Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Game ya kesho ni kipimo tosha cha kujua timu yetu imefika wapi.

Sorkskjaer ahakikishe points 3 anarudi nazo kama anahitaji kumaliza ndani ya big 4.

Ukizingatia msimu huu hatujashinda kwenye game yeyote na timu ngumu pale EPL swala ambalo baadhi ya mashabiki wamekua wakitilia wasiwasi na uwezo wa Sorkskjaer, so kwa kukata mzizi wa fitina kesho anatakiwa aje na dawa ya tatizo.

Kosa pekee atakalo fanya ni kumuweka nje Bailey na kuwaanzisha Maguare na mwenzie Lindelof, hapo tukipoteza nitamlaumu kocha.


Akibidi aje hivi


Cavani
Rashfood Fernandez Greenwood

Fred Tomney

Show Bailey Maguare Wan be Saka.

Degea.
Cavani na Scot ni majeruhi hivyo hawatacheza kesho.

Tuna mechi ngumu sana kesho hasa ukizingatia record ya chelsea recently.

Kikubwa tujitahidi kutumia nafasi chache tutakazozipata lakini tuombe Matic na Fred wawe form kidogo kuwalinda mapazia yetu kule nyuma.

I would opt for 3 centre backs lakini wing ya kulia tumtumie Daniel James kumzuia Marco's Alonso asipande sana.

Kushoto I would opt for Telles halafu Shaw aje aunde 3 centre backs.

Katikati Fred and Matic ni lazima watakuwepo kwa sababu wengine wote ni majeruhi.

Left wing acheze Rashford ili Reece James asipande sana na Kovacic awe busy kuweka cover shadow badala ya kudictate game.
 
Game ya kesho ni kipimo tosha cha kujua timu yetu imefika wapi.

Sorkskjaer ahakikishe points 3 anarudi nazo kama anahitaji kumaliza ndani ya big 4.

Ukizingatia msimu huu hatujashinda kwenye game yeyote na timu ngumu pale EPL swala ambalo baadhi ya mashabiki wamekua wakitilia wasiwasi na uwezo wa Sorkskjaer, so kwa kukata mzizi wa fitina kesho anatakiwa aje na dawa ya tatizo.

Kosa pekee atakalo fanya ni kumuweka nje Bailey na kuwaanzisha Maguare na mwenzie Lindelof, hapo tukipoteza nitamlaumu kocha.


Akibidi aje hivi


Cavani
Rashfood Fernandez Greenwood

Fred Tomney

Show Bailey Maguare Wan be Saka.

Degea.
Mechi ya kesho inauwezekano mkubwa sana wa kutoa sare.
 
Ole vs PSG 4 games 2 Wins.
Ole vs Man City 8 games 3 wins 3 defeats 1 draw.

Ole vs Liverpool 5 games 2 defeats 2 draws 1 win

Ole vs Chelsea 5 games 1 defeat 3 Win one draw.

Total wins 9
Defeats 8
Draws 4.

Takwimu zake against big games siyo mbaya kama unachotaka kuonyesha.

Msimu huu alone ndiyo hana record nzuri against big teams lakini nazo kafungwa mara moja tu na Man city kwenye kombe la EFL
 
  1. suluhu dhidi ya liverpool, ok unaweza kusema liverpool bado ilikuwa ni timu tishio pale anfield
  2. suluhu dhidi ya everton, hii ilikuwa ni suluhu yenye kuzuilika kwa sababu tulikuwa mbele kwa magoli mawili na baadae tukawa mbele tena kwa goli la 3
  3. kufungwa na sheffield
  4. suluhu dhidi ya west bromwich huku tukiendelea kuonyesha udhaifu dhidi ya low blocks setup
  5. suluhu dhidi ya arsenal iliokosa huduma ya saka na aubameyang
  6. tumekuwa tukicheza ovyo second half na hata namba ya ufungaji wa magoli imekuwa ikipungua, rejea mechi ya west bromwich, sheffield baada ya kuwarejeshea goli, everton baada ya kuwafunga goli la 3
utofauti wa points 10 dhidi ya manchester city umetokea hapo na si kwamba walituacha tokea mwanzoni mwa ligi kama ilivyozoeleka misimu iliopita.
wiki 8-10 nyuma manchester city walikuwa wanashika nafasi ya 9 huku wakiwa na mechi 1 mkononi, tafsiri yake ni kwamba walikuwa na form mbovu ya kiuchezaji mpaka wachambuzi wakawa na wasiwasi na pumzi ya guardiola na kikosi chake.

wiki za mbeleni man city wakaongoza wao ligi kwa alama 7 huku wakiwa na mechi moja mkononi (kabla ya kucheza na everton), kwa takribani mechi 7 hadi 10 manchester city wamecheza wakiwa wanakosa huduma ya mshambuliaji, changamoto hii ndio imeibua ubora wa manchester city (tatizo wameligeuza fursa) hatimaye wamekuwa wakibadilisha shapes tofauti za kiuchezaji (mara 3-4-3, 3-3-4) ndani ya uwanja mpaka kuzalisha unbeaten run kwa takribani mechi 21.

mechi nyingi za karibuni tunaziamua kutokana na jinsi adui anavyoamka (angalia jinsi sociedad walivyokuja tofauti dhidi yetu, najua tutasingizia kupata matokeo bora kwa mechi ya kwanza),

atleast ilihitajika liwepo gapes la pointi 4 na si 10 kwa sababu sisi hatujapata tatizo la majeruhi kwa wachezaji wetu muhimu ukilinganisha na man city, leicester city na liverpool.

mwalimu wetu ana muhali (woga wa msimamo dhidi ya wachezaji wazembe)
Hizi ndiyo mechi tulizopotezea mwelekeo.

Timu yetu ikifanya vizuri mechi mbili wachezaji wanarelax tunapoteza wanaanza upya tena.

Last season nilisema tunapoteza mechi kwa sababu ya laissez faire attitude ya mwalimu.
 
Kipindi season inaanza Mimi sikuwa na matarajio ya Man U kupambania ubingwa.

ManU alipokuwa kileleni kwa tofauti ya Pointi 3. Bado sikuwaza United inaweza kuchukua ubingwa.

Nilitegemea Man City au Liverpool mmoja akae juu ya msimamo Kisha Man U iwe second.
Ila Sasa kitu kinachouzi ni unawezaje kupoteza point tano dhidi ya timu zinashika mkia(Shelfield + West Brom)
Ingekuwa ni mechi moja tungesema ni a bad day in the office
Kweli unafungwa na timu ambayo katika mechi 20, imeshinda mechi 1, tena kwa goli la penalty.
Kwa kiasi kikubwa defence ndio imetuangusha, haiwezekani tufungwe goli 32.
Hata timu iliyonafasi ya kumi huko imefungwa idadi ndogo kuliko sisi.
 
Majeruhi hayamwangushi peke yake, mpaka mimi shabiki wake yana niathiri.

Pata picha angekua yuko fiti msimu mzima, akina Maguar & Lindelof wangekua wanagombea nambamba tu.
Uko kwao Ivory coast wanamloga na ukizingatia na uracist wa Ole ndo kabisa kiwango kinaporomoka.
 
kujadili mwenendo wa manchester united ni sawa kurejea kitabu ulichokwisha kisoma zaidi ya mara moja.
ari na hamasa kwangu imeondoka, ni bora niwe msomaji zaidi
Hili timu ni litakataka mkuu wala lisikupe presha za kijinga ..leo hili jitu litakufa..
#CFC
 
Ukiyakuta ma fan boys ya manure yanavyochambua timu lao
Sasa utadhani ni bonge la timu ..kumbe ni matapishi matupu..
Sasa angalieni tunavyowaonesha leo kuwa hii timu ni matapishi tu
#CFC
 
dirisha lijalo
  1. uza fred ikijitokeza team yenye ofa nzuri ya kuanzia paundi millioni 27 / mjadala mzito huu
  2. uza jesse lingard japo kwa paundi millioni 15
  3. antony martial apewe nafasi ya mwisho
  4. mkono wa kwaheri kwa juan mata
  5. ole apunguze mapenzi kwa phil jones,
  6. antonio conte akimuhitaji matic apewe (mzee wa kukusanya vizee)
baada ya makusanyo ya kusadikika
  1. kalvin phillips
  2. miguu ya jack grealish au mchezaji mwenye sifa zake
View attachment 1713136
Tetesi zipo hivi;

United walikataa kuweka kipengele cha kumuuza Lingard kwenye mkataba wake wa mkopo ambayo ilikuwa ni kwa £15M kwa makusudi akipata form yake wapige cha juu, kwa sasa Lingard thamani yake ni £20M.

Inasemekana United wanataka kumshusha Declan Rice mwenye thamani isiyopungua £50M na ikiwezekana kufanya swap deal na West Ham United kukamilisha usajili huo. Wakimuacha Lingard West Ham na kuna uwezekano akaongezwa Matic na Jones kwenye dili hilo.

Anthony Martial huenda huu ukawa msimu wake wa mwisho akiwa United, ni wazi akiuzwa United watakamilisha dili la Sancho kwa ada ya uhamisho isiyopungua £50M wala kuzidi £80M.

United pia wanataka kununua CB kutoka Sevilla, Jules Kounde. Pia RB kutoka Norwich City, Max Aarons mwenye thamani ya £35M anafukuziwa na United pamoja na Everton na Bayern Munich.

Msimu huu tunaweza kutoka hivi:

Buy
RICE - DM
SANCHO - RW
KOUNDE - CB
AARONS - RB

Sell
LINGARD
MATA
POGBA
MATIC
JONES

Siioni United ikimuuza Fred ambaye yupo on form na muhimu katika maslahi ya kikosi kipana cha United, zaidi naona Pogba akiondoka na kuachia nafasi kwa watu kama VDB. Kuondoka kwa Pogba hakutaathiri sana kikosi chetu kama tukikamilisha usajili wa DM.
Tukimpata Kounde na Aarons itakuwa tumefanya sajili muhimu sana katika eneo la ulinzi, Kounde siyo mwenye kimo kirefu wala kasi kubwa sana ila ni moja ya mabeki wa kati hatari.
Aarons ni one of the best attacking RB, huyu jamaa ataleta challenge kwa Bissaka. Jamaa anajua kupandisha mashumbulizi vizuri na kumwaga maji vizuri bila kusahau defending skills nzuri.

Mpaka hapo tukiongezea na Sancho tutakuwa tumemaliza kazi, Siioni United ikinunua striker kwa sasa kutokana mahitaji yetu muhimu. Cavani akiongeza mkataba tutakuwa vizuri bila Martial huku tukiwa na options za Rashford na Sancho kwenye wings pamoja na Greenwood kama ST nikiamini msimu ujao utakuwa wa kuanza kuitetea namba hiyo endapo Martial atauzwa.
 
Back
Top Bottom