri namba 19 duniani, tajiri wa Kampuni ya Zara Fashion mwenye utajiri wa thamani ya dola za kimarekani bilioni 61.3
5. Apple kampuni kubwa zaidi ya kiteknolojia yenye thamani ya paundi bilioni 2000
6. Wengine
Je Glazers wanaiuza klabu kwa Hasara?
LA HASHA. Miaka 17 Glazer Snr alinunua Manchester United kwa paundi milioni 790, milioni 600 kati ya hizo walikopa na baada ya kuinunua mkopo ukahamishiwa kwenye klabu ya Manchester United. Endapo wataiuza klabu kwa paundi bilioni 5, watakuwa wametengeneza faida ya zaidi ya asilimia 600, tena kwa hela ya mkopo ambao kwa sasa ni klabu ndio inadaiwa.
Mashabiki United wanasemaje?
Mashabiki walio wengi wanatamani klabu ya Manchester United ibadili mmiliki ambaye ataimarisha miundombinu ya klabu na kusajili wachezaji watakaoirudisha klabu katika enzi za ufalme wake
Bila kujali ni Wamarekani, Wasaudia, Wadubai, Wachina, Wahindi au Waingereza... Mashabiki wengi wanataka mmiliki mpya mwenye pochi nene ya kuiletea mapinduzi makubwa klabu ya Manchester United.
Sent from my M2004J19C using JamiiForums mobile app
According to Forbes value ya City ni £3.4B na Psg ni €3B. Zilinunuliwa kama Timu ndogo hivyo wakiuza watapata faida kubwa.Alieinunua Man City au PSG unadhani wakiiuza leo wataziuza kwa kiasi gani?