Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Aisee Chief, hauoni kuwa hapo umei-downgrade sana timu yako. Yaani back to back top four finish ndiyo yawe mafanikio kwa timu kama United! Duh, kwamba dunia inakimbia kasi kiasi hicho. Kwa hiyo unataka kumaanisha kuwa yule kocha wenu aliyewahi kusema 2018 kuwa malengo yenu wakati ule yalikuwa sawa na Everton!

Mimi nadhani zile timu traditional top six (ukiacha Arsenal) zinapaswa kuita mafanikio pale zinapochukua kikombe. Au walau kutinga fainali. Top four finish ni mafanikio kwa emerging teams kama Leicester, Everton, Wolves, Villa na akina West ham.

Nyie msilete visingizio, kipimo chenu ubingwa. Sisi tunaanza na Europa na Karagabaho kisha msimu ujao kocha wetu tutamwomba tena aende na kale karedio kwenye press conference.
 
Unfortunately wewe ni katika minority, majority ya mashabiki wa man U bado wanamuhitaji na board Pia inamuhitaji.

Swali la kizushi tu nani aje akiondoka yeye? Na kwa nini?
Uje ubongo wa kuweza kupambana na pep na klopp......kuhusu kocha mwenye huo ubongo mimi simjui ila wazo langu ndio ilo
 
Ndio ujue maisha yanaenda kasi sana leo raia zinafurahia kuingia top four mi najiuliza tu hii crisis tunayopitia si ndio madrid anapitia kipindi hiki lakini mbona perfomance yao ipo pale pale sisi wapi tulikosea.....ina maana hatukujiandaa kuachana na babu kipindi kile

Unajua kama mzaha mzaha tu ten years hii hapa bila ubingwa wa epl
 
Sisi timu yetu ina clear path ambayo Ole ameiweka na tunaifuata hio path na so far tupo mahala pazuri.

Tatizo lenu mashabiki wa kibongo mnapenda kufaidi end result Ila tabu za process haziwahusu, wengi wameanza kushabikia man U matunda ya Fergie wakati wanavuna Ila kipindi fergie anapanda wengi hawajui tabu zake zilikuaje.

Hao Liverpool na Klop miaka takribani mitano wamestrugle hadi nafasi ya 8 wameshika wakaja kufaidi matunda mbeleni.

Hao man city tushazungumzia mda humu, walianza kuandaa ujio wa kina pep miaka kibao nyuma, Tixi amekuja 2012 kama sijakosea that time Fergie bado yupo Man U, wakati fergie akitawala baadae Chelsea vipindi tofauti na Leicester wao wanajipanga wanasajili Watu wanaofit mfumo fulani Kina DE bruyne, fernandinho, Aguero, Silva, kompany na wengine kibao walisajiliwa zamani tu ila matunda yake ya nakuja kuonekana baadae baada kuwa na philosophy fulani.

Sasa kuna Watu wanajua utaleta kocha XXX halafu hapo hapo anachukua ubingwa tu, mpira hauna hivyo aisee usifikiri tu kupanga wachezaji 11 kunatosha...

Na ndio kinachofanyika sasa hivi, cultural overhaul, kukibadili kikosi kama man U inavyohitajika.
 
Sababu Spain hakuna ushindani, hata barca na Madrid ziwe mbovu vipi ngumu kutoka top 4.
 
Shaw na rashford wanatengeneza uelewano mzuri sana
Tatizo Rashford mchoyo sana kwa wenzake. Crystal Palace wametuzoea sana. Game ya kwanza walitupiga 3. Hapa wachezaji wetu wanarukaruka tu. Sioni dalili za ushindi. Kama nammiss Pogba vile maana kuna nyakati aliibeba sana team.
 
Yaan namtaja James anaingia... ila sioni Greenwood anafanya nini leo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…