Manchester United (Red Devils) | Special Thread

We na Ronaldo wako unaboa sasa, mtu yupo kwenye kikosi na kaingizwa kipindi cha pili wakati timu ishafungwa goli mbili bila na bado unalaumu kwnn kaingia ulitaka asiingie ili awe analipwa mshahara wa bure? Punguza bias basi, kuna mda uwe rational bhn.
 
Maake hapo kwanza ncheke [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kama umenisoma vizuri,nimemlaumu kwakuwa inaonekana chaguo lake ni Frankie pekee na anaonekana hana plan B kama akimkosa Frankie.

Hayo matatizo mengine yanafahamika ni ya timu nzima.
Plan B ni Eriksen na ameshafika. Na kocha hawezi kuwa na pendekezo la mchezaji mmoja bodi ya United iliwachukua miezi minne kumsajili Harry Maguire, ikawachukua miezi mitatu kumsajili Wan Bissaka.

Kwa hatua tuliyoifikia kwa sasa kama timu ni wazi kwamba tatizo letu siyo ubora wa makocha tena.

Hata Ole alikuwa kocha mzuri tu ila hakuwa na watu sahihi wa kufundisha.
 
Duh unaota wewe mdada
 
Hata kama tunahitaji kusajili ila mchezo wa jana tangu line up inatoka nliwaambia wadau kwenye group whatsapp kwamba kocha kashaua team balance ni ngumu sana kutoboa

Kulikua na haja gani ya kumuanzisha bruno kama winga? Kwanza hana sifa za winga,pili kiwango chake kiko chini


Poor team selection imetucost sana jana

Nimepoteza imani na Ten haag kabisa
 
Man u shida yao kuu hawasajili wachezaji sahihi
 
Nafasi ya bruno angecheza nani?
 
Team yetu ina matatizo makubwa bado ila kocha nae awe makini ingekuwa busara angemsikiliza Ralf kuhusu hii team bahati nzuri hakutaka kufanya naye kazi

Kitendo cha kumpick Maguire kama nahodha mkuu wa team nalo ni mojawapo ya kosa na kuendelea kuamini kina McFred na Rashford kwamba watatupa matokeo bado ni makosa

Kuna kauli katika mahojiano yake kautumia kama mara 2 kwamba kikosi hiki hiki ndicho kilichoshika nafasi ya 2 chini ya Ole na kina wachezaji potential hapa nikaona kabisa kocha anataka kuonesha kwamba yeye ana mbinu zaidi kuliko watangulizi wake

Tukubali tu kuwa kuna wachezaji hawastaili tena kuchezea Man Utd au wanatakiwa kuwa watu wa benchi, leo mchezaji kama Rashford ni mchezaji wa kutumainiwa kwetu ,Scott McTominay team ya taifa anacheza centre back hivi makocha hawajiulizi kuhusu ubora wake

Kocha kama anataka rebuild ya kweli kama atashindwa kusajili bora hata tutumie wachezaji wa academy kuliko kuendelea na wachezaji waliotufelisha kwa misimu karibu minne
 
Aaa! bhana huo ni ushabiki mandazi, we game mmoja tu hauna imani na kocha?πŸ˜‚πŸ˜ƒ.
Hama timu njoo chelseaπŸ˜…
 
McTominay mchezaji ambaye hapati namba kwenye kiungo cha Scotland leo hii unampanga at the middle of the park of Manchester United team kwenye EPL..hatupo serious kabisa.

Naskia saivi tunamtaka Mark Arnatovic..naskia kashafanya kazi na EtH huko Udachi..naona tunaenda kuwa Ten Hag affiliates FC..

Wenzetu wanasajili kina Haaland,Nunez,na kina Alvarez sisi tunapambana na kizee kilichotoka kucheza ligi ya Uchina..si ni Ighalo tu in the making hapa?

EtH,Arnold na Mortough wanafeli sana.
 
Naamini man utd ingekuwa bongo tayati ingeshasusiwa na mashabiki...Mimi binafsi nampa mechi kumi ETH za kuona mabadiliko kidogo, nataka kuona tu spirit fulani Kama timu nyingine tu.
 
Utd fans Ni sikio la kufa!
Tulishaambiwa ni Ni re-building,,, sio process ya siku moja au mwaka mmoja,,,,

Mnataka timu nzima isajiliwe kwenye window moja ? Ni Kitu ambacho hakiwezekani, hata kidogo ,,, ! It will take time,,,

Au mnataka tuchukue EPL na combination ya macFred? [emoji23], !!!!

Wenzetu wako too professional kwenye kuendesha timu zao,sio Kama sisi huku Africa tunaendesha na mihemuko, kukomoana na siasa ! mfano kila window lazima wanaangalia outgoings na incomings, ili kubalance madaftari yao kibiashara na kuepuka rungu la FFP,,,, !!

EtH apewe muda, naamini board itamsapoti, ndani ya misimu walau miwili ndio tuje hapa tupime uwezo wake,,,,!!! Kuna kitu anakiongea Sana hatumuelewi(right player), alafu enzi za punic buying za Woodward zilishapita,,,, ! (rejea kina falcao, dimaria, rojo ,blind , n.k, mikataba minono , hamna wanacho-deliver)


Pep alipokuja city pamoja na wahuni wale wa kiarabu kumwaga hela atakavyo lakini ilimchukua zaidi ya msimu mmoja kuijenga city tunayoiona Sasa hivi,,, ,,

Vile vile klop alikuta magarasa kibao akayasafisha na kusajili karbia misimu minne, ndio liver tunayoiona Leo kila msimu wanagombania kombe,, !!!!

Utd sasa baada ya mechi moja kila mtu anaongea yake,,, serious tunataka kuchukua epl au [emoji23][emoji23][emoji23], !! EtH sio kocha mmbaya, tumpe muda, tukubali kebehi, maumivu na masimango ya kila namna kutoka kwa majirani zetu ,,, !!

Thought on other teams,,, ??
City untouchable

Liver wako Good, mid yao tia maji tia maji waombe Sana wachezaji wao wawe fit na consistent!

Arsenal ni Ile ile miaka nenda rudi

Chelsea wakikaza wanaweza kuingia top four

Spurs,,,dah Conte tunamchukulia poa ila this time anaweza kutupa lesson!

Trust the process,,, Glory Glory Utd
 
Yani siku kadhaa tu hapa tunaongelea kumpa kocha muda, ila timu imefungwa mechi 1 tayari watu wamegeuka, panic kila sehemu.

Japo tumefungwa jana ila kuna positive nyingi tu za kutupa moyo, Eriksen jana hasa kipindi cha pili alivyodrop deep pengine anaweza kum convice ETH anunue DM kupair naye tuondokane na MCfred.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…