Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Ushindi wenu etihad ni kupoteza na kutupa point tatu kwa hiali kabla hatujawapelekea moto ..!
 
Saizi man utd wako wanafanya mazoezi ili waje kufungwa na city jumapili ..!

Life is not fair
 
mpaka tarehe 27/01/2021 ligi kuu ya uingereza ilikuwa bado ina mvuto, nakumbuka ilifikia hatua timu ikiwa itapoteza alama 4 ndani ya mechi 2 basi inateremka mpaka nafasi ya 5. Tafsiri yake ni kwamba takribani timu zote zilikuwa na utofauti mdogo sana wa alama na hii ilitokanwa zaidi na ukosefu wa ushindi mfululizo.

udhaifu wa liverpool na manchester city mwanzoni mwa msimu ndio kulitupa fursa ya kuonekana wapigania kombe lakini ndoto hiyo kwa makusudi imefutwa.
  • unafungwa na sheffield = point 3
  • unatoa suluhu na everton ambayo umeifunga mechi mbili mfululizo uwanjani kwao = points 2
  • unatoa suluhu na arsenal = points 2
  • unatoa suluhu na west bromwich = points 2
hizo mechi zitaendelea kuniumiza kadri nitakavyoendelea kuzikumbuka, laiti kama man city angelituzidi kwa alama 6 bado ushindani ungelionekana dhahiri.
hata tulipofika kwa washambuliaji wetu tulionao ni afadhali, uko na rashford anapata mpira wa kusukuma ata kwa upepo tu uingie, anaanza kuvuta mpira kududi nyuma, anamtafuta martial ambaye anakua kama anasubiri mpira umfuate (poor positioning) tunahitaji clinical finishers kuliko hawa tulio nao, ndio tunatengeneza nafasi za kutosha lakini tunamtengenezea nani hizo nafasi?
 
Nasikia kwenye mkataba mmeweka kipengele cha kuto nunuliwa huko westham ,mlijua kama atakiwasha hahaaaaaa
...!

United haiwezi Fanya biashara na city kwa sawa ...

Sema united haijui inataka nin Lingardinyo anaenda westham anatupia magoli ila united mlikuwa mnamuona useless ...
Lingard ni "super sub" anayeweza kukupa vifuatavyo;

1. Maamuzi ya papo kwa papo (ni mwepesi kufikiri haraka). Muda wote wa mchezo akili yake iko pale.

2. Anajituma. Atakupa kila dakika.

3. Ana kasi muda wote. Hivyo ukimwingiza dk 30 au 20 za mwisho atawakimbiza sana mabeki waliochoka. Unamkumbuka Ji Sung Park?

4. Hachoki kukaba. Hivyo dk za mwisho ikiwa unataka kulinda matokeo atakupa advantage kiulinzi na kiushambuliaji (counter attacks).

Wasiomjua vema Lingard (akiwemo kocha) wanaangalia udhaifu mmoja tu alio nao; "quality". Pamoja nakujituma sana kijana hana ubora mkubwa miguuni. Hawezi kupiga chenga hata moja one on one.

Hivyo ni makocha wanaojua tu wanaoweza kumtumia vema. Kumtoa Lingard na kuwaacha James na Mata kunaonesha kiwango cha kocha kikoje.

Lingard amewasaidia kuua michezo kadhaa ukiwamo ule wa City.
 
Kwa mwenendo huu wa Rashford pamoja na mwenzake Martial,nadhani ni wakati muafaka wa kuirudisha mezani hoja ya uwezo sahihi wa hao madogo wawili kama kweli wanaweza kutubeba msimu ujao au tunaendelea kucheza kamari na kumuachia Pep atuadhilishe atakavyo.

Ningependa kuona madhaifu ya mwalimu yanafichwa na ubora wa wachezaji wake kama alivyofanya Zidane na Madrid yake kabla CR7 hajawa historia pale bernabeu,lakini mapenzi ya Ole kwa hawa vijana ndio yatamfukuzisha pale OT.
Martial hauziki kirahisi. Mbali na kuwa kipenzi cha kocha ni kipenzi pia cha Ed Woodward kibiashara. Ukiacha kuwa kipenzi cha mashabiki na hivyo kuuza sana, deal yake kutoka Monaco inaipa disadvantage United mauzo yanapofanyika.

Akiuzwa United na Monaco zitagawana pasu kwa pasu faida yoyote inayopatikana kwa kuzingatia bei aliyonunuliwa. Ni kama ilivyo kwa deal ya De Gea na Atleti. Hivyo wapenzi na mashabiki mjifunze tu namna ya kuishi na vijana hao.

Kuhusu Rashford pale ndiyo kwao.
 
mpaka tarehe 27/01/2021 ligi kuu ya uingereza ilikuwa bado ina mvuto, nakumbuka ilifikia hatua timu ikiwa itapoteza alama 4 ndani ya mechi 2 basi inateremka mpaka nafasi ya 5. Tafsiri yake ni kwamba takribani timu zote zilikuwa na utofauti mdogo sana wa alama na hii ilitokanwa zaidi na ukosefu wa ushindi mfululizo.

udhaifu wa liverpool na manchester city mwanzoni mwa msimu ndio kulitupa fursa ya kuonekana wapigania kombe lakini ndoto hiyo kwa makusudi imefutwa.
  • unafungwa na sheffield = point 3
  • unatoa suluhu na everton ambayo umeifunga mechi mbili mfululizo uwanjani kwao = points 2
  • unatoa suluhu na arsenal = points 2
  • unatoa suluhu na west bromwich = points 2
hizo mechi zitaendelea kuniumiza kadri nitakavyoendelea kuzikumbuka, laiti kama man city angelituzidi kwa alama 6 bado ushindani ungelionekana dhahiri.
Bado hajafukuzwa tu...
 
Inter Milan failed to pay #mufc a bonus for the Romelu Lukaku transfer, triggering a clause that will force them to immediately pay the remaining fee of the deal. United are asking for Lautaro Martínez or Milan Škriniar to balance the deal. [
@CorSport
]
 
Ushindi mwembamba leo kisha kipigo jumapili..hiyo ndo curve yetu.

Chief-Mkwawa leta stats..nini kimetokea mbona City wametupita kama upepo vile?
 
nimejiuliza maswali:
  1. Je tukimsajili jack grealish na sancho ndio tutakuwa tumefanikiwa kutatua tatizo la umiliki wa mpira?
  2. mbona van gaal aliweza kujenga team yenye uwezo wa kutawala possession licha ya kuwa na wachezaji wa kawaida hususani wa kiungo, kwa nini wengine waliomfuata wanashindwa na uwanja wa mazoezi bado ni ule ule?
================================
rudi kaiangalie timu ya xavi hernandez jinsi inavyocheza, je tuseme wale waarabu wana wachezaji bora kuliko manchester united?
matatizo ya umiliki mpira ni ya mwalimu na falsafa zake na si wachezaji.
Kwn nyie mnaosema Man utd haimiliki mpira mnaiangalia ktk angle ipi?
 
Scot na Fred siyo wabovu sana katika passing ukilinganisha na midfielders wengine

Kikubwa wanatakiwa waimprove katika foward passing na kuipandisha timu mbele badala ya kusubiri Bruno aamue mpira uende wapi.

Striking force yetu inapoteza nafasi nyingi sana kuliko msimu uliopita sijajua kuna nini kina wasumbua mastriker wetu.

Msimu uliopita timu yetu ilikuwa inatengeneza nafasi chache sana za kufunga magoli lakini tulikuwa clinical sana kwenye chances conversion.

Pattern yetu ya uchezaji haieleweki ndiyo maana hatuonekani kuwa mwelekeo mzuri kwenye uchezaji tunacheza kwa kubahatisha bahatisha tu this is down to coaching.
Leo umeongea mkuu.
 
Kwn nyie mnaosema Man utd haimiliki mpira mnaiangalia ktk angle ipi?
ukisoma vizuri comment ya huyo member niliyemnukuu utapata tafsiri ya aina gani ya soka analolihitaji.
anataka umiliki wa mpira wa dakika 1 hadi mbili


anataka tuwe kama hivi kila mechi bila ya kuangalia mpinzani, kudominate match isiwe dhidi ya under dog pekee
 
Ushindi mwembamba leo kisha kipigo jumapili..hiyo ndo curve yetu.

Chief-Mkwawa leta stats..nini kimetokea mbona City wametupita kama upepo vile?
Mimi ndio nimechanganyikiwa kabisa kwa kilichotokea halafu humu watu wakajisahaulisha makusudi tulivyopitwa wakawa wapo bize kuwananga livapool.....kuja kushtuka pointi kumi tumeachwa jamani inauma hii kitu acheni tu......mi ndio maana kauli yangu moja tu "bado hajafukuzwa tu"......sosha hajakaa kiubingwa kabisaaaaa
 
Back
Top Bottom