Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Kaka tusubrie....ERA COMES TO AN END hii ni kauli ya 10hag kwa city na liver na lzm itatimia
United is back, ETH atatufikisha tena mpm kweny mafanikio
Roma haikujengw kwa cku moja...hata izo Liverpool na city zili delay kabla ya kuwa kwenye form hii ya sasa
 
Kitoabu, Daemusin, Chief Mkwawa, Bavaria

Nje kidogo ya nyumba yetu, hivi ni kitu gani kinaendelea Chelsea? Mbona wachezaji wengi hawaendi? Na ofa zao huwa zinakuwa nzuri kuliko hata wapinzani wao. (Raphinha na Jules Kounde)

Jules Kounde anaenda Barcelona kwa Pound 46M na mshahara wa euro 7M kwa mwaka hapo hapo ofa ya Chelsea ilikuwa pound 55M na mshahara wa euro 12M kwa mwaka. Naomba nipewe ufafanunuzi kidogo hapa nini kinaendelea?
1. Barca ni brand kubwa kushinda Chelsea.

2. Barca na Madrid ni club za mataji, ni rahisi kushinda kombe la ligi ukiwa Barca au Madrid kuliko ukiwa Chelsea. Ni kutokana na EPL kuwa na timu nyingi zinazokaribiana uwezo na kuongeza ugumu katika ukusanyaji points.

3. Kucheza Barca una nafasi kubwa ya kushiriki UCL kila msimu kwasababu ya uhakika wa kumaliza ndani ya top 4. EPL huo uhakika haupo ukiwatoa City na Liverpool.

4. Kuna nafasi kubwa kushinda taji la UCL kutokana na ushiriki wa mara kwa mara inayoongeza uzoefu katika kikosi.

5. Project ya Barca chini ya Xavi inaeleweka.

6. Chelsea ni kama ndiyo wanaanza kuchochea moto uliozima, Barca moto ushaanza kuwaka ni kuongeza tu mkaa uwake vizuri.

Ukitoa pesa hizo ni mojawapo ya sababu zinawafanya wachezaji waende Barca badala ya Chelsea.
 
FYsCmOXWYAE3l5w.jpeg
 
Kitoabu, Daemusin, Chief Mkwawa, Bavaria

Nje kidogo ya nyumba yetu, hivi ni kitu gani kinaendelea Chelsea? Mbona wachezaji wengi hawaendi? Na ofa zao huwa zinakuwa nzuri kuliko hata wapinzani wao. (Raphinha na Jules Kounde)

Jules Kounde anaenda Barcelona kwa Pound 46M na mshahara wa euro 7M kwa mwaka hapo hapo ofa ya Chelsea ilikuwa pound 55M na mshahara wa euro 12M kwa mwaka. Naomba nipewe ufafanunuzi kidogo hapa nini kinaendelea?
Most of players bado wanaamini Chelsea Ni klabu ndogo TU,
 
Sure, anazingua.
Huyu fala pamoja na kumtetea sana humu ila safari hii ameamua kutuvua nguo kabisa hadharani, hichi anachotuonyesha ni ubinfsi wa hali ya juu sana.
Alivyo na akili mbovu timu karibia zote hazimtaki halafu yeye anaamua kunyea kambi.
Binafsi nimeanza kumchukia na hata akiamua kubaki sidhani kama atapata sapoti kubwa kutoka kwa mashabiki.
 
Timu yetu haiko serious tu tusubiri msimu basi. Hizo sajili 2 hazitufikishi popote hata de jong akija atacheza msimu mzima?? Siku akiumia miezi miwili tunarudi na kina macfred hehehe okay tulihitaji watu wapya hata watano au 6 kuanza kua serious na ligi. Tunashangilia mechi za pre season sijui wacha tuonee.
Timu inapoingia kwenye project mpya hutakiwi kuwa na matarajio ya ubingwa.

Matarajio yangu mimi timu icheze kwa muunganiko mzuri na iwe na matokeo chanya tu.

Ubingwa utakuja tu tutakapokuwa na matokeo consistent hata kwa mechi 20 mfululizo.
 
Back
Top Bottom