Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Mim binafs nilijua title contenders ni

Liverpool na man city


Kitendo cha liverpool kupoteana sioni kabisa mwingine wa kutusogelea city...

Mpaka sasa timu inayonipa hofu ni liverpool tu ,man utd haina madhara kabisa kwenye mbio zetu ...

Man utd huwa sina hofi nayo kabisa

Hata tukiwapa game 4 mshinde mchukue epl bado hamna uwezo sasa hiyo ni timu ...


Epl hiyoo inatua etihad kiulain kabisa

Nawakumbusha tu tulipokuwa ,wakat huu spurs alikuwa anashona suti za kusherekea ubingwa hhaaaaaa...

View attachment 1703088
New ferguson in epl
 
Pogba learnt it all from Messi and CR7...
IMG_20210215_211533_420.jpg
 
kwa hili jibu lako kwa mujibu wa swali alilouliza jamaa pale maana yake tuendelee kujaribu tena mpaka apatikane aliyesahihi??
Nimejaribu tu kumuuliza swali hilo..lakini Nagelsman akija United kwa sasa haiwezi kuwa sawa na Ole aliyetoka cardiff..Leipzig walikuwa semi-finalist wa Uefa msimu uliopita na pia at times wamecheza soka fulani safi huku bajeti ikiwa chini sana.
 
Nimejaribu tu kumuuliza swali hilo..lakini Nagelsman akija United kwa sasa haiwezi kuwa sawa na Ole aliyetoka cardiff..Leipzig walikuwa semi-finalist wa Uefa msimu uliopita na pia at times wamecheza soka fulani safi huku bajeti ikiwa chini sana.
Jombaa, Julian Nagelsmann yule ni mtu mwenye akili nyingi sana za kiufundi. Ana silaha kubwa sana tunayoikosa kitu ambacho makocha kama Pep Guardiola na Jurgen Klopp wanacho, GAME MANAGEMENT SKILLS.

Umuhimu wa game management skills Everton wasingeweza kupata sare wakati tunaongoza goli mbili bila siku ile. Tusingefungwa na PSG kabla ya Fred kupewa kadi. Ukiangalia vizuri safu yetu ya ufundi ni kama wanabahatisha bahatisha hawajui nini cha kufanya muda mchezo unapoendelea.

Kusema ukweli kama tutaendelea kuamini Ole atakuja kuwa kocha mzuri tunapoteza muda. Kwa sasa ni heri amalize msimu tupate nafasi ya top 4 msimu mpya aje mwalimu mpya pamoja na mkurugenzi wa ufundi.
 
Hivi bado kuna fans kwenye haya majukwaa wanaendekeza matusi? Nyie si ndio mnajiita watu wazima mmeanza kushabikia mpira toka 90? Naanza kupata mashaka na ushabiki wenu naamini kwa wingi mnaweza kuwadhibiti hawa watoto amvao naamini kwa asilimia 100 bado hawajawa na familia.
 
Waingereza huharibu wachezaji wao kwa kuwapa vichwa pale wanapochipukia. Hiyo huwafanya kujiona nyota kabla hata hawajawa nyota. Kilichotokea kwa Theo Walcott ndiyo kinatokea kwa Rashford na ndiyo kitatokea kwa Foden na kimekwishatokea kwa Greenwood.

Rashford anapoenda kupiga freekick kwa mfano, utasikia watangazaji wakimsifia kuwa na upigaji sawa na Ronaldo Cristiano! Ukiangalia Rashford kafunga freekick ngapi unabaki kuduwaa.

Nakumbuka mechi ya kwanza Danny Welbeck akiwa amepata nafasi baada ya Rooney kutokuwepo alifunga goli akashangilia kisupastaa. Siku ile ile Ferguson kumrudisha kwenye academy akasema anajiona mkubwa wakati bado sana. Ndiyo sababu Fergie aliweza kufanya wachezaji wake wa kiingereza kuwa wakubwa sana.

Lakini hawa wa leo akifunga goli moja tu vyombo vyote vya habari vinaanza kumfananisha na Ronaldo.
Mkuu umeongea vema sana. Na mfano mwingine ni Foden pale Man city,wakiwa wameshinda hata goli 3-4 na dogo akatoa assist au naye akatupia kambani maongezi yote kwa foden wakati Gundogan ndio anawaweka mjini kwa sasa.
Inakera sana yani.
 
Back
Top Bottom