Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Wazee Moyes anajipigia tu, tatizo siyo wachezaji kabisa ni kochaaaa.

Kama United wapo serious kweli wamlete Ralf Rangnick huyu ndiyo kichwa cha wanayofanya makocha kama Klopp na Tuchel. Kwa style yake na aina ya wachezaji (mapafu ya mbwa) anaowahitaji wapo apewe timu naona tetesi nyingi ni kwa kocha wa Leicester, hapo United wanapotea kwa mara nyingine tena.
Brandon Rojas ni kuku kishingo (Mwana Liverpool) hawezi kuja United.
 
Najua hilo halitakuja kutokea, lakini likitokea tutakua tunaendelea kutest mitambo tu.

Brandon ni wakawaida sana, achilia mbali ulivapuli wake.
Brendan sio mlivapuli Mzee ..kabla ya kwenda Liverpool alitoka Chelsea kama kocha wa academy ...so sio kwamba n mwana Liverpool halisi km kina dalgish
 
Naamini hivyo pia ....sema naona wanahangaika na succession plan .....wanawaza nani wampe timu pia wanavizia kupata kocha wa moja kwa moja na nafikiri kocha wanaemtaka yupo na timu

Ten hag. Poch na the others
Erik Ten Hag ni mzuri ila ufanisi wake upo nyuma ya Edwin Van Der Sar (Football Executive) na Marc Overmas (Director of football) ukimchukua pekee yake kwa mfumo wa timu yetu namuona akifeli vibaya sana ndani ya muda mfupi sana.

Huu ni wakati sahihi sana wa ile nafasi ya Ed kupewa mtu mwenye uzoefu wa kuendesha vilabu vyao soka as a football executive. Wasifanye kosa la kuleta kilaza kama Ed, niliwahi kuelezea impact ya kuwa na mtendaji mkuu mwenye kichwa kizuri.

Wamiliki wa Man City waliponunua timu wakamtafuta football executive toka Barcelona Ferran Sorriano kuwaendeshea timu. Mtu wa kwanza kuanza kumuajiri alikuwa ni football director kutoka Barcelona Aitor Txiki Birigistan moja kwa moja wakaanza kusuka upya scouting staffs globally na wengi wao walitoka Barcelona.

Ferran Sorriano aliwaambia mabosi wa City ndani ya miaka 5 ya uongozi wake atabeba makombe 5 na Club itapunguza 50% hasara inazotumia kujiendesha na kweli msimu wake wa kwanza alimuondoa Mancini akamleta Manuel Pellegrini kichwani walifahamu fika wanamtaka Pep Guardiola. Sisi tunakosa hii kitu watu wanaojua nini wanafanya. Ole anacheleweshwa kufukuzwa ni kwa sbb Ed na DoF wake hawana mtu kichwani kwako atayeendelezea project waliyoipanga muda mrefu.

Angalia takwimu za hawa football Executive wawili walioanza kazi pamoja ndani ya hii misimu 9, Ferran Sorriano vs Ed Woodward

Ferran Sorriano (Sept, 2012 - )
Premier League trophies: 4
FA: 1
EFL:4

Ed Woodward (July, 2013 - )
Premier League trophies: 0
FA: 1
EFL:1
UEFA Europa: 1
 
Kuna rafiki yangu mmoja mtaani aliwahi niambia kua timu yetu haiwezi kurudi tena kama zamani mpaka Ferguson afe.

Siku ile nilimuona kama karopoka tu kwakua yeye ni mshika manati.

Ila kwakweli naanza kuamini mdogo mdogo.

Hata uwepo wa Ole mpaka sasa pale OT unatokana na Ferguson, laiti angekua kocha ambae hayupo ndani ya mfuko wa suruali ya Ferguson saizi Ole tulisha msahau tangu tulipo donyolewa na kuku.

Kuku alitufanya kitu mbaya sana.

Kichapo kile kiliidhinisha kabisa kufukuzwa kwa Sorkjaer, lakini kwakua yuko ndani ya mfuko wa suruali ya babu mpaka leo tunaendelea kumuona akitamba.

TATIZO SIO WACHEZAJI, KOCHA, WALA UONGOZI, TATIZO NI ZIDUMU FIKRA ZA FERGUSON.
Hili nakupinga Ferguson hakuwahi kufundisha timu goi goi namna hii.

Huu ugoigoi wa timu yetu ni replica ya attitude ya Ole.

Unaona kabisa timu ile huwa haifanyi tactical training zaidi ya kukimbia kuondoa hangover za mapenzi na bia tu.

Uliona wapi timu ya Ferguson inanyanyaswa kwenye physicality na timu yoyote EPL?

Uliona wapi timu ya Ferguson inacheza hovyo consecutively mechi kumi bila Ferguson kufanya overhaul ya squad.?

Ulishawahi kuona mchezaji chini ya Ferguson anafanya upuuzi halafu Fergi asimkoromee au kutompanga kikosini hata kwa mwezi mzima ?

Kifupi Ole wachezaji wake wanamchukulia kama ROOMMATES na siyo watu wanaotakiwa kutii anavyotaka yeye hiyo ni kwa sababu Ole anawachukulia wachezaji wake kama COLLEAGUES tu badala ya kuwa subordinates wake.

Ole is just a nice boy not a Man.
 
Hii mambo ya international break ndio inayo exacerbate crisis kwa OLE ujue? sio kwamba nawish, lakini intuitive trend analysis yangu inaproject kipigo next mechi, tena hii international break ndio inaongeza odds za kipigo.
Ole atashinda mechi na Watford then atadraw na Arsenal baada hapo atapigwa na Chelsea.

Inasikitisha sana
 
Back
Top Bottom