Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Huu Utakuwa Usajili Mzuri, Yeye Wing Ya Kulia Sancho Wing Ya Kushoto
hiyo taarifa ya anthony imeandikwa na waandishi wa habari wa brazil pekee, inaweza kuwa ni sahihi au ni uzushi wa mawakala kuitumia brand ya manchester united kwa lengo la kutengeneza mazingira ya kupata mikataba mikubwa kwa wateja wao
 
Klop alivyo mbahili vile, akitoa tu £40m huyo mchezaji anakua hatari, ukiona kakubal kutoa zaid kwa Nunez usitegemee kuflop
anaweza kuendeleza moto wake wa kufunga magoli kwa msimu mwengine au pia ikawa kinyume chake. tufahamu darwin nunez ni msimu huu tu amekuwa bora. pia unadeal na benfica. wazee wa kuuza wachezaji wanaotrend kwa bei kubwa kama walivyofanya kwa joao felix.
 
Klop alivyo mbahili vile, akitoa tu £40m huyo mchezaji anakua hatari, ukiona kakubal kutoa zaid kwa Nunez usitegemee kuflop
mbahili hawezi kulipa pound million 60 au zaidi kwa ajili ya goalkeeper, liverpool wanajiandaa na maisha ya baadae kutokana na sintofahamu ya mkataba wa salah unaomalizika msimu ujao pamoja na sadio mane. bila ya shaka ameona ugumu wa kupata winga mwengine aina ya salah mwenye uwezo wa kuhusika na magoli 30 au zaidi ndio ameamua kurudisha mfumo wa kutumia striker. kama liverpool wangelikuwa na nafasi ya kumsajili kylian mbappe kuziba nafasi ya salah wasingelisita kufanya hivyo.
 
mashabiki na wapenzi wa manchester united tunaandamwa na khofu, woga wa kuendelea kubaki chini, presha ya kutaka kurudi tena juu bila ya kujali njia ya kutufikisha huko. tumekuwa kama wasafiri waliovurugwa na dhoruba ya bahari. Nimeanza kuyaelewa na kupambana nayo mfano wa maumivu na frustrations waliyopitia mashabiki wa timu nyengine wakati huo sisi tunakula bata. Tumevurugwaaa!!!!
 
laurie whitwell anasema hiyo taarifa ya jorge mendez kukutana na erik ten hag kwa dhumuni la kujadili usajili wa darwin nunez ni bogus, kwa maana ni feki
Huwa Mkuu nafurahi sana Tier 1 kama hawa wakiclarify mambo.

Pia Amesema De jong yupo Open Kujiunga Man U, tofauti na Rumors za mwanzo kwamba hataki kuja kwetu.

Kwa usalama wa Afya ya akili yako vyema ukaepuka kabisa hivi ijumaa na uwazi za ulaya.
 
Ngoja nitoe mfano huu kwa dhumuni la kujadili swala la frankie de jong: Jaalia manchester united ni boti, dau, jahazi au meli. Wakati huo huo erik ten hag (kocha) ndiye nahodha wa hicho chombo. Frankie de jong ndiye atakayekuwa ramani au compass ya kumuongoza nahodha na hiyo boti pindi itakapokuwa safarini (uwanjani). Erik ten hag ameshafanya kazi na frankie de jong hivyo basi hata kama atamsajili siku mbili kabla ya kuanza kwa ligi itakuwa ni rahisi kwa frankie kuadapt mazingira ya kiuchezaji ya kocha ten hag kuliko mchezaji mwengine na changamoto kubwa atakayoipata ni match fitness. Erik ten hag anataka kujenga timu yake kiuchezaji ndani ya uwanja kupitia frankie de jong, kwa lugha nyepesi frank ndiye kampasi au ramani tukiwa na mpira na tusipokuwa na mpira. Frankie atahusika na buildup kwa maana atakuwa wa kwanza kupokea mipira kutoka kwa mabeki, jukumu hili kwa sasa halifanyi vyema pale barcelona kwa sababu position yake anacheza sergio bosquet. Tumuelewe erik ten hag, kama atashindwa kumpata frankie ndio tunamuandalia mazingira ya kufeli kwake.
 
Huwa Mkuu nafurahi sana Tier 1 kama hawa wakiclarify mambo.

Pia Amesema De jong yupo Open Kujiunga Man U, tofauti na Rumors za mwanzo kwamba hataki kuja kwetu.

Kwa usalama wa Afya ya akili yako vyema ukaepuka kabisa hivi ijumaa na uwazi za ulaya.
umenisaidia sana kuvifahamu vyanzo vya taarifa vyenye uafadhali na rubbish, uzuri pia ukitembelea subreddit za timu wanakuwekea list ya chanzo sahihi na takataka. Vijarida uchwara sivifuatilii
 
anaweza kuendeleza moto wake wa kufunga magoli kwa msimu mwengine au pia ikawa kinyume chake. tufahamu darwin nunez ni msimu huu tu amekuwa bora. pia unadeal na benfica. wazee wa kuuza wachezaji wanaotrend kwa bei kubwa kama walivyofanya kwa joao felix.
Hapo yanatengenezwa mazingira tupigwe tena kama kawaida, wacha aende Liverpool haina shida kuliko kutoa mapesa yote hayo kwa mchezaji aliyewika msimu mmoja alafu anatokea timu ndogo, huo ni upuuzi.
 
Back
Top Bottom