Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

  1. Dakika 10 za Donny van de beek zimeleta matumaini kuliko dakika nyingi za Paul pogba, Donny anaonewa bila ya sababu.
  2. Back 3 bila ya proper wingback ni kujihashua,Shaw na wan bissaka bado hawatoshi.
  3. Luke shaw amekata moto, huenda zile sifa za kijinga alizokuwa akipewa na waingereza wenzake kwenye michuano ya kombe la euro zilimjaza upepo wa kijinga, eti walikuwa wanamwita shawberto Carlos.
  4. Bila ya winga hatuna makali, si ajabu kipindi cha kwanza tulidhibitiwa vilivyo kwa sababu hatuna uwezo wa kupita katikati, nilifurahi alipoumia mlinzi mmoja(natumai atarudi mapema uwanjani)na kuswitch mfumo.
  5. Wan bissaka ameimprove anapokuwa na mpira lakini bado hatoshi kuwa mchezaji wa Manchester united.
  6. hivi harry Maguire anamzidi mlinzi yupi kati ya wale watatu tulionao, ni lini benchi la ufundi watakisikia kilio cha mashabiki waliowengi duniani wanaokerwa na performance mbovu ya Maguire kila wiki, harry Maguire na Phil Jones ni ndugu wawili wasiojuana kifamilia. Kwani kuna ubaya kwa mwanadamu kukiri makosa yake alioyatenda, mbona ole amekuwa mgumu kumpumzisha huyu jamaa (hata msema ovyo paul scholes ameonyesha kukerwa na kiwango chake duni).Leicester wametubikiri hadharani.
  7. Scott mctominay ni press resistance asiyejitambua, uoga na upumbavu wa maamuzi umemjaa miguuni na kichwani, huenda hana bando la kumuwezesha kuangalia video za Marco verratti, bosquet,kovacic,moussa dembele n.k
  8. Tulishawahi kuifikiria partnership ya Eric Bailly na Raphael varane japo kwa mchana mmoja?.......NEPOTISM ni ugonjwa mbaya sana.
  9. CR7 ni mbuzi wa miongo miwili(g.o.a.t), anatufurahisha na muda huo huo anatukera.
  10. Nimeikumbuka ile thread yenye kichwa cha habari kifuatacho
We are an awfully coached team, jamaa sijui aliwaza nini mwaka mmoja uliopita mpaka akaanzisha thread hii kwenye forum ya redcafe
Ukisikia kusafiri kwa muda ndio mfano wa thread hiyo, wengi tumeanza kumuelewa.

 
eti hangover, kwani wenzake hawakucheza Euro....
Waingereza ni wanafiki kupitiliza,
Nimeanza kumuelewa PTER , tatizo ni Maguire na si lindeloff,
Tulichokuwa tunakifanya ni kumtoa kafara victor lindelof huku tukilinyamazia tatizo kuu.

Paul Scholes: "Harry Maguire... I don’t know if he is injured or has a hangover from the Euros, it just does not look right. He is all over the place." #mulive [bt]
 
Kwa utopolo mnaocheza muda wa Ole kung'ata unakuja....

Kinachinipa amani Conte ashajiendea Totte....

Muda wa kulia unakuja.
 
Alietuaminisha hii timu inawachezaji wazuri sana leo na ina DNA yake ya kucheza kwa kushambulia leo hii....

Anatumia 3_5_2 formation ya kujilinda

hawatumii wachezaji kwakulingana na ubora wao...

tunacheza na wachezaji wakabaji wawili (defensive midfielders) na mabeki 5

sijui tutafika lini
 
Mfumo huu ni mzuri kwa timu ndogo ...

Ila kwa mtu kama mancity ukijifanya uko happy kukaa na mabeki watano kulinda na wao wanaweka mvua ya nyuki wanakuja dkika 90
 
Bado nafikiria wale waliosema ronaldo ni mzigo cjui walimaanisha nini aisee.
walimuona kwenye ile mechi ya Liverpool alivyokua mzgo badala ya kupiga mpira akawa anapiga watu uu kama so mzigo n nn
IMG-20211026-WA0003.jpg
 
Bado nafikiria wale waliosema ronaldo ni mzigo cjui walimaanisha nini aisee.
We nae umekazania ronadooo ronadooo umesimamisha misuli ya shingo hadi mate yanakutoka pembeni ya limdomo.

Muite basi akutolee mahari uwe mke kabisa ili uwe unamsifia vizuri.
 
Bado nafikiria wale waliosema ronaldo ni mzigo cjui walimaanisha nini aisee.
Ronaldo ni mzigo mkubwa kabisa kwenye timu ,hakabi ,hapandi na kushuka ,anataka kutelezeshewa tu mpira .....


Ronaldo out

Ole out

Maguire ni bonge la beki ,ndio nguzo iliyobaki united .,..
 
Ni kama nayaelewa maneno ya Bavaria. Aliwahi kusema Ole anavi-element vya ubaguzi, haiingii akilini wale mabeki wote watatu wakiwa fit eti huyu msenge Maguire ndio anatafutiwa nani wa kucheza nae wakati wote wanamzidi uwezo.

Hata huu mfumo wa kuanzisha mabeki watatu pale nyuma ni namna tu ya kumu-accomodate huyu msenge Harry ila anatugharimu sana. Michezo yote aliyecheza msimu huu ametoa maboko.
Mkuu niliwahi kusemea humu ndani hizi sajili za watoto wa malkia zinatugharimu sana ila nadhani sikueleweka vizuri. Mfano mzuri ni kwenye team selection zinazofanywa na Ole kwa kuangalia utaifa kuliko form ya mchezaji.

Sancho anapigiwa chapuo ya kuanza kuliko wanavyomsemea VdB dhidi ya Mctominnay butu kwa sasa. Fred anapigwa vita kuliko Maguire aliyepoteza mvuto. Wan bisaka on/off kibao lakini hawajibishwi kwa kukaa bench. Telles hajui ni lini atapata namba dhidi ya Luke Shaw ambaye hana form nzuri. Rashy ndio kesi yake naiweka pembeni sababu bado analindwa na msemo kuwa ametoka majeruhi.

Kwa mfumo wa 3-5-2 anaotumia Ole tulitegemea kupata ufanisi mzuri toka kwa Dalot na Telles kama wingbacks lakini watoto wa malkia wamekalia mashavu yote mawili. Una Cavan na CR7 wanadamu wanaojua vizuri sana matumizi ya vichwa vyao kufunga mpira wa krosi lakini una Wanbisaka asiyejua kupiga krosi.
Ni kama nayaelewa maneno ya Bavaria. Aliwahi kusema Ole anavi-element vya ubaguzi, haiingii akilini wale mabeki wote watatu wakiwa fit eti huyu msenge Maguire ndio anatafutiwa nani wa kucheza nae wakati wote wanamzidi uwezo.

Hata huu mfumo wa kuanzisha mabeki watatu pale nyuma ni namna tu ya kumu-accomodate huyu msenge Harry ila anatugharimu sana. Michezo yote aliyecheza msimu huu ametoa maboko.
 
Ni kama nayaelewa maneno ya Bavaria. Aliwahi kusema Ole anavi-element vya ubaguzi, haiingii akilini wale mabeki wote watatu wakiwa fit eti huyu msenge Maguire ndio anatafutiwa nani wa kucheza nae wakati wote wanamzidi uwezo.

Hata huu mfumo wa kuanzisha mabeki watatu pale nyuma ni namna tu ya kumu-accomodate huyu msenge Harry ila anatugharimu sana. Michezo yote aliyecheza msimu huu ametoa maboko.
Yani unaambiwa atafutwe beki wa kucheza na Maguire na sio vinginevyo.

Huyu jamaa ni mweupe sana. Am sure hata Lindelof angecheza na Baily tusingekuwa tunafungwa kizembe sana.

Kutoa 80M kumchukua Maguire ni fraud.
 
Back
Top Bottom