- suluhu dhidi ya liverpool, ok unaweza kusema liverpool bado ilikuwa ni timu tishio pale anfield
- suluhu dhidi ya everton, hii ilikuwa ni suluhu yenye kuzuilika kwa sababu tulikuwa mbele kwa magoli mawili na baadae tukawa mbele tena kwa goli la 3
- kufungwa na sheffield
- suluhu dhidi ya west bromwich huku tukiendelea kuonyesha udhaifu dhidi ya low blocks setup
- suluhu dhidi ya arsenal iliokosa huduma ya saka na aubameyang
- tumekuwa tukicheza ovyo second half na hata namba ya ufungaji wa magoli imekuwa ikipungua, rejea mechi ya west bromwich, sheffield baada ya kuwarejeshea goli, everton baada ya kuwafunga goli la 3
utofauti wa points 10 dhidi ya manchester city umetokea hapo na si kwamba walituacha tokea mwanzoni mwa ligi kama ilivyozoeleka misimu iliopita.
wiki 8-10 nyuma manchester city walikuwa wanashika nafasi ya 9 huku wakiwa na mechi 1 mkononi, tafsiri yake ni kwamba walikuwa na form mbovu ya kiuchezaji mpaka wachambuzi wakawa na wasiwasi na pumzi ya guardiola na kikosi chake.
wiki za mbeleni man city wakaongoza wao ligi kwa alama 7 huku wakiwa na mechi moja mkononi (kabla ya kucheza na everton), kwa takribani mechi 7 hadi 10 manchester city wamecheza wakiwa wanakosa huduma ya mshambuliaji, changamoto hii ndio imeibua ubora wa manchester city (tatizo wameligeuza fursa) hatimaye wamekuwa wakibadilisha shapes tofauti za kiuchezaji (mara 3-4-3, 3-3-4) ndani ya uwanja mpaka kuzalisha unbeaten run kwa takribani mechi 21.
mechi nyingi za karibuni tunaziamua kutokana na jinsi adui anavyoamka (angalia jinsi sociedad walivyokuja tofauti dhidi yetu, najua tutasingizia kupata matokeo bora kwa mechi ya kwanza),
atleast ilihitajika liwepo gapes la pointi 4 na si 10 kwa sababu sisi hatujapata tatizo la majeruhi kwa wachezaji wetu muhimu ukilinganisha na man city, leicester city na liverpool.
mwalimu wetu ana muhali (woga wa msimamo dhidi ya wachezaji wazembe)