Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Nimeandika kadri ninavyoweza.

Bahati mbaya haujanielewa.
 
 
 
YouTube › watch
Shabiki wa Man U Ajiua kwa Kujirusha Kutoka Orofani - YouTube
 
Binafsi naona man u ikikosa michuano ya Europa/Conference atakua position nzuri sana ya kurudi kuliko kulazimisha kuwepo

Kwa mchezaji mmoja mmoja ni kwel man u amewaacha arsenal, spurs, Chelsea mbali kidogo
Swali linakuja tatizo ni nini sasa?

Unaweza ukasema tatizo ni makocha wanaofika pale ikiwa tu hautakua na mtazamo mkubwa
Tatizo kuu la man u ni wachezaji
Wachezaji wamekua na sauti kuliko kocha
Wachezaji wanaamua kugoma bila sababu za msingi ili kocha atimuliwe.
Rashford, pogba, Bruno, degea, ........ Elanga
Hao wote wameshakua virus

Nini kifanyike,
Wanaomaliza mikataba wasiongezwe makataba, wanaobaki piga bei ata ya hasara sio mbaya
Kwa mfano lingard ukampush kwa 20 au 15 utakua umekosa nini!!! Bisaka peleka pori lolote kwa mkopo. Hii yote n kuondoa vizur
Ili vijana wataokuja wasiambukizwe ujinga wa kina rashfod, magwaya, Fred, cr7,....

Timu isukwe upya for long term plan
Kuwe na wage structure nzuri
Strictly laws and policies
Lengend wapunguze mdomo, waache watu wafanye kazi.

Mkiona mnaingia kwa msmu mpya wa ligi hamjauza/fukuza/kuacha wachezaji zaidi ya 8. Mjue kabisa hakuna jipya
Brighton watapiga tena 4, Liverpool, man city wataokota points 6
Arsenal atawapiga cap nje ndani

Niwatakie majonzi mema, sitaacha kupita hapa
 
Watu awaelewi wanachukulia mupira seriyaz ndio maana majitu hapa ukiyatania tu kidogo mzee yanaporomosha matusi adi shety( shetani) anaomba poo ..hahaha usipokubali kutaniwa ..Basi mtu kaa Mimi ndio naongezaga mautani adi zile asira za kuweka mguu mfukoni au kumeza wembe zinakushika hahahaha na Mimi nasema hiiiiii😂😂😂😂
 
Mkuu mpira ni burudani mpaka kufungwa kuna burudani yake hivi mashabiki kama wa Bayern munich ambayo msimu wa 10 huu wanabeba ligi wakiambiwa ligi yao ni urojo unadhani wanakuwa wanajisikiaje.

Raha ya mpira inatakiwa kuna kipindi kama ichi kije hili baadae timu itapoanza kufanya vizuri hata mzuka nao unakuwa mkubwa. wakuishangilia timu yako.

Kwangu naona raha ya mpira ni pamoja na kupoteza hili wakina OllaChuga Oc Pain killer wanavyo kuja kutania tania hapa ndo burudani ya mpira iyo.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] AsaniAli eti wako serious wanataka kukuchomoa hapo nafasi ya 3.
Ila nyie ni kenge kweli yaani li timu lenu limekubali kuvalishwa jezi iliyoandikwa kabisa namba 3, hio ni lugha ya picha inayomaanisha msimu huu mtaishia nafasi ya 3 kenge nyie[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kuna uwezekano Haaland akaja United. Hata binafsi nakubaliana na hilo.

Ni natural goal getter. Akikupa goli 30 kwa msimu na Ronaldo akikupa nae 25.

Mnakuwa kwenye nafasi nzuri.
Darwin Nunez ni cheap option ya Haaland. Bei zao wote ni Euro 75M ila mshahara wa Darwin ni nusu wa Haaland maana yake anatoa room ya ku-accommodate mchezaji mwingine kikosini. (Haaland si chini ya 350k/weekly vs Darwin Nunez 175k/weekly)

Kwa kifupi Haaland hafai kwa timu inayotaka kujengwa kila idara yeye pekee yake anaturudisha kule kule kujaza wachezaji wenye mishahara mikubwa kwa wakati mmoja. Hii kitu ni hatari kama unajenga timu inaku-limit kuongeza watu.
 
Sifa ya kwanza ya kiungo ni kuwa na akili..I'm sorry to say McSouce akili hiyo hana.
mgogoro wa mourinho dhidi ya paul pogba ndio ulimfaidisha scott mctominay, jose alimpandisha kutoka academy. uwezo wa mctominay ni wa kuchezea vilabu kama burnley na si kuwa regular starter wa manchester united. Tumerudi nyuma sana.
 
bora hata wewe unakimbilia jukwaa la mapishi ukifungwa
 
Ndio naona hapa muda sio mrefu kutoka kwa Fabrizio kumbe majirani zetu tayari wamemalizana na 'Lukaku' mpya?
ile taarifa nilifanikiwa kuisoma asubuhi kutoka kwa mtaalamu david ornstein, nafikiri yeye ndiye muandishi wa mwanzoni kuripoti taarifa hiyo. Kwa nini awe erling haaland na si harry kane?. Any tips.
 
Mpira ni mchezo wa hisia unapotoka kufungwa kwa dakika kadhaa nyongo inakuwa imechafuka mtu akileta utani ni kama anaweka chumvi ktk kidonda sasa hapo tuna tofautiana jinsi ya ku-handle hizo reactions. Kadri unavyozidi kuwa mtu mzima hisia za maumivu hupungua (above 25 yrs old).

Binafsi nimeanza kuangalia mechi za United toka mwaka 1999 May, 26 mpaka sasa labda nimekosa michezo isiyozidi 30. Unaweza kujionea hapo nimepitia vipigo vingapi ndani ya miaka karibu 23. Nishawahi kunyata kurudi chumbani kwangu nilipokuwa chuo kikuu baada ya kufungwa na Barcelona fainali.

Michango ya watu waliokomaa hata timu ikifungwa hujikita ktk mchezo zaidi ni wapi palikuwa na mapungufu na nani kazingua na nini kifanyike ila watoto wadogo wengi labda hata wewe pia ni mmoja wao hujikita zaidi ktk mizaha ila mimi huchukulia kawaida najua wapo ktk kipindi cha umri sahihi kufanya hayo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…