Sikazi fuvu ila ukweli ndo huo mkuu, hakuna msimu hata mmoja ambayo mliwahi kukaa na kuevaluate mapungufu ya team kwa ujumla, badala yake ni mabingwa kupoint mchezaji mmoja mmoja na kumuona kama aliyefelisha team nzima.
Huko nyuma mmewahi kuwalaumu akina de gea, Lukaku, Pogba, Bissaka, Tominay, Maguire,Fred, OLE baada ya hapo mkahamia kwa waingereze na sasa ni Ronaldo.
Sasa kama kikosi chote mmewahi kukilalamikia kwanini usikubali kuwa tuna wachezaji avarage, na kwamba hiyo ndio sababu ya kufeli kwetu sikuzote?
Mpaka sasa hata tukimtoa Ronaldo, bado hakuna uhakika wa kutoboa top four wala kuchukua kombe lolote.
TUKUBALI TU KUWA TUNA TEAM AVARAGE NA TUANZE KUJIJENGA UPYA.