★Tupo kwenye uchungu mzee maana kuna watu washaanza kusema OGS anatumia Jani
Huwa najiuliza kauli kama hizi OGS huwa anamwambia nani sana sana?
Hizi ni kauli za kuongelea uwanja wa mazoezi uko au wakati wa half time.
Sisi mashabiki tunataka sababu za kiufundi za kwanini timu haifanyi vizuri sio siasa uchwara zake
 
★One en Only Sir Alex Ferguson★

#GGMU

manutd |
IMG_20201123_160655_267.jpeg
 
Uwe na goal getters kama Lukaku, Chicharito, Berbatov, RVP.

Ndo maana nasema, Man Utd tunamuhitaji sana Haaland kuliko Sancho.View attachment 1633208
Hapana aisee tunahitaji winga wa kulia kuliko kitu chochote kile,

Huyo Haaland akija atakabwa vile vile sababu timu ipo predictable,

Nafkiri dunia nzima ni sisi peke yetu tunaocheza na fluid strikers bila mtu wa kulia.

Dortmund mastriker wengi wapo njema sababu ya kina Sancho, reus, hazard, brandt etc, angalia miaka nenda miaka rudi lazima utakuta Dortmund kuna wide players wazuri, kina Pulisic.

Unapokuwa na watu watatu mbele ambao wote ni hatari kufunga ina maana hata mabeki unawagawanya, hapa hata Striker akimvuta Beki mmoja pembeni ni rahisi mtu kama Bruno kufunga.

Ila ukicheza bila forward/winga wa kulia inamaana beki wa kushoto ama fullback wa kushoto anakuwa free muda wote na ku re enforce beki.

Fluid Attacks Zote Kuanzia BAle benzema na Ronaldo, Messi, Neymar na suarez hadi hii ya Mane, firmino na Salah lazima itimize huo utatu, huwezi kuwa fluid halafu utokee tu kushoto 99%.
 
Back
Top Bottom