Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Hivi ni mimi peke yangu au tuko wengi tunaoshangazwa na upotevu wa AMADI DIALLO aliyesajiliwa kwa mbwembwe pale OT?
Kama sikosei hata kwenye benchi simuoni kabisa. Mwenye taarifa zaidi kuhusu huyu dogo atufahamishe nini kinamsibu
Msimu umeisha mdau tusubirie msimu ujao
 
El Matador
Screenshot_20210510-191014.jpeg
 
Kuna kitu kama umegundua Ole anatumia mbinu ambazo haziendani na aina ya wachezaji alionao kikosini. Mechi nyingi anazifanya zionekane ngumu bila sababu ya msingi.

Kwa aina ya wachezaji tulionao inapaswa tucheze offensively zaidi na sio kujilinda na kushambulia kwa kushtukiza. Tukikaba sana huwa tunashambulika kirahisi sana na tuna ukuta mbovu sana.

Kwa maoni yangu anapaswa awe anamtumia mmoja tu kukaba kati ya Fred au Scott juu namba 8 awe anacheza Paul na juu yake namba 10 shimoni Bruno kama kawaida mwisho Cavani upande mmoja Rashford na mwingine Greewood.
Ni rahisi sana kuandika kuliko kupanga hivyo unavyotaka uwanjani.

Ukifuatilia Attributes za Midfielders wa Man U wote(Matic, Fred, Pogba na McT)
Lazima utaelewa kwann OLE na Jopo lake la Ufundi hawataki kupanga hivyo.

Kingine fuatilia Kipindi ambacho Pogba amekuwa katika kiwango kizuri huwa anacheza sehemu ipi.

Tatu, jiulize kwanini OLE amuamishe Rashford upande wa kushoto, ili kum-accommodate Pogba.




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi ni mimi peke yangu au tuko wengi tunaoshangazwa na upotevu wa AMADI DIALLO aliyesajiliwa kwa mbwembwe pale OT?
Kama sikosei hata kwenye benchi simuoni kabisa. Mwenye taarifa zaidi kuhusu huyu dogo atufahamishe nini kinamsibu
Ulitegemea kabisa Diallo aje aanze kikosi cha kwanza.?

Wakati kule Itally alikuwa hajafikisha hata mechi tano za kikosi cha Kwanza.

Na Dogo ndio kwanza ana miaka 18.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawa waingereza mwisho miaka 25 tu. Huwa wanaanza moto ila usiwaamini kufika mbali. Sina takwimu za kitafiti kutetea hoja yangu ila sababu kubwa nahisi wanakuzwa mno na vyombo vyao vya habari kuliko uwezo wao halisi.

Kuna kipindi (2008 ~ 2012) walikuwa na Tom Cleverley, Jack Wilshere, Daniel Welbeck, Daniel Sturridge, Theo Walcott, Jack Rodwell, n.k na wote hawa walikuwa wamezaliwa mwaka 1989 ~ 1992 sawa sawa na hawa wa sasa waliozaliwa mwaka 1999 ~ 2002. Ila sasa hivi wapo vitimu vidogo hata namba hawana.
Kama watanzania tu
 
Ole Gunnar Solskjaer on Manchester United's four matches in eight days: "I run too much of a risk of injuring [the players], so talking about integrity in the league and stuff, don't blame me when I have to make changes because I have to"; United host Leicester on Tuesday night
 
Back
Top Bottom