Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Katika hiyo misimu lete kikosi cha Liverpool halafu uangalie na baada ya Klop kupewa mahitaji yake.

Muangalie na Ole baada ya kupewa mahitaji yake huku ikiwa limebaki eneo moja sanasana la RW.

Halafu rudi tena timu aliyoachiwa Klop na aliyoachiwa Ole halafu tujadili sasa.
Umeniwahi
 
Mkuu nimekuwa nikifuatilia sana maoni yako juu ya Ole una positive view sana kwake (which is good) na ni dhahiri upo upande wake. Una point nyingi za msingi kumtetea Ole na naheshimu hilo kwa mawazo yako ila Ole HAJUI!

Msimu huu 'Ole Boys' mnasema ni match fitness ndiyo imeleta matokeo mabovu; kwa 40% nakubaliana na mawazo yako ila 60% sikubaliani na wewe. Hii timu ya Ole haijaanza kupata shida ikicheza na timu ndogo msimu huu, tumeona last season ilikuwa ni kama vile timu kubwa tu ndiyo Ole anaziweza kwenye mbinu zake.

Kipindi cha Ole tumefanikiwa kusajili wachezaji wazuri sana ila amekuja kuonyesha ni jinsi gani bench lake la ufundi linaua vipaji.

Nakumbuka maneno ya vibanda umiza mapema msimu uliopita:

"Wan, two, three Bissaka"
"James the Flash"
"Maguire" hii wadau walikuwa wanaitamka Kiswahili kuonyesha msisitizo.

Leo hii imebaki story, yapo mengi mazuri Ole kafanya ambayo yananifanya nitamani abaki ila kwa machache mabaya anayofanya ndiyo chanzo cha United kufeli.

Ukienda Everton utakuta World class player mmoja sidhani kama kuna mwingine, nenda Leeds sidhani kaka kuna World class player. Ila ukirudi Manchester United utakuta kuna Pogba, De Gea, Bruno na wachezaji wengi wenye uwezo binafsi mkubwa ambao ukiunganisha uwezo wao ndiyo unapata timu ya kueleweka.

Mimi sililii mataji kutoka kwa Ole, nataka mpira unaoeleweka uwanjani. Makombe yatakuja tukiweza kucheza soka safi as a team na kila mtu ajue namba yake na mbinu za kocha ibaki ku-deliver tu uwanjani.

Test yangu kwa Ole ni game ya Newcastle, hawa ni the likes of Crystal Palace na Brighton. Sasa hivi sitegemei kisingizio cha fitness sasa hivi mtatuambia shida ni wachezaji au mbinu na ufundishaji wa kocha.
Kwa kuzingatia hoja yako niliyoquote kule juu, je tukitwaa kombe lolote msimu huu itakuwa ni kwa sababu ya mbinu za Ole au ni juhudi binafsi za wachezaji ?

Je iwapo tutashinda mechi ya New Castle itakiwa ni kwa sababu ya mbinu za Ole au juhudi binafsi za wachezaji ?

Sent from my SM-A105F using JamiiForums mobile app
 
Yaani kwa kifupi wadau wanamaanisha hawana imani tena na Ole na ikitokea timu ikashinda inakuwa imeshinda kwa kujituma na uwezo binafsi Wa wachezaji na si mipango ya mwalimu. Na ikitokea imefungwa basi si kitu cha kushangaa Mana uwezo Wa mwalimu si Wa kushinda! Kwa maana nyingine kwa sasa ile timu inapocheza, pale kwenye benchi awepo kocha au asiwepo ni sawa tu!
Kwani huwa wanajitrain peke yao wachezaji kule mazoezini ?

Sent from my SM-A105F using JamiiForums mobile app
 
Hapa hata mimi nakuunga mkono. Huyu Mikel Arteta watu watamkataa kabla hata msimu huu haujaisha.
Yawezekana akaendelea vizuri hata kwa msimu mzima bila shida baadae mambo yakaenda hovyo.

Pep Guardiola huu ni msimu wake wa pili anachezea vichapo msimu uliopita Man city alifungwa mechi nyingi kuliko alizofungwa Ole lakini hatuoni watu wakimshambulia Guardiola.

Claudio Ranieri aliipa ubingwa Leceister City msimu uliofuata alifukuzwa timu ikiwa imebakiza mechi 10 za ligi ikielekea kushuka daraja.

Kwahiyo kuanza vizuri kwa kocha siyo hoja atamalizaje ni jambo la msingi.

Sent from my SM-A105F using JamiiForums mobile app
 
Mkuu elewa walifukuzwa,,,
Labda utwambiye wewe ,,kwann ole asifukuzwe?
Nikukumbushe tu Van Gaal alifukuzwa kwa sababu mbili.
1. Kushindwa kuingia top four kwenye UCL.

2 Alipoteza ushawishi dress room hasa kwa senior players.

Mourinho alifukuzwa kwa sababu tatu.
1. Kutofanya vizuri mfululizo mechi kuanzia August mpaka December timu ikiwa nafasi ya 12.

2. Kupoteza ushawishi dress room kwa kugombana na kila mchezaji mfano Pogba, Martial, na Juan Mata.

3.malalamiko ya kila mara na Board kwenye media.
Mourinho alichangia sana kuturnish image ya board ya united.

Sent from my SM-A105F using JamiiForums mobile app
 
Hivi ingetokea tungeshinda mechi zote za mwanzo!
Tungeletewa wachezaji?
Hivi watu hawashtuki na mara hii mashabiki tumesahau!
Wakati wa usajili, board walikuwa kama wako chooni wanakunya, ubabaishaji mwingi.
Kabla ya game na sevilla europa, akina matic walikuwa wanamuuliza ole, vp sancho anatua au niaje!
Ole alikuwa anawapa moyo, ni hela nyingi lakini subira ni muhimu.
Hivi imagine wewe ndiyo mchezaji, unajituma kwa moyo wote, mnaambiwa mkiingia UCL, salary zenu zinarudi, bonus ya kutosha, na kikosi kitaimarishwa, ghafla bin vuu dirisha la usajili kimya!
Morali lazima iwe chini hata kama mna wachezaji wa vipaji wa sayari gani.
Board ya man utd ina mambo ya kijinga sana, ole hana kosa.
Tena ole namuona ni kocha anayejua mikakati zaidi ya ki mgt kuliko makocha wengi wa sasa.
 
Nimeangalia Record za Klop na Ole toka wamekuja Epl, klop ameshika hadi nafasi ya 8, imemchukua hadi misimu 4 kuja kushika hio nafasi ya 2. Ole ameweza kushika nafasi ya 3 ndani ya misimu miwili tu. Alichofanya Ole Ndani ya misimu miwili Klop alishindwa kukifanya Misimu 4 ya mwanzo, ila Bado ole hafai.

Class ya mashabiki wetu ndio ilipo siku hizi, kocha anafaa au hafai kwa mihemuko ya mechi moja moja na sio target ya timu.
Kabla hawajafika England Klopp tayari alishachukua ubingwa wa Bundesliga(one of the best league in Europe after LaLiga & EPL) back to back mbele ya Bayern na kuingia fainali ya Champions league tofauti na OGS aliyekuwa anafundisha Norway (ignore mambo ya Cardiff)
Klopp na OGS wote walipewa timu katikati ya msimu lets compare them msimu uliofuatia ambao walisajili/kuuza wachezaji wakaenda pre-season msimu ambao Klopp alifanya vibaya alimaliza EPL na point 75 linganisha na OGS ambaye amemaliza na point 66 ukiangalia Klopp kulikuwa na progress inaonekana (style ya kucheza & matokeo) point 76 akaja 75 akaja 97 akaja 99 then angalia magoli ya kufunga/kufungwa na mechi walizofungwa .OGS (club legend) won us Champions league as a player but kwenye ukocha United sio size yake hakuna progress kwenye matokeo wala style of play
 
Sawa utashinda. Unajua hii mechi itakuwa ni battle ya wachezaji wenyewe na akili zao maana makocha wote weupe tu, Arsenal ukitoa vile vipasi hamna jipya. Timu yako ni mbovu na muda ukifika utajua.
Eti vipasi,, Endelea Kusubiri Treni Airport..

Kwasasa Timu yetu inacheza kwenye pattern inayoeleweka , Timu inakimbia ,inakaba na kushambulia kwa pamoja ...

Unafananisha na timu yako Hata Kukimbia ,kufanya buildup hawawezi ....

IMG_20201011_174331_573.JPG
 
Nikukumbushe tu Van Gaal alifukuzwa kwa sababu mbili.
1. Kushindwa kuingia top four kwenye UCL.

2 Alipoteza ushawishi dress room hasa kwa senior players.

Mourinho alifukuzwa kwa sababu tatu.
1. Kutofanya vizuri mfululizo mechi kuanzia August mpaka December timu ikiwa nafasi ya 12.

2. Kupoteza ushawishi dress room kwa kugombana na kila mchezaji mfano Pogba, Martial, na Juan Mata.

3.malalamiko ya kila mara na Board kwenye media.
Mourinho alichangia sana kuturnish image ya board ya united.

Sent from my SM-A105F using JamiiForums mobile app
Bado hujatueleza kwann ole asitimuliwe
 
Hivi ingetokea tungeshinda mechi zote za mwanzo!
Tungeletewa wachezaji?
Hivi watu hawashtuki na mara hii mashabiki tumesahau!
Wakati wa usajili, board walikuwa kama wako chooni wanakunya, ubabaishaji mwingi.
Kabla ya game na sevilla europa, akina matic walikuwa wanamuuliza ole, vp sancho anatua au niaje!
Ole alikuwa anawapa moyo, ni hela nyingi lakini subira ni muhimu.
Hivi imagine wewe ndiyo mchezaji, unajituma kwa moyo wote, mnaambiwa mkiingia UCL, salary zenu zinarudi, bonus ya kutosha, na kikosi kitaimarishwa, ghafla bin vuu dirisha la usajili kimya!
Morali lazima iwe chini hata kama mna wachezaji wa vipaji wa sayari gani.
Board ya man utd ina mambo ya kijinga sana, ole hana kosa.
Tena ole namuona ni kocha anayejua mikakati zaidi ya ki mgt kuliko makocha wengi wa sasa.
Kama unani shawishi vilee!!!!
 
★Mkuu ko ole anaonyesha hana kitu akipewa Muda???★
Hata kama ilimchukuwa miaka 10 ,,lakini tangia mwanzo alionyesha ana kitu cha ziada kuwapa spurs kama akipewa muda.
Ole has proved already ,,,he has nothing more to give for man u..
 
Back
Top Bottom