Tutakuja kuongea lugha moja baadae sana. Waingereza sio wachezaji wa kununua wanauzwa ghali mno kuliko uwezo halisi. Wana vipaji kweli ila wanabebeshwa mzigo wa price tag unaokuja na expectations kubwa sana kwa mashabiki kitu ambacho kinawaletea pressure za kufanya vizuri. Tuwe na sera ya kuwapandisha kama Mason Greenwood na Marcus Rashford.
Huwa napinga wazi wazi usajili wa wachezaji kiingereza kwa ssb huwa wanauzwa bei kubwa sana kuliko wachezaji wa mataifa mengine wenye uwezo ule ule au kuwazidi. Hebu jaribu kufikiria muda tuliokuwa tunamtaka Jack Grealish tuliambiwa tulipe Pound 80M wakati huo huo Bruno alikuwa anapatikana kwa Pound 47M tu.
Niliandika pia kuhusu Pedro Goncalves yupo pale Sporting Lisbon ni kijana wa kireno mwenye miaka 23 amewaongoza Sporting Lisbon kubeba kombe la ligi kuu msimu ulioisha Ureno toka mwaka 2002. Na alikuwa mfungaji bora (23 goals) na mchezaji bora wa ligi pia. Huyu anacheza kama winga wa kushoto, kulia na nyuma ya mshambuliaji wa mwisho. Huyu bei yake ni Pound 51.7M. Just imagine angekuwa muingereza, bei yake inge-double.
Msimu huu ulioanza tayari kacheza mechi 4 kafunga goli 3 za ligi kuu ureno kuelekea international break.