Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Jamani hakuna haja ya malumbano, mtu anayeharibu furaha yetu ni Ed Woodward hata aje kocha gani pale Manchester United bado nyumba imeoza ndani. Hii nafasi ya Ed inahitaji mtu smart sana anayeweza kujenga timu nzuri pasipo kuwaza kutumia pesa zaidi. Ed ndiye mtu responsible ku-assemble talents zote from coaching staffs to recruitment team, sasa unapokuwa na mtu mwenye uwezo mdogo kuunganisha hivi vichwa vifanye kazi kwa ufasaha ni shida. Hata akiajiri director of football as long as ana-report kwake ktk chain of command bado ni kazi bure.

Kama kuna watu ni wapenzi wa mpira wa kikapu utaona kuna mtu yupo Toronto Raptors anaitwa Masai Ujiri jinsi anavyoitendea haki ile nafasi yake ya u-rais wa timu ile ni same model hata football executive anaweza akawa ana-manuvre timu yake kwa akili kubwa pasipo kutumia pesa sana ktk usajili. Timu hujengwa kwa mikakati na sio taswira ya kibiashara sana. Pesa huja ukianza kufanya vizuri. Uunganisha kwanza talents (coaches & recruitment teams) zinazoweza kuleta wachezaji sahihi na kwa wakati sahihi na sio kuwa watu wenye ufikiri finyu na sio ajabu sokoni tunatangaza nia na hatuwezi ku-strike deal hata moja.
Kumlaumu Woodward ni kumuonea tu saivi. Jamaa ametumia hela nyingi kununua wachezaji ambao walikuwa talent kabisa. Ishu ilokuwepo ni kocha, ukweli usemwe tu, ni MBOVU hajui analolifanya uwanjani wala analotaka. Wachezaji alokuwa nao ni wa kuhakikisha ushindi na kufungwa ni bahati mbaya tu. Watu wanajichezea tu uwanjani watakavyo na kocha anatizama tu.

OGS atoke tu, Man utd sio timu ya kuwa na manager ambae level zake ni za kufundisha Cardiff. Ushindi wetu kazi kutegemea penalties tu!
 
MAGEREZA UNITED
IMG-20200908-WA0008.jpeg
 
Back
Top Bottom