Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Ronaldo auzwe tu hizi sasa ni dharau kwa wachezaji wenzake, mashabiki na timu kwa ujumla. Sababu ipi ya msingi imemfanya aondoke uwanjani kabla mechi haijaisha?
Screenshot_20220731-200247_Samsung%20Internet.jpg
 
Ronaldo auzwe tu hizi sasa ni dharau kwa wachezaji wenzake, mashabiki na timu kwa ujumla. Sababu ipi ya msingi imemfanya aondoke uwanjani kabla mechi haijaisha?View attachment 2310262
Hapo anwafundisha nn vijana huyu ndo anatuharibia team ,watu waliokuwa wanampinga walikuwa na sababu muhimu sana.

Kwa sasa aende tu ukizingatia hakuna alichobadilisha katika team ,hana mapenzi tena na club japokuwa mashabiki wanampenda
 
Hawa ndio mashabiki wa Man utd wasio hata na chembe ya uvumilivu.

Hao Liverpool wanaooneka wazuri hawakujengwa kwa msimu mmoja pekee,kulikua na wachezaji kibao vimeo wakina sturidge,moreno n.k wakaanza kuchujwa mmoja mmoja mpaka ukatengenezwa mfumo ambao kila mchezaji akija anafit.

Na bado mashabiki wa Liva wakavumilia japo hawakuchukua ubingwa wa epl miaka 30,leo hii wanakula matunda.

Hapa tuna mwezi mmoja tu na Ten Hag ,ten pre season watu tunatoa mapooovu,tunataka kufanya ujinga ule ule wa kunnunua tu bila kutengeneza mfumo.

Bado tuna safari angalau misimu miwili tuwe vizuri,tuvute subira tusijaribu kujifananisha.

Trust the process.
 
Atahitaji kufanya squad overhaul ili aweze kutengeneza timu imara anatakiwa kuachana na David De Gea.

Afumue safu ya ulinzi yote na afumue midfield yote.

Anatakiwa kutengeneza attacking trio nyingine ambayo iko serious na makombe.

Ana wachezaji wazembe sana ambao kwa modern football ni kama hawana cha kumpa.

Lakini inaonekana bodi ya Man united haiko serious na usajili katika timu yao ni kama wanajaribu kubahatisha bahatisha.

Kikosi alichonacho hakitaweza kupambana mpaka katikati ya ligi.

Ole aliokolewa na Bruno Fernandez angefukuzwa kabla ya 2021.

Je tutegemee nani mwingine wa kumuokoa Ten Hag.

Degea amekuwa consistent sana kufanya makosa kiasi kwamba anaigharimu timu kwenye hatua nyingi nyingi sana.

United kama wataingia top four msimu huu siyo kwa ubora wao ila kwa sababu timu nyingine tu hazitakuwa bora.

Angalia Arsenal msimu uliopita alifanya vizuri kuliko sisi lakini usajili amefanya mzuri kuliko sisi tena kwa kuziba maeneo muhimu waliyoonekana kupwaya.

United wanahitaji wachezaji watano muhimu kikosini kwao lakini msimu huu hakuna hata mmoja muhimu aliyesajiliwa ni kama wamesajili squad players .
Inaonekana wewe jamaa unaujua mpira vizuri sana

Uwe unatembelea kule jukwaa la gunner. Karibu sana pande zile mkuu
 
Back
Top Bottom